saidoo25
JF-Expert Member
- Jul 4, 2022
- 602
- 1,407
WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa ametangaza rasmi bungeni kusitisha zoezi la uvishaji hereni mifugo baada ya kubaini upigaji wa Shilingi Bilioni 8.8 uliofanywa na Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mashimba Ndaki.
Kwa mujibu wa Majaliwa hadi sasa jumla ya Ngombe 5,068,616 zimeshawekewa hereni hizo ambazo wafugaji wanauziwa kwa Shilingi 1,750 kwa kila ng'ombe mmoja
Ufisadi huu ulilalamikiwa kwa muda mrefu na wafugaji wengi lakini Waziri wa Mifugo, Mashimba Ndaki alishupaza shingo na kuendelea na msimamo wa kuendelea kuwaibia wafugaji huku akiwatangazia vitisho mbalimbali ikiwemo kufungwa au kupigwa faini ya shilingi milioni 2 kila ngombe atakayekuwa hana hereni.
Hadi Waziri Mkuu anasitisha zoezi hilo tayari Wafugaji wameshapigwa Bilioni 8.8 ambapo hadi sasa hawajui hatma ya fedha zao hizo baada ya agizo la Waziri Mkuu kusitisha mpango huo.
Mashimba Ndaki kwa muda mrefu sasa amekuwa akilalamikiwa kwa utendaji mbovu hasa kushindwa kusimamia Wizara hiyo na kujitika kwenye jambo moja tu la kuhamasisha uvishaji hereni mifugo
Huku Wafugaji wakikabiliwa na matatizo mengi ikiwemo ukosefu wa malisho, mifugo kufa kwa kukosa chanjo na madawa, migogoro kushamiri ambapo wafugaji wamekuwa wakiuawa na wakulima maeneo mbalimbali nchini lakini yote hayo Waziri ameshindwa kuyashughulikia amejikita kwenye suala moja tu la kuuza hereni.
Heko Majaliwa kwa kubaini upigaji huu mkubwa uliofanywa na Waziri Ndaki kuwaibia wafugaji masikini Bilioni 8.8 hii ni Kashfa kubwa sana tunaamini Mama akirejea kutoka China atachukua hatua dhidi.
Kwa mujibu wa Majaliwa hadi sasa jumla ya Ngombe 5,068,616 zimeshawekewa hereni hizo ambazo wafugaji wanauziwa kwa Shilingi 1,750 kwa kila ng'ombe mmoja
Ufisadi huu ulilalamikiwa kwa muda mrefu na wafugaji wengi lakini Waziri wa Mifugo, Mashimba Ndaki alishupaza shingo na kuendelea na msimamo wa kuendelea kuwaibia wafugaji huku akiwatangazia vitisho mbalimbali ikiwemo kufungwa au kupigwa faini ya shilingi milioni 2 kila ngombe atakayekuwa hana hereni.
Hadi Waziri Mkuu anasitisha zoezi hilo tayari Wafugaji wameshapigwa Bilioni 8.8 ambapo hadi sasa hawajui hatma ya fedha zao hizo baada ya agizo la Waziri Mkuu kusitisha mpango huo.
Mashimba Ndaki kwa muda mrefu sasa amekuwa akilalamikiwa kwa utendaji mbovu hasa kushindwa kusimamia Wizara hiyo na kujitika kwenye jambo moja tu la kuhamasisha uvishaji hereni mifugo
Huku Wafugaji wakikabiliwa na matatizo mengi ikiwemo ukosefu wa malisho, mifugo kufa kwa kukosa chanjo na madawa, migogoro kushamiri ambapo wafugaji wamekuwa wakiuawa na wakulima maeneo mbalimbali nchini lakini yote hayo Waziri ameshindwa kuyashughulikia amejikita kwenye suala moja tu la kuuza hereni.
Heko Majaliwa kwa kubaini upigaji huu mkubwa uliofanywa na Waziri Ndaki kuwaibia wafugaji masikini Bilioni 8.8 hii ni Kashfa kubwa sana tunaamini Mama akirejea kutoka China atachukua hatua dhidi.