everybody
JF-Expert Member
- Oct 30, 2010
- 337
- 103
Mara kadhaa nimesoma habari kwenye magazeti na huku kwenye great thinkers (Jamii Forum) na kuona kwamba tunaendekeza majadiliano ya udini ambayo yanabomoa zaidi ya kujenga ka nchi ketu ka Tanzania. Jamani embu tuongelee vitu kwa fact. Population ya Tanzania kwa kadiri ya takwimu za 2009 ilikuwa na 62% Wakristo, 35% Waislam and 3% other religions. At the same time 97% ya population ya Zanzibar in Waislam. Sasa kama CHADEMA ni cha wa Kristo tu au kina udini si kingekuwa kimeshinda uchaguzi huku bara mwaka 2010?!!! Mimi nasupport kwa upande wa Wazanzibar kwamba uislam umetawala na hii ni kutokana na historia. Sasa tusitake kulazimisha Tanganyika nayo iwe na dini moja ambayo ndo inatawala. Embu tuacheni siasa ambazo hazina tija kwa nchi yetu. Mbona kuna wabunge waislam na wameshinda ubunge kupitia CHADEMA? Kama tunataka kuijenga Tanzania tuanzie hata huku kwenye JF. Tuache ushabiki ambao unabomoa nchi unless kama tupo kisiasa zaidi hadi huku kwenye JF. Mimi ningeshauri kwamba kwa vile hii JF ina great thinkers tusi support au kuchangia majadiliano ambayo yanazidi kutugawa zaidi. Sitaki kuamini kwamba kuna chama ambacho kipo kwa ajili ya dini fulani tu unless kama chama chenyewe kimedeclare hivyo. Tuvipe vyama vyote usawa and neutrality kwenye mambo ya udini, ukabila na rangi kama tunataka kukuza democracia kwa nchi yetu ya Tanzania.
Ni mtazamo tu.
Ni mtazamo tu.