Maisha yanakwenda Speed sana, Leo eti CCM hawaiamini TAKUKURU wala Mahakama

Elli

Platinum Member
Mar 17, 2008
55,180
85,340
Namalizia Wine yangu nirudi nikalale! Nikakukumbuka hili, nikaona wine yangu isiishe bure.

Eti MATAGA leo ndio wanailalamikia PCCB, POLICE na Mahakama kuwa "hawamtendei haki" Sabaya!

Nikacheka sana sana, hakika kuna nyakati za kulia na kuna nyakati za kuomboleza.

Yaani hawa Walioitwa Wazalendo, wenye Wabunge 99.9%, wenye Viongozi wote kuanzia kwenye shina hadi Taiga, Wenye Police na Green Guard, LEO NDIO WANALIALIA HIVI?

HAKIKA MUNGU anaipenda Tanzania. Tanzania ni zaidi ya CCM
 
Ushirika wa wachawi haudumu, pia ikumbukwe there's no honor among thieves.

Ccm wote Ni wezi na majambazi, mafisadi hakuna msafi kuanzia top mpaka bottom wote wananuka kila aina ya ubaya
 
CCM itabaki kuongoza nchi miaka na miaka
Kama ambavyo mlivyokua mnapendekeza aongezewe Muda atawale maisha/milele ...

... nia ilikuwepo, nguvu ilikuwepo, uwezo ulikuwepo, mamlaka ya kutimiza hilo yalikuwepo lakini haikuwezekana ... !!!

Vivyo hivyo CCM pengine inawezekana akishindwa kuongoza nchi baada ya mwaka huu kuisha

Katika mazingira hayo sisi waislamu huwa tunasema ALLLAHU YA'AALAM (Mwenyezi Mungu ndie ajuae)
 
Kwani CCM imetoa TAMKO kuwa hawaviamini hivyo VYOMBO?!!

CCM tuko wengi tu....Binafsi ninaviamini vyombo vyetu.....

Usituingize wote kwenye KAPU MOJA kama ambavyo si wote wanaoendelea kusimamia kuwa "Mh.Hallima Mdee na wenzake ni wanachama wa CHADEMA".

#KaziInaendeleaKwaKasiYaKutisha
#DieHardFanOfCCM
#StaunchSupporterOfSSH
 

Similar Discussions

21 Reactions
Reply
Back
Top Bottom