Mkuu wa chuo
JF-Expert Member
- Feb 3, 2011
- 7,608
- 5,269
Okay ukiachana na hilo, Kwa hiyo Serikali inasubiri hiyo video ndio ichukue hatua!? Halafu wewe kama wewe unahitaji hiyo video ili iweje!? ni kweli tukio lilitokea...1. sijasema tukio ni uzushi nimeraise doubt juu ya uwapo wa video ambayo haitolewi mpaka kwa masharti maalum. Masharti ambayo ni sawa na kuiamrisha serikali nini cha kufanya bila kuwa na reasonable doubt ya kufanya hivyo. Hivi kweli hata serikali iwe ya haki kiasi gani, unategemea iunde "tume ya kimahakama" just because kiongozi wa upinzani kasema hivyo?
Hivi unataka kusema ya kwamba haukuona, ile mihamala iliyotolewa kipindi kile, yale mawasiliano ya e mail, na zile transfer za yule dada wa Ujerumani, mpaka Zitto akaanza kummind Yericko Nyerere...2. Uthibitisho uko wa aina nyingi: unapodai zitto kapokea bilioni 3 toka kwa dr kimei na usalama wa taifa tunahitaji kujua WEWE UMEJUAJE! Una mkanda wa video, una transcript za mazungumzo yao, unaweza kutuonyesha bank statement ya zitto inayoonyesha miamala hiyo to that effect au?
Naona unaamua kuongea, hao kina Zitto si ndio waliunda uasi kwenye chama, wakaja na lile kundi la kina Ben Saanane, Juliana Shonza, kwani ni wapi Mbowe amefanya hayo ndani ya chama, mpaka uzungumzie na Mbowe kuweza kulinganisha na huo mfano wako...3. Zitto kuwasiliana na jack zoka tatizo liko wapi? zitto ana uhuru wa kuzungumza na yoyote yule. kwani chadema wana uadui na vyombo vya serikali? jack zoka ni usalama wa taifa kwa raia wote including wanachama wa vyama vya upinzani, polisi, jeshi, wizara n.k vyote hivyo ni vya raia wote. Chadema inafanya kana kwamba ukiwa chadema then wewe automatically ni adui wa serikali! Je Chadema kwenye katiba yake inatii sheria za nchi gani? au kuna kipengele kinasema "chadema member shall not talk to usalama wa taifa" humo ndani ambacho ndio zitto kavunja?
vile vile, kama nakumbuka vizuri (nisahihishe kama nakosea), gazeti halikutoa mazungumzo (transcript), bali lilitoa namba za simu na call duration, je unaweza kutuambia walikuwa wanazungumzia nini? au kwa sababu zitto ni "adui wa mbowe" basi "lazima awe anapanga mipango dhidi ya chadema". Bila kujua kilizungumziwa nini the rest is mere speculation. Hivi gazeti likichapisha simply namba za simu na call duration kati ya Mbowe na Kikwete utaconclude hivyo hivyo kuwa Mbowe anauza chama kama ilivyo kwa zitto au?
Wewe unang'ang'ania kwamba Chadema watoe huo ushahidi wao kama wanao, lakini haung'ang'anii Mwigulu atoe ule ushahidi wake kwamba ana ushahidi mpaka mbinguni, ni jinsi gani Chadema wanavyohusika na ugaidi... Mbona Lwakatare ameachiliwa halafu Mwigulu amebaki na huo Ushahidi wake, au hiyo sio Conspiracy theory!?4. Ushahidi wa mwigulu ambao siuongelei ni upi huo? sijaona video ya mwigulu popote pale, naomba link tafadhali niione kisha ndio nijadili.
Unasema mahakama haijadili Video, lakini ni hiyo hiyo video ndio iliyptumika kumkamata Lwakatare...5. Mahakama haijadili video kama video inajadili mashataka ambayo video ni ushahidi. Nilichotaka mimi ni maelezo kwa mtu kama wewe kuwa pale lwakatare kwa nini alikuwa anaongea yale? hivi wewe hujiulizi hili swali? Mipango ile haikupi maswali? Mpaka sasa hakuna alternative story ya video ile, kinachoonekana ni lwakatare kupanga mipango miovu baas! Chadema walitakiwa kusema kuwa the real story ni hii: "lwakatare alikuwa anaanda mswada wa bongomuvi", kitu kama hicho! sio kushabikia ushindi wa technicalities za kisheria mahakamani. Mwisho wa siku video iko pale pale bila maelezo.
Na kwanini hujiulizi ni huyo huyo Ludovick aliyeonekana kwenye tukio tena la Absalomu Kibanda... kwanini usijiulize Ludovick alikuwa na mission fulani ovu...Pili, Ludovick pia ni mwanachama wa chadema, sababu za yeye kurekodi mimi nisiye chadema siwezi kujua. Lakini je, kama mwananchama wa chadema anapanga mipango ya kuvunja sheria kama ile, si wajibu wa mwanachama wa chadema kuifichua? au mwananchama wa chadema anatakiwa kulinda mipango miovu ya chadema wenzie? Kwangu mimi yoyote aliyefichua video ile ni mwananchi mwema anayetakia mema nchi yetu. Unless of course chadema/lwakatare waseme kuwa lwakatare alikuwa ana-act or something, then aliyefichua ndio tutamuita mchochezi. Lakini kama tunavyojua Chadema hawajawahi kutueleza lwakatare alikuwa anapanga mipango hiyo kwa sababu gani....perhaps ni mipango ya kichama?