Maisha yamenishinda, vita imenishinda

Just relax, chukua glass ya maji unywe kupoza hasira na umkemee shetani,,, ikibidi ujambe kwa nguvuu....


Relax nniga maisha ndani ya Tanzania ya viwanda ni matam sana kuliko huko unako tamani kwenda wakati hukujui,, changamana na watu, fanya kazi sana, sikiliza mziki, kula sana ushibe ukiwa umechoka utasinzia na kusahau yalo pita.


Kukata tamaa nalo ni kosa kwa mungu broh,, jitahd saana hata kwenda kanisan/msikitini kutubu dhambi hizo ili shetan akuondolee majaribu hayo


Nasema tena, maisha ndan ya tanzania ni matam sana,, ila jikaze sana na ujitahd furaha yako isitegemee kutoka kwa mtu flan, tengeneza fraha we binafs. Pia usiwe mwema sana kuliko kuwa mwema kwako binafsi maana wapo wasio na shukrani
Music is
 
Mods. Mtafuteni huyu jamaa apewe msaada.

Atakiua huyu kimzaha mzaha
Nadhani wamiliki wa JF wameamua kuwa na policy ya kutotaka kujihusisha kwenye mambo ya aina hii yanayohusu their members (na kimsingi kwa sababu wao ndo wamiliki wa platform, wana haki hiyo).
Nilijaribu initiative ya kwanza kujaribu kuwa na njia za kuweza kusaidia au kuwaunganisha na msaada watu watakaopost vitu vya aina hii na wengine watakaoonyesha dalili za hivi, i met with JF leadership tukiwa na wadau wengine, tukakubaliana mambo fulani fulani.... Ila hayakufanyika, kukawa tu na ukimya, nikajaribu kukumbushia, ukimya ukazidi, nikiwa kama mtu mzima nikaelewa maana ya ule ukimya, nikaendelea na hamsini zangu.
Initiative ya pili pia ilikua ya kujaribu kusaidia vijana wenye hali fulani fulani, na yenyewe niliwasiliana nao vizuri, tukakubaliana mambo fulani fulani, ikaishia hewani, nikakumbushia mara nyingi kweli kweli, ukimya ukazidi kutamalaki, nikaelewa pia maana ya ule ukimya.
Kwa hiyo nadhani kama kuna anaefikiria kusaidia vijana wa hivi afikirie zaidi kufanya hivyo nje ya hii platform ya JF, kwa sababu inaonekana uongozi wa JF umeona labda it is not for the best interest of their platform kufanya hivyo; au kwamba negative effects kwao zitakua kubwa zaidi kuliko positive effects-as a company (which is very understable of course). It is sad kuwa hatuwezi fanya chochote juu ya watu wanaoonyesha dalili kama za mtoa mada (Hata tu kuweka "panick button").
Tusubiri tu kutoa RIP should the worst happen, as we have experienced previously.
Cc:
Maxence Melo
Mshana Jr
Moderator
 
Pole sana ndugu, changamoto kama haziji kwetu wanadamu unataka ziende kwa nani? nasikitika sana kuona mtu anafikia uamuzi wa kujitamkia kujiua huwa naona kama amefika mwisho, mwisho kabisa ule mwisho.

Mkuu wafikirie basi wanaokupenda, hauna watoto? wategemezi je?

Kama huna vyote hivyo, nakuomba kwa heshima na taadhima usijiue, wewe ni wa thamani na wa muhimu sana. Walau ubaki tusaidiane kulipa deni la taifa, tafadhali ndugu.
 
Una umri gani Mkuu...!!
Hutakiw.i kukata famaa....Mungu nae ana Makusudi yake....
Nimepambana kwenye nyanja nyingi za kimaisha ila bado, nimeitafuta furaha kwa muda mrefu ila siku zangu za kuishi hapa duniani zimekuwa za mateso na maumivu,

Matatizo yako ni yako binadamu hawajali na hata hawatawaza hicho ndio kitu kikubwa nimekutana nacho, nimehangaika kwa kila namna kufanikiwa kimaisha, ila ukweli destiny yangu nimeishaijua niliandikiwa kufeli toka nazaliwa, hilo nimejua,

Sioni haja ya kuendelea kuhangaika kwenye dunia hii ambayo imeshanihukumu kwamba mimi nitakuwa mtu wa kufeli maisha yangu yote, siku za kukosa furaha na maumivu zinatosha sasa, mimi moja kati ya wanadamu ambao furaha tumegombana nayo,

Naishia hapa na hii ndio point ambayo sina budi kurudi kwa yule aliyeniumba
 
Usijiue wewe..

Watu wote usione wanacheka ukadhani wana furaha, msala ule ule tena si ajabu ukisimuliwa yako ukaona madogo...

Kitu kikubwa humu duniani tafuta furaha yako wewe mwenyewe usisubiri kupewa, haipo hiyo

Jipende, jifurahie

NB:

Ila ishu ya kukosa pesa hasa mwanaume ni kipengele yaan ni special task mweeh
Tena special task kweli kweli.

Hebu vuta picha pale unaowatumainia pengine wakufariji ndio wanakua wa kwanza kukusimanga, heshima yako inaposhuka kwenye familia na kuonekana kama mtoto mdogo pengine wa nursery....

Mambo yote ya msingi hushirikishwi na wala hakuna yeyote anayejali tena hisia zako, si wazazi wako, si wadogo zako, si kaka wala dada zako na badala yake wote wakuone wewe kama mtu usiye na dira na ni mzigo tu kwao.

Mbaya zaidi ukute una elimu yako nzuri tu na ulikua na matarajio makubwa zaidi maishani mwako.

Mwanaume bila pesa katika uhuru huu huu tulionao ni bora tu kurudi enzi za utumwa kwa kweli. Kama kuna adhabu binadamu mwanamume asiye na pesa anaweza ona Mungu amempa (akamkufuru) basi ni yeye kuumbwa mwanamume katika ulimwengu huu.

Njia pekee ya kupambana na hali kama hii ni kuchukulia changamoto zote hizi kama njia ya mafanikio hivyo kupambana kwa jitihada zote na kumshirikisha muumba katika kila jambo kwa maana baada ya dhiki huja faraja
 
Nimepambana kwenye nyanja nyingi za kimaisha ila bado, nimeitafuta furaha kwa muda mrefu ila siku zangu za kuishi hapa duniani zimekuwa za mateso na maumivu,

Matatizo yako ni yako binadamu hawajali na hata hawatawaza hicho ndio kitu kikubwa nimekutana nacho, nimehangaika kwa kila namna kufanikiwa kimaisha, ila ukweli destiny yangu nimeishaijua niliandikiwa kufeli toka nazaliwa, hilo nimejua,

Sioni haja ya kuendelea kuhangaika kwenye dunia hii ambayo imeshanihukumu kwamba mimi nitakuwa mtu wa kufeli maisha yangu yote, siku za kukosa furaha na maumivu zinatosha sasa, mimi moja kati ya wanadamu ambao furaha tumegombana nayo,

Naishia hapa na hii ndio point ambayo sina budi kurudi kwa yule aliyeniumba
Pole sana mkuu kaza moyo kaka
 
Kuna watu wanalala barabarani, wanakula kwa kutafuta kwenye majalala wewe na bando na simu ya smart unayo unataka kujifanyeje??

Nenda soko lolote karibu nawe kila jionj hukosi masalo ya matunda na mboga mboga kila siku yanayobakia na kumwagwa.

Usitake life la MO usikope kama hujui biashara. Jipende wewe kwanza na Mungu wako, unataka ndugu wakupende WHY??

Everyday is Saturday............................... :cool:
 
Wanasaikolojia njooni muokoe jahazi huku kuna mtu anataka kujinyonga.

Ila we bwana mdogo unachekesha sana hapa bongo kulivyo na mazuzu wengi maisha yanakushinda vipi?

Au una too much expectations ambazo pia ni unrealistic

Hivi huwaoni hao vijana wenzako wanaouza utumbo na miguu ya kuku na maisha yanaenda vizuri tu huku wakiamini ipo siku watatoboa

Huwaoni wale kina mama wanauza karanga na mihogo kwenye beseni na maisha yanaenda tena wana familia zinawategemea

We mtoto mayai mayai sana ungekuwa karibu ningekuwasha makofi mawili matatu kwanza akili ikukae sawa.
Hufai kushauri mtu wa aina hii mkuu.. Unazidi kumtwika mitusi ya moyo wakat maelezo yake Tu hapo moyo wake umefadhaik na matusi kutoka kichwani mwake
 
Back
Top Bottom