Maisha ya Gerezani siku unapowasili na kuanza kutumikia kifungo

Ukiitwa jina hata askari mwenye umri wa kumzaa inabidi useme"BWANAMKUBWAAA" na usiposema mkong'oto hautajali umri wako nasikia.
 
Daah,we jamaaa umefanya nkumbuke visivyokumbukika daah . .MAISHA SAFAR NDEFU Aiseee..
Mkuu maisha ndivo yalivo.
Na unapokumbuka unapata nafasi ya kujilinganisha na mtu sahihi.
Ukumbuke ulinganifu wa mtu sahihi ni kati YAKE na YEYE.

Ajilinganishe alivo leo ndio yeye wa miaka ya nyuma??

Utakumbuka tuu mkuu haina namna
 
Umesaidia sana kuwafungua baadhi ya watu ambao wamekuwa na mtazamo hasi juu ya Magereza.Ni kweli si mahali pazuri pa kuishi kwasababu unaenda huko ukiwa ni amri ya Mahakama kwa makosa fulani na kwa muda specific au maisha kabisa au kifo kulingana na hukumu yenyewe.Lakini wapo wengi tu ambao kwa kuishi hayo maeneo wametoka na mengi mazuri na kusahau yale yasiyo mazuri hukohuko na hilo ndilo ambalo wengi limewasaidia kuishi tena uraiani.

Kikubwa ambacho wengi huwa kinawauma ni ule muda waliokuwa kule ndani kwasababu huku nje kuna mengi yamefanyika kwahiyo mara nyingi hilo ndilo ambalo huwa linaumiza sana kwasababu maisha na muda hausimami mtu akiwa gerezani.

Stori na kumbukumbu yako kuhusu hayo maisha ni funzo kubwa kila mmoja anayesoma habari yako na kuondoa dhana potofu juu ya maisha gerezani pamoja na changamoto zake.
Huu ni ukweli mtupu.

Kuna tulio wengi tumetoka huko na faida kubwa kuliko muda wenyewe wa kuwa huko,

Adhabu ya kutumikia jera ukijitambua ukaacha kujitetea baada ya hukumu ukaamua kupanga namna ya kuishi jera hakika huwezi umia kiasi ambacho mtu wa nje anawaza.

Tatizo

Adhabu unayokutana nayo nje magereza sasa hasa uliyopewa na jamiii inayokuzunguka aseee huwa kubwa. Unarudishwa nyuma mpaka umri, aseee

Hili tatizo la watu kufikiria jera ni jehanam ndilo linalosababisha mfungwa kuteseka nje ya jera amalizapo kifungo chake

Watu wakisikia umefungwa wanaanza kugawana mali zako mpaka mke wako kana kwamba umekufa hili jamii hailioni kama ni mateao zaidi kuliko jera lenyewe

Hawajui ya kuwa unakuwa jera huku ukiutuma moyo wako na kuukabidhi katika familia hasa pale ubapokuwa na watoto ambao walikuwa wamefikia pahala ambapo baba huwa anatengeneza historia katika vichwa wanae
Wao kirahisi tuu wanakuja wanawafanyia maajabu, mke anashindwa na changamoto mpaka anaamini katika kupotea kwako mwisho watoto waweza geuka kuwa wa mitaani huku taswira yako ikiwa haiwaishi machoni hasa pale unapofungwa mtoto anapewa taarifa lakini hajui maana yake.

Hakika ukiwa jera amini usiamini nafsi yako huwa haiko mle kwani kunawakati moyo unauma bila sababu hapo unajua tuu wanangu wako katika magumu, ukikumbuka uliwaacha kipindi ambacho bado wanaamini baba anaweza piga dunia nzima na suruhisho la kila tatizo ni baba yao sasa leo hawakuoni na jamii inayowazunguka inachukua nafasi ya kuwafinyia vile wapendavyo



Mimi huwa naamini mateso ya mfungwa hayapo jera huwa yapo nje kulingana na jamii inayomzunguka
 
Huku kwetu Kwamtogole Juma kijana aliua akapelekwa mahabusu. Ndugu walihonga sana kesi iishe lakini wa kuambiwa anashtakuwa na Jamhuri.

Amekaa ndani miaka 10 sasa, waliokwenda huko wanasema amenenepa shavu dodo. Familia ina contract na mkuu wa gerezani kumhudumia. Tunaambiwa chakula chake kinatoka kwa mkuu wa gereza, amepewa chumba, godoro, shuka, blanket hata mswala cha kuswalia.
 
AROON UKIONA MFUNGWA ANATATULIWA MARINDA BAS UJUE AMETAKA MWENYEWE MAANA SYO LAZIMA, NA UKIBAINIKA MIAKA 30 INAKUHUSU.... UKIWA MKOROFI UTAPEWA ADHABU MPAKA UPATE ADABU..
Kwa asilimia kubwa hili linaukweli
Na mambo haya hata yakifanyika hufanyika kwa siri kubwa na si harali kabisaaa


Tatizo linakuja kwa wale sijui ni matatizo utakuta mwenyewe anajisogeza kwa watu wa dizaini hiyo.


Nacho amini kuishi jera wewe ndio unarchagua aina ya maisha yakupendezayo kama hukuhuku uraini.



Tukatae tukubali jera ina umuhimu wake pia katika jamiii.

Kuna watu wako jera unajiuliza hivi huyu mtu akiwa huru ni viumbe wangapi watateseka??
 
Huu ni ukweli mtupu.

Kuna tulio wengi tumetoka huko na faida kubwa kuliko muda wenyewe wa kuwa huko,

Adhabu ya kutumikia jera ukijitambua ukaacha kujitetea baada ya hukumu ukaamua kupanga namna ya kuishi jera hakika huwezi umia kiasi ambacho mtu wa nje anawaza.

Tatizo

Adhabu unayokutana nayo nje magereza sasa hasa uliyopewa na jamiii inayokuzunguka aseee huwa kubwa. Unarudishwa nyuma mpaka umri, aseee

Hili tatizo la watu kufikiria jera ni jehanam ndilo linalosababisha mfungwa kuteseka nje ya jera amalizapo kifungo chake

Watu wakisikia umefungwa wanaanza kugawana mali zako mpaka mke wako kana kwamba umekufa hili jamii hailioni kama ni mateao zaidi kuliko jera lenyewe

Hawajui ya kuwa unakuwa jera huku ukiutuma moyo wako na kuukabidhi katika familia hasa pale ubapokuwa na watoto ambao walikuwa wamefikia pahala ambapo baba huwa anatengeneza historia katika vichwa wanae
Wao kirahisi tuu wanakuja wanawafanyia maajabu, mke anashindwa na changamoto mpaka anaamini katika kupotea kwako mwisho watoto waweza geuka kuwa wa mitaani huku taswira yako ikiwa haiwaishi machoni hasa pale unapofungwa mtoto anapewa taarifa lakini hajui maana yake.

Hakika ukiwa jera amini usiamini nafsi yako huwa haiko mle kwani kunawakati moyo unauma bila sababu hapo unajua tuu wanangu wako katika magumu, ukikumbuka uliwaacha kipindi ambacho bado wanaamini baba anaweza piga dunia nzima na suruhisho la kila tatizo ni baba yao sasa leo hawakuoni na jamii inayowazunguka inachukua nafasi ya kuwafinyia vile wapendavyo



Mimi huwa naamini mateso ya mfungwa hayapo jera huwa yapo nje kulingana na jamii inayomzunguka
Kabisa unachokisema na ndiyo maana hata Nelson Mandela alipofungwa mwaka 1962 huko South Africa katika Gereza la Robben Island alikuwa anaandika sana barua kwa mkewe Winnie Mandela za mapenzi na hasa kutaka kujua watoto wake wa kike aliowaacha wakiwa wadogo sana wanaendeleaje....na inasemekana aliandika barua mamia na kwa mara ya kwanza rundo la barua zilizochambuliwa kama 250 zitawekwa hadharani July 2018.

Hiyo ni moja ya barua za Mandela akiwa gerezani alizomuandikia Winnie mwaka 1969
27mandela-image-1-blog427.jpg

27mandela-image-2-blog427.jpg
 
Huku kwetu Kwamtogole Juma kijana aliua akapelekwa mahabusu. Ndugu walijenga sana kesi iishe lakini wa kuambiwa anashtakuwa na Jamhuri.

Amekaa ndani miaka 10 sasa, wanaolwenda huko wanasema amenenepa shavu dodo. Familia ina contract na mkuu wa gerezani kumhudumia. Tunaambiwa chakula chake kinatoka kwa mkuu wa gereza, amepewa chumba, godoro, shuka, blanket hata mswala cha kuswalia.
Huduma za malazi na chakula ni haki kila mfungwa wala hakuna mfungwa special.shavu dodo ni kuridhika tu na hali halisi ya maisha.
 
miaka ya 90 mvua zilikua za shida hadi ilipokuja el nino..labda kama kwake tu mvua zilikua nzuri..na akapata pembejeo za kilimo,ambazo zilikua juu na yeye akiwa tu katoka jela..



Si umeona kasema kilimo cha kisasa alifanya? Wengi wa wananchi wa vijijini ni watu wasiopenda kutanguliza maarifa ndio maana wako vile. Nenda leo hii ambapo technology inatawala ukaone watu ambavyo hawalimi kwa mistari na wanalima bila kuweka mbolea!

Na sio pesa nyingi, nakumbuka gharama za kilimo cha Mahindi kisasa kwa ekari inagharimu kama laki tatu tu kuanzia kupanda mpaka kuvuna hiyo nikijumlisha na gharama za wafanyakazi na mkuu hapa ametuambia alitumia nguvu zake mwenyewe.
 
Anafikiri nyumba ni zile za vyumba vinne
Ramani kwa archtecture
Tiles
Gypsum


Nyumba tofali linapigwa na wasela kijijini linachomwa nyumba inapandishwa na udongo siyo simenti na inakalika.


Kijijini watu hawacomplicate maisha, kule mtu anafyatua tofali mwenyewe ananunua tumifuko twa cement kwa ajili ya Msingi na kona pamoja na sakafu anamalizia na bati,mbao,frame za madirisha,milango maisha murua. Hapo Plasta anaweka kiporo kwa mbeleni huko!
 
Kijijini watu hawacomplicate maisha, kule mtu anafyatua tofali mwenyewe ananunua tumifuko twa cement kwa ajili ya Msingi na kona pamoja na sakafu anamalizia na bati,mbao,frame za madirisha,milango maisha murua. Hapo Plasta anaweka kiporo kwa mbeleni huko!
Hiyo ndiyo hali halisi ya ujenzi wa baadhi ya vijiji si vyote wengine wako makini na ujenzi kwa kufuata kanuni bora za ujenzi kama mjini.
 
Back
Top Bottom