Maisha ya sinema yanatesa tuishi maisha yetu halisi

Siku zote matumizi ya kila siku usipoyadhibiti huwezi kuona pesa hata kama unatumia elfu 5 kwa siku..

Naomba nipe ufafanuzi wa bajeti yako kwa siku halafu na mie nikushushie yangu ya mwezi mzima uone utofauti.
 
Unasema matajiri hawaSpend pesa nyingi kwenye kula na kuvaa umefanya reserch au unaongea maneno ya vijiweni hemu mfuatilie Dadayake MO kwanza FatmaDewji then uje tena hapa na MO mkanda wa LV tu anaovaa unajua shingapi.

Musilete utopolo wa vijiweni mbaya hakuna mtu anaweka ptofile ya msosi ila wakikuwekea hao hutoandika maneno ya vijiweni.
Kakariri huyo
 
Utanashati unaficha shida nyingi sana.

1.unakula vibaya.
2.Huna pesa/pesa ya mawazo.
3.Huna kazi ya maana.
Hata kuvaa uvae chini ya kawaida..Utaonekana chizi.

Pendeza na Funika shida|sio kila mtu anajue unashida shida.
 
Utanashati unaficha shida nyingi sana.

1.unakula vibaya.
2.Huna pesa/pesa ya mawazo.
3.Huna kazi ya maana.
Hata kuvaa uvae chini ya kawaida..Utaonekana chizi.

Pendeza na Funika shida|sio kila mtu anajue unashida shida.
Huo ndio utumwa wenyewe mkuu
 
mkuu wewe ulisikia waapi.

pesa bila matumizi ni upuuzi,ukikutana na mwenye pesa halafu hatumii kuna 1,za kiganga 2,haoni cha akununua eneo hilo vyote anavyo au viko chini ya kiwango.

binafsi mimi simlaumu masikini anayenunua iphone ya milioni ili asumbue watu(lengo afarijike)kama anafarijika poaaa.

masikini anayenunua gari ya gharama( sawa tu maana maisha mafupi huwezi subiri mpaka uzipate hujui kesho utaamkia wapi)

masikini anayekula kuku na nyama kila siku jioni(ukweli anajipenda sana)

mwisho wa siku maisha ni mafupi mnoo,usipoonja raha hapa duniani ukaishi unasononeka tu,utakuwa umeidhurumu nafsi yako,fanya chochote ilimradi kinakupa furaha na hakiumizi mtu.
yupo mtu wangu alikopa 28mln akanunua silubaru forester new model,wife wake akalichomeka nyuma ya gari la uchafu yeye akiwa hayupo,aliporudi akaambiwa gari iko garage inasubiri uende ukasema unataka upewe shingapi ichinjwe,hakuwa mjinga ila bahati haikuwa upande wake.
 
Sasa kila siku kula nyama ndo utajiri au kuishi maisha ya juu?
Eti matajiri hawali vizuri au hawavai vizuri. Unaweza ukamuona mtu mwenye pesa kavaa tshirt ukasema kaiokota Karume lakini ukibahatika kuishika unajua kabisa hii ni expensive.
Kwenye chakula ndo usiseme sasa nyama nayo ndo yakuja kututolea povu hapa? Kwa taarifa yako watu wenye hela hasa wanakula vizuri mno ndo maana hawanenepeani hovyo kama wengine wenye hela za kubahatisha.
 
Sasa kila siku kula nyama ndo utajiri au kuishi maisha ya juu?
Eti matajiri hawali vizuri au hawavai vizuri. Unaweza ukamuona mtu mwenye pesa kavaa tshirt ukasema kaiokota Karume lakini ukibahatika kuishika unajua kabisa hii ni expensive.
Kwenye chakula ndo usiseme sasa nyama nayo ndo yakuja kututolea povu hapa? Kwa taarifa yako watu wenye hela hasa wanakula vizuri mno ndo maana hawanenepeani hovyo kama wengine wenye hela za kubahatisha.
Hapo umeongea ukweli watu wanajua kula ugali au ubwabwa na nyama ndo good life Ila matajiri huwa wanafuata ratiba ya mlo kamili
 
Members nije kwenye maada husika. Hii mada inalenga hasa wale watabaka la chini tunajiita wa uswazi, kwanza kabisa ifahamike kua familia nyingi za kishua wamekua hawatumii fedha nyingi kwenye mahitaji ya msingi ya kila siku kwa mwanadamu kama mavazi na chakula wengi hua na ratiba ya kula ugali mboga za majani wiki nzima na jpl ndio siku ya kula nyama.

Kwetu uswahilini tunaongoza kwa kununua nguo za gharama na kukaangiza vitoweo mbali mbali kama kuku nyama na samaki kila siku huku tukiunga na nazi tatu nyanya kisado. Tunasahau kua tupo kwenye utumwa wa kifikra uswazi ukila dona mchicha au tembele unaonekana ni umechoka kiuchumi hiyo dhana ndio inawatesa watu na kuwamalizia akiba zao.

Jambo lingine ni ununuaji mavazi ya gharama kuliko uhalisia wa maisha yako afu umepanga nyumba ya gharama kubwa wakati kuna nyumba za bei nafuu lengo lako uonekane upo vizuri lakini kiukweli unajitesa fedha yote unayopata inaishia kujaza kabati na kukaangiza.

Umepanga apartment vyumba vitatu huna familia ili uonekane nawe upo vizuri, umekopa umenunua gari used unashindwa kukatia hata bima kubwa ukipigwa pasi unatelekeza gari gereji huo ni utumwa tutafute pesa na tuitumie kwa nidhamu itusaidie zaidi. Tuishi kulingana na hali zetu sinema hazina faida....ni hayo tu
Chakula kizuri ni kipi? Hivi Masai kula mbuzi kwake ni anasa? Zizi limejaa mbuzi tele.Mkulima wa mchele kula pilau kila siku i anasa? Mtu mwenye kuku wa mayai 10 akila mayai kila Siku ni anasa? Chakula unachokiona kizuri wewe mwingine kwake sio cha gharana.Nahisi upo Dar huko vyakula ni vitu adimu.Mbeya kilo ya ng'ombe sh.5000
 
Unasema matajiri hawaSpend pesa nyingi kwenye kula na kuvaa umefanya reserch au unaongea maneno ya vijiweni hemu mfuatilie Dadayake MO kwanza FatmaDewji then uje tena hapa na MO mkanda wa LV tu anaovaa unajua shingapi.

Musilete utopolo wa vijiweni mbaya hakuna mtu anaweka ptofile ya msosi ila wakikuwekea hao hutoandika maneno ya vijiweni.
Kwanza kabisa ujembe hujaelewaa

jamaa kamaanishaa save, invest and develop!

mfano hyo dewij net worth yake ni bei gan !??

na yakwako ni ngap!!??

sio judge vitu pasi na facts!!
 
Unasema matajiri hawaSpend pesa nyingi kwenye kula na kuvaa umefanya reserch au unaongea maneno ya vijiweni hemu mfuatilie Dadayake MO kwanza FatmaDewji then uje tena hapa na MO mkanda wa LV tu anaovaa unajua shingapi.

Musilete utopolo wa vijiweni mbaya hakuna mtu anaweka ptofile ya msosi ila wakikuwekea hao hutoandika maneno ya vijiweni.


JESUS IS LORD
 
Mtoa mada unataka kutuaminisha kuwa masikini ndo hunywa Jack Daniels au Hennessey...wakati matajiri wao hupiga tu Double kick na Kitoko au siyo..

Fanya research yako vizuri bhana...huyo mwenye uwezo na anakula Nyama Jumapili tu ni either sababu za kiafya au kaagizwa na mganga au haipendi tu maana bucha zipo kote uswahilini mpaka ushuani na zote zinauza tu tena sana...mwenye uwezo Mara nyingi hula balanced diet na si michicha tupu acha uongo bhana.
 
Back
Top Bottom