sayoo
JF-Expert Member
- Nov 19, 2014
- 5,272
- 7,870
*Fahamu maisha ya ubachela*
Maisha ya ubachelor unaweza kujishaua kufululiza kupika msosi hata mwezi mzima ila vyombo visafi vikiisha ndani unarudi kwenye utaratibu ule ule wa kula chipsi na paja la bukujero.Maisha ya ubachela kila siku tunapoteza vijiko kidogo kidogo kwa kumwaga maji ya ukoko wa ugali.
Maisha ya ubachela unaweza kuloweka sufuria ulopikia ugali likakaa na maji wiki nzima yakianza kunuka unamwaga halafu unaweka tena maji mengine.
Maisha ya ubachela mara nyingine neti hugeuka kuwa hema.Ikichomekwa haichomolewi mpaka siku utakapopata mgeni.
Maisha ya ubachela hufika kipindi mtu unageuka mbwa, unanusa kwanza nguo ili ujue kama unaweza kuipa round ya pili au hapana.
Maisha ya ubachelor unaweza kujishaua kufululiza kupika msosi hata mwezi mzima ila vyombo visafi vikiisha ndani unarudi kwenye utaratibu ule ule wa kula chipsi na paja la bukujero.Maisha ya ubachela kila siku tunapoteza vijiko kidogo kidogo kwa kumwaga maji ya ukoko wa ugali.
Maisha ya ubachela unaweza kuloweka sufuria ulopikia ugali likakaa na maji wiki nzima yakianza kunuka unamwaga halafu unaweka tena maji mengine.
Maisha ya ubachela mara nyingine neti hugeuka kuwa hema.Ikichomekwa haichomolewi mpaka siku utakapopata mgeni.
Maisha ya ubachela hufika kipindi mtu unageuka mbwa, unanusa kwanza nguo ili ujue kama unaweza kuipa round ya pili au hapana.