Infantry Soldier
JF-Expert Member
- Feb 18, 2012
- 15,893
- 16,317
Maisha yamekuwa magumu sana huku uswahilini kwetu. Ninatamani hata kuuza hii Taxi bubu yangu (Chaser Avante GX-100) nifungue walau pub ndogo.
Sasa ni karibia mwezi wa saba huu tangia nianze biashara hii ya kuendesha Taxi bubu. Nilianza mwezi wa tano (May) mwaka huu wa 2020. Biashara imekuwa ngumu sana kwa maana siku hizi kuna Bajaj.
Mtu anaona bora akodishe Bajaj kwa bei nafuu ndio ampeleke mgonjwa hospital au kwenda mjini. Sisi Taxi Drivers tupo hoi biashara imeshuka. Kabla ya Bajaj kuja huko mambo yalikuwa shwari sana mwaka jana 2019, ila sasa hivi ni balaa tupu.
CHASER AVANTE NUMBER "A"
Kabla ya kuja Bajaj kulikuwa na hawa bodaboda ambao wao hawakuwa kikwazo kwetu kwa maana mtu hawezi kukodi bodaboda akabeba maharusi au akampeleka mama mjamzito kujifungua hospitali ya mbali.
Niliwahi kuwaza niendeshe gari hii kama Uber ila kutokana na ukubwa wake wa engine nisingeweza kupata faida yoyote. Ninaombeni msaada wenu wa mawazo.
Sasa ni karibia mwezi wa saba huu tangia nianze biashara hii ya kuendesha Taxi bubu. Nilianza mwezi wa tano (May) mwaka huu wa 2020. Biashara imekuwa ngumu sana kwa maana siku hizi kuna Bajaj.
Mtu anaona bora akodishe Bajaj kwa bei nafuu ndio ampeleke mgonjwa hospital au kwenda mjini. Sisi Taxi Drivers tupo hoi biashara imeshuka. Kabla ya Bajaj kuja huko mambo yalikuwa shwari sana mwaka jana 2019, ila sasa hivi ni balaa tupu.
CHASER AVANTE NUMBER "A"
Kabla ya kuja Bajaj kulikuwa na hawa bodaboda ambao wao hawakuwa kikwazo kwetu kwa maana mtu hawezi kukodi bodaboda akabeba maharusi au akampeleka mama mjamzito kujifungua hospitali ya mbali.
Niliwahi kuwaza niendeshe gari hii kama Uber ila kutokana na ukubwa wake wa engine nisingeweza kupata faida yoyote. Ninaombeni msaada wenu wa mawazo.