Maisha ya Dar ni magumu sana kwa walio nje ya system: Jua kali, mmebanana, sijui mnatafuta nini huko

Joel Johansen

JF-Expert Member
May 12, 2016
242
319
Naombeni tu mrudi mikoani kwenu muwaachie waliozaliwa hapo maana hao ndio wenye Dar. Nyie ambao babu zenu walihamia Dar miaka ya 60 na mlioenda Dar kwa malori na treni, mna maisha magumu hakuna mfano. Tatizo ukizoea shida unakuwa 'Surviver' matokeo yake unaendelea na routine bila kuwaza.

Kuna raha gani kubanana kwenye basi la kutoka Mbagala hadi Kariakoo huku ukiamka saa 10 usiku eti uwahi siti na kuepuka jam kisa kuwahi kazini?

Kuna raha gani kupishana na magari ya kitajiri kila siku, kujambishwa na mitaa K.V. Masaki, Osterbay na Sinza huku wewe mvua ikinyesha tu amani inakosekana, mshahara wako unaishia kweny basic needs k.v. chakula na rent?

Sikatai kuwa mikoani hakuna matabaka, lakini kuna unafuu mkubwa kwa wazawa wa mji husika kuliko wahamiaji; yaani kama hawakuja na mtaji maisha yao ni changamoto.

Kuishi kwa kuona magorofa na kufatilia siasa au burudani ati kwasababu ndio mji wa biashara hivyo siku moja unaweza kubahatika ni ulimbukeni na ukosefu wa maono. Rudini mikoani kwenu mkaendeleze mashamba na kuwa karibu na wajomba zenu ili lolote likitokea ni rahisi kusaidika kuliko huko Dar ambapo mtu huwezi hata kuchat kwa amani kwa kuhofia simu yako kukwapuliwa dirishani.
 
Kuna watu wanaishi ktk mazingira magumu afadhali hata ya mifugo mikoni. Ebu nenda bonde la msimbazi na mkwajuni kinondoni kaone watu wanavyoishi. Mtoa mada hii ulisahau
 
Tunakomaa na jiji hatutoki, unajuwa kilicho tukimbizama mikoani?
 
Dar kuna uzuri wake aisee japo shida zipo lakin sio kama za kijijini kwetu,maana ni dry hakulimiki chochote maji ya shida,biashara hazitoki,umeme hamna,vocha tu inabidi uagize mjini,lakini dar angalau nauza matikiti maji alhamdulah nnaishi sasa kijijini utamuuzia nani matikiti?hapa nazichanga nikifikia lengo nahama mkoa.wewe vipi wewee.
 
Kama wana mashida yao wabaki hukohuko dar watuache wa mikoani tupumue.
Waendelee kuchakaa wapate akili
 
Niko morogoro,kwa miezi mitatu iliyopita kutokana na shughuli zangu nimeishi kibaha maili 35 ,kongowe ,kwa mathias,picha ya ndege,kisha nikaingia kufanya utalii dsm kwa mwezi mmoja.(sikuwahi kufika kwa miaka kama kumi).kuna watu wengi sijapata kuona,kuanzia mbezi mpaka katikati ya mji,nikajiuliza hawa watu wanafanya nini jiji hili?,nikakaa ubungo darajani kwa saa nzima,movement ya eneo hili ni zaidi ya mji wote wa morogoro,lakini ukichunguza wakazi wake wengi ni wababaishaji tu,lakini nimepapenda sana kwa kuzugia lakini si kuishi,morogoro ni mji mzuri na tulivu sana.foleni za dar zilifanya nilichukie hilo jiji,wenyeji mtujuze mnaishije?
 
Usisahau vumbi la morogoro ni zuri maana linanenepesha mkuu, ukweli Dar watu wanaishi kwa kuunga unga ila hata kama hauna kazi unawwza unga dili mbili tatu hela ya kula unapata lakini mikoani ni kulima tu au uwe na shughuli maalum...
 
Hivi mkoani kama hauna ajira unapataje pesa? kwanza mkoani una ajiriwa wapi? ukitaka biashara mzunguko wa pesa upo wapi! mkoani ukiuza soksi zitatoboka umening'iniza kwenye enka.
 
Naombeni tu mrudi mikoani kwenu muwaachie waliozaliwa hapo maana hao ndio wenye Dar. Nyie ambao babu zenu walihamia Dar miaka ya 60 na mlioenda Dar kwa malori na treni, mna maisha magumu hakuna mfano. Tatizo ukizoea shida unakuwa 'Surviver' matokeo yake unaendelea na routine bila kuwaza.

Kuna raha gani kubanana kwenye basi la kutoka Mbagala hadi Kariakoo huku ukiamka saa 10 usiku eti uwahi siti na kuepuka jam kisa kuwahi kazini?

Kuna raha gani kupishana na magari ya kitajiri kila siku, kujambishwa na mitaa K.V. Masaki, Osterbay na Sinza huku wewe mvua ikinyesha tu amani inakosekana, mshahara wako unaishia kweny basic needs k.v. chakula na rent?

Sikatai kuwa mikoani hakuna matabaka, lakini kuna unafuu mkubwa kwa wazawa wa mji husika kuliko wahamiaji; yaani kama hawakuja na mtaji maisha yao ni changamoto.

Kuishi kwa kuona magorofa na kufatilia siasa au burudani ati kwasababu ndio mji wa biashara hivyo siku moja unaweza kubahatika ni ulimbukeni na ukosefu wa maono. Rudini mikoani kwenu mkaendeleze mashamba na kuwa karibu na wajomba zenu ili lolote likitokea ni rahisi kusaidika kuliko huko Dar ambapo mtu huwezi hata kuchat kwa amani kwa kuhofia simu yako kukwapuliwa dirishani.
Mkuu ngoja waje wazee wa mahindi na pilipili na ndimu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom