Maisha ya Raia wako Yana thamani Kubwa Sana: Tujifunze kutoka Thai

BabaTina

JF-Expert Member
Aug 29, 2008
429
573
Huko nchini Thailand, timu ya watoto wachezaji mpira waliamu kufanya matembezi ya utalii wa ndani baada ya mazoezi yao ya mpira wa miguu katika moja ya mapango maarufu huko kwao. Wakiwa na baiskeli zao walipofika eneo la kuingilia ndani walipaki nje na wao kuanza safari ya matembezi kujionea uumbaji wa Mungu kwenye eneo hilo.

Kwa bahati Mbaya sana, Mvua kubwa ikanya na kujaza maji ndani ya pango hilo na vijana kulazimika kutafuta upenyo katika moja ya miinuko ya pango na kujibanza eneo hilo.
upload_2018-7-11_9-23-37.png


Mmoja kati ya vijana waliokuwa kwenye msafara huko alipaswa kusherehekea siku yake ya kuzaliwa siku inayofuata. Kutoonekana kwake kukazua hofu ambayo iliwafanya wazazi wake watoe taarifa katika vyombo husika. Nayo mamlaka ikachukulia taarifa hizo kwa umakini mkubwa na kuanza kuwasaka vijana hao yapata 12 pamoja na mwalimu wako wa soka.

upload_2018-7-11_9-33-51.png


Jitihada zikafanyika na kugundulika kuwa vijana wamebandwa kati ya viunga vya pango hilo lenye urefu wa KM 10. Waokoaji toka nchini Thai wakajaribu na kukwama hivo kuitisha msaada wa kutoka jumuiya ya Kimataifa.

Hatimaye timu kutoka UK, china na sehemu nyingine zikafika na kufanikiwa kuwanasua vijana hawa ambao walikaa ndani ya pango hilo kwa siku 10.

Binafsi nimejifunza kuwa, Mamlaka za nchi zipo kwa ajili ya watu wake na sio watu wake kwa ajili ya wenye mamlaka. Ndio sababu wanapaswa kuthaminiwa na kulindwa kwa namna yoyote ile.

Ushauri wangu kwa vyombo husika hususani wanaosema wakati mwingine mtu akipotea ni masuala binafsi hawawezi kuingilia wakajifunza hapa. Tazama video ya historia nzima ya tukio husika kwenye link hii



 

Attachments

  • upload_2018-7-11_9-22-21.png
    upload_2018-7-11_9-22-21.png
    442.5 KB · Views: 31
Huko nchini Thailand, timu ya watoto wachezaji mpira waliamu kufanya matembezi ya utalii wa ndani baada ya mazoezi yao ya mpira wa miguu katika moja ya mapango maarufu huko kwao. Wakiwa na baiskeli zao walipofika eneo la kuingilia ndani walipaki nje na wao kuanza safari ya matembezi kujionea uumbaji wa Mungu kwenye eneo hilo.

Kwa bahati Mbaya sana, Mvua kubwa ikanya na kujaza maji ndani ya pango hilo na vijana kulazimika kutafuta upenyo katika moja ya miinuko ya pango na kujibanza eneo hilo.
View attachment 807034

Mmoja kati ya vijana waliokuwa kwenye msafara huko alipaswa kusherehekea siku yake ya kuzaliwa siku inayofuata. Kutoonekana kwake kukazua hofu ambayo iliwafanya wazazi wake watoe taarifa katika vyombo husika. Nayo mamlaka ikachukulia taarifa hizo kwa umakini mkubwa na kuanza kuwasaka vijana hao yapata 12 pamoja na mwalimu wako wa soka.

View attachment 807055

Jitihada zikafanyika na kugundulika kuwa vijana wamebandwa kati ya viunga vya pango hilo lenye urefu wa KM 10. Waokoaji toka nchini Thai wakajaribu na kukwama hivo kuitisha msaada wa kutoka jumuiya ya Kimataifa.

Hatimaye timu kutoka UK, china na sehemu nyingine zikafika na kufanikiwa kuwanasua vijana hawa ambao walikaa ndani ya pango hilo kwa siku 10.

Binafsi nimejifunza kuwa, Mamlaka za nchi zipo kwa ajili ya watu wake na sio watu wake kwa ajili ya wenye mamlaka. Ndio sababu wanapaswa kuthaminiwa na kulindwa kwa namna yoyote ile.

Ushauri wangu kwa vyombo husika hususani wanaosema wakati mwingine mtu akipotea ni masuala binafsi hawawezi kuingilia wakajifunza hapa. Tazama video ya historia nzima ya tukio husika kwenye link hii




Mimi sikuwatuma.
 
Yote hayo yanatokana na kitu upendo .. asiyekuwa na upendo hawezi kuona hilo.
 
Kwenye nchi masikini uhai wa wananchi siyo priority kabisa. Hivi wangapi wanakufa kwa uzembe kila siku hapa Tanzania? ajali, mahosipitalini, mikononi mwa polisi nk? sad reality is that, in poor countries kwa sababu ya ugumu wa maisha na uongozi mbovu tulishaona vifo ni vitu vya kawaida. Hopefully, taifa letu likiendelea tunaweza kuanza kuona mwamko wa kuthamini uhai.

Ndo maana viongozi wakuu wa nchi bado wanaamini kwamba "vyombo vya usalama' vipo kuwaadabisha wananchi na si kuwalinda na mali zao!
 
Kaka waafrika kwa waafrika hatupendan ,kizazi cha kupendana kilishapita.

Watu waige mifano, Nchi nying dunian hasa za watu weupe, Raia mmoja kupotea tu ghafla ghafla ni balaaa hapatulii.

Umesahau ,Marekan walitumia Dola milion 87 kumtafuta ruban wao wakike wakwanza aliyepotea nandege ??.

Bongo hapa,ungeambiwa Bwana alitoaaa ,na ametwaaa..kwisha
 
Dah! Nilipo waona hao watoto kama mzazi chozi limenitoka, tofauti na hapa kwetu, viongozi hawapendi watu wao. wakishakuwa viongozi hujifananisha na miungu watu. na wanafikiria kuwa kiongozi kila uliwazalo ndilo dira ya unao waongoza.
 
Kwakweli watu weupe wametuzidi mengi sana si utajiri tu hata utu wametuzidi
Ndio maana tuliweza kutawaliwa kwa sababu ya unafiki wetu watu weusi, Mzungu anataka kumdhuru jirani au ndugu yako wewe unasadia miundi mbinu ya kurahisisha kazi ya kumuangamiza ndugu yako ,.

Bila kujua kuwa ndugu yako akiangamia kesho itakuwa zamu yako kwa sababu nawe utakuwa dhaifu kwa kukosa mtu wa kukusaidia.

Africa hatuna upendo wa kibinadamu tunamapenzi ya ngono tu kulaleki ndio maana watu wanajitoa roho kwenye hiko kitu.
 
Mtu anayeweza kukwapua rambirambi za wahanga atafikiria kuwaokoa?? Sanasana atapenda yatokee ili akwapue tena
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom