Maisha wilayani Missenyi ni magumu

Mkuu hayo uliyoyasema nimeyasikia leo.
Naifahamu Missenyi sana nadhani kuna kitu ulilenga kukipata huko ulipokikosa ndo ukaja na haya, lakini nikukumbushe kuwa.
1) Missenyi ina sehemu nyingi na aridhi kubwa sana ya kilimo na yenye rutuba na mvua za kutosha. Wana misimu miwili ya kulima kwa mwaka. Tofauti na maeneo mengi hapa nchini.
2) Aridhi ya huko mbali ya kwamba kwa mwaka inalimwa mara 2/ lakini huwa hawatumii mbolea hata kidogo( aridhi ina rutuba ya kutosha)
3)Mashamba ya miwa ya Kampuni ya Kagera Sugar, yanaeleweka na yana ukomo wake, ukiingia kwenye vijiji ukakuta kuna mashamba ya miwa jua haya ni mashamba ya watu binafsi tu.
4) Wanachi wa eneo hilo kwa asilimia kubwa hawategemei Kiwanda cha Sukari hata kidogo, yaani namba kubwa ya wafanyakazi wa kile kiwanda si wenyeji wa Missenyi, wafanyakazi walio wengi hutoka Wilaya ya Ngara, mkoa wa Kigoma pamoja na Mkoa wa Morogoro pia na wilaya ya Ukerewe.
5) Furusa Missenyi ni nyingi sana mbali na hicho kiwanda cha Kagera sugar pia na kiwanda cha Kahawa cha OLAM(ambacho kilifanya kazi kwa mda mfupi na kikafungwa japo sijui kama kimeshafunguliwa). Maisha ya wakaazi wa eneo hili hutegemea sana kilimo, ufugaji, uvuvi ndani ya mto Kagera, hutegemea sana biashara zinazofanyika kwenye mipaka ya Mutukula pamoja na mipaka ya Minziro, Bubare na Bugango yote mipaka hii inapakana na Uganda,
7) Pia katika shughuli za kiuchumi bado biashara zinafanyika sana hasa za mazao ya chakula ambazo mazao mengi hupata soko kwa wafanyakazi wa kiwanda cha Kagera . Vilevile mazao mengi hupata soko Bukoba mjini, na Uganda.
6) Mashamba ya miwa ya Kagera yaliyo mengi sana yako upande wa Magharibi mwa Wilaya hii na asilimia kidogo sana ni mashariki mwa Wilaya haswa kilipokuwa kiwanda cha Sukari cha zamani kabla hakijalipuliwa kwenye Vita ya Idd Amini. Hivyo sehemu za watu kulima ni nyingi sana na sidhani kama kuna mwananchi alishaingiliwa na kiwanda kuhusu aridhi ya kulima.
7) Lakini karibia mazao yote ya chakula hupatikana kwenye wilaya hii isipokuwa Mchele tu ndiyo haulimwi katika Wilaya ya Missenyi.
8) Haipo siku utasikia Missenyi ina njaa labda yatokee majanga mengine ya asili kama ilivyo ada kwa mkoa wa Kagera.
# Ni wilaya ambayo maisha yake yako chini sana na siyo gharama labda kwa mtu anayetaka mterezo tu.
# Naomba nikosololewe pale nilipoweka jambo ambalo halipo#
Misenyi ni wilaya inayoongoza mkoani kagera kwa uhaba wa chakula,, kilimo chenye tija huko ni miti tu lakini miwa!!! Yaani unalima kwa machungu halafu bei anapanga mnunuzi ambae ni mmoja tu kagera sugar ukijitia mgumu unabaki na miwa yako kaikamue utie kwenye chai sasa hivyo wakulima wanalazimika kukipa kiwanda tu kishingo upande

Misenyi chakula inakitegemea kutoka karagwe hasa ndizi,

Hiyo wilaya ngumu mnapamba kwa kuangalia kyaka na bunazi tu na sehemu za mipakani tu nendeni buyango, luzinga bwanja na kwingineko huko muone hali ya kiuchumi ilivyo, tuna roho ya choyo sana siku tukiacha hii nayo itasaidia kupambana na changamoto hizi
 
Du pole sana kwa maisha magumu mnayopitia huko mkuu. Kama wewe sio mtumishi wa umma hama hapo utazeeka huna maendeleo yoyote mkuu.
Lengo si kudharua Bali ni uhalisia.

Kwa wasio ifahamu Missenyi ni moja kati ya wilaya zinazopatikana mkoani kagera imepakana na wilaya ya karagwe, Bukoba vijijini na nchi ya Uganda pia ni eneo ambalo linapatikana kiwanda kikubwa cha sukari KAGERA SUGAR.

1. Ni wilaya ambayo uchumi wake mkubwa unategemea mwekezaji(Kagera sugar) Trust me wewe kama sio mwajiriwa wa serikali au mwajiriwa wa kampuni ya sukari uwezi kutamani kuishi wilaya ya Missenyi

2. Ni wilaya ambayo haina mazingira rafiki kwa kilimo sababu asilimia kubwa ya eneo lake ni mashamba ya miwa ya mwekezaji(kagera sugar) maeneo yaliyobaki ni hifadhi za maliasili na tetesi zilizopo ni kuwa mwekezaji anakula njama na serikali ili wananchi wengi wasijiajili kwenye kilimo waende kufanya kazi kwenye mashamba ya miwa kama vibarua.

3. Biashara. Mzunguko wa pesa unachanganya mwisho wa mwezi na mwanzo wa mwezi tu kutokana na kuwa na wakazi wengi ambao ni waajiriwa kwenye kampuni. Kama wewe ni mfanyabiashara inabidi ujiandae kufanya biashara ndani ya vipindi hivyo tu au ukubali kufanya biashara ya kukopesha. Pia wakazi wengi bado wanakasumba ya kununua vitu gulioni ambalo ufanyika jumamosi ya kila wiki hapa mtu yupo tayari kutofanya manunuzi yoyote ndani ya wiki mpaka ifike siku ya gulio kitu ambacho ufanya maduka ya rejareja kuwa na hali mbaya.

4. Fursa za ajira ni chache kuna viwanda viwili tu vikubwa cha kahawa na sukari bahati mbaya kiwanda cha kahawa kimefugwa kutokana na masharti na sheria nyingi za serikali kitu kilichofanya kubakiwa na kiwanda kimoja tu cha sukari.

Kama wewe ni mtafutaji na unatamani kuja wilaya ya missenyi kutafuta pesa huu ni ushauri wangu kwako jiandae kisaikolojia.
 
Wewe unaambiwa eneo lote limechukuliwa na miwa na hifadhi huelewi mkuu?
Kuna fursa Fulani kubwa naijua iko misenyi hivi nikitaka eneo eka Moja naweza pata kwa shilingi ngapi kwa wenyeji?
 
Sasa mtu utaenda kulima kwenye mapori ya akiba ya serikali mkuu?
Huyo mwongo tu! Wilaya ina mapori mengi sana. Yeye kang'ang'ania kagera sugar ambapo wengi ni warundi wanaolima miwa
 
Achana nalo hilo TAGA mkuu litakusumbua bure. Mwenyeji unalieleza ukweli halisi linapinga. Halafu usalama wa raia huko Missenyi sio mzuri.
Usiniite mwongo tuheshimiane hunijui. Watu wanafukuzwa na viboko mazao yao yanafyekwa afu unajifanya unaijua missenyi sana wakati hujui kinachoendelea
 
Misenyi ni wilaya inayoongoza mkoani kagera kwa uhaba wa chakula,, kilimo chenye tija huko ni miti tu lakini miwa!!! Yaani unalima kwa machungu halafu bei anapanga mnunuzi ambae ni mmoja tu kagera sugar ukijitia mgumu unabaki na miwa yako kaikamue utie kwenye chai sasa hivyo wakulima wanalazimika kukipa kiwanda tu kishingo upande

Misenyi chakula inakitegemea kutoka karagwe hasa ndizi,

Hiyo wilaya ngumu mnapamba kwa kuangalia kyaka na bunazi tu na sehemu za mipakani tu nendeni buyango, luzinga bwanja na kwingineko huko muone hali ya kiuchumi ilivyo, tuna roho ya choyo sana siku tukiacha hii nayo itasaidia kupambana na changamoto hizi
Sijawahi kushuhudia uhaba wa chakula katika maeneo haya, siandiki haya kwa kupamba bali naongea kile ninacho kijua. Ni wananchi wachache sana wanao jihusisha na na kilimo binafsi cha miwa na watu kuingia katika kulima miwa ni suala ambalo limekuja miaka ya hivi ya karibuni. Ndizi kutoka karagwe ni sawa na Mahindi yanavyotoka Missenyi kwenda Karagwe.
 
Haya ndiyo madhara ya kuendesha nchi kama familia kwa kutumia sheria za kijijini.
Watu walitolewa kwenye mashamba wakidaiwa wamevamia misitu na kigezo kingine ni kuwa sio raia waTanzania kitu ambacho sio kweli afu kuhusu kahawa kwenda Uganda kimagendo ni kweli lakini kwa nini serikali ishindwe kuzuia usafirishaji wa magendo na kuja kudai kwamba kiwanda cha kahawa hakifuati utaratibu kitu kilichopelekea kiwanda hicho kufungwa mwaka wa pili mfululizo.
 
Mkuu mbona wewe unaambiwa ugumu wa maisha ya Missenyi unakuwa mkali? Una maslahi gani na ugumu wa maisha ambayo watu wanapitia huko Missenyi?
Kwa hiyo we unapajua kwa bibi yake January Makamba tu. Inahuzunisha sana mwenzako napajua Minziro, igayaza, kabwoba, missenyi center Bubale kilimilile, Nsunga, kasambya we baki kupajua kwa bibi yake January Makamba.
 
Amesema maisha ni magumu kulinganisha na fursa zilizopo kwenye wilaya nyingine. Suala la uvumilivu linakujajje mkuu?
Kama uliyoelezea ndiyo unadhani ni ugumu wa maisha basi huyajui maisha magumu, Kama watu wanapata Kazi kwenye makampuni ya miwa wewe unataka wapate Kazi zipi tofauti na hizo?

Popote maisha huwa magumu tu, kikubwa Kazi na uvumilivu tu!
 
Sijawahi kushuhudia uhaba wa chakula katika maeneo haya, siandiki haya kwa kupamba bali naongea kile ninacho kijua. Ni wananchi wachache sana wanao jihusisha na na kilimo binafsi cha miwa na watu kuingia katika kulima miwa ni suala ambalo limekuja miaka ya hivi ya karibuni. Ndizi kutoka karagwe ni sawa na Mahindi yanavyotoka Missenyi kwenda Karagwe.
Hiki ni kichekesho yaani wanyambo waagize mahindi kutokea misenyi,,, hahahahaha nimeuishi huo mkoa naujua vilivyo baki na mapambio yako
 
Yaani mtoa post ni mbabaishaji hatari, umefika hapo Bunazi hadi Kagera Sugar kiwandani unajifanya kuifahamu Misenyi, kila kitu unarejea kiwanda cha sukari na mazingira yanayokizunguka kwamba ndo Misenyi, hopeless kabisa! Unapafahamu Minziro, Kanyigo, Mugana, Kakunyu, Mutukula, Katoro, Nkenge, Mwemage, Ishozi nk yaani umetembelea kote huko ukakuta miwa? Kwamba maisha magumu!!

Unakumbuka Rais JPM aliwahi kuuliza randomly kwenye mkutano wa hadhara hapo Kyaka kama kuna mtu anaweza kuwa na milioni mia ili apewe tenda ya kuuzia wenyeji sukari toka kiwandani akapatikana palepale 'yanki' mwenye zaidi milioni 200 na anafanyia shughuli zake hapohapo Misenyi!! Unamfahamu Dr. Remmy, agent wa mafuta ya Mukwano toka Uganda, maisha yake ya utafutaji kaanzia hapo Misenyi na sasa ana mafanikio ya kufa mtu.

Nenda Kanyigo, Kashenye ununue dagaa watamu kutoka Z. Victoria uje kuuza jumla hapa Dar uone utavyopiga hela. Miti ya kupandwa imejaa kila kona, kama huwezi kupanda yako, nunua iliyokomaa uuze mbao hela utaikimbia mwenyewe...

Mwingiliano wa kibiashara kati ya Misenyi na Kampala, Mbarara Uganda ni mkubwa mno na watu wamenufaika na hali hiyo toka kitambo.

Hayo mapori yanayokuzunguka wajanja wanafuga nyuki na kuuza asali, ardhi ina rutuba ya kutosha lima vanilla kama wenyeji upige hela, kilo moja ya vanilla Tsh. Laki na zaidi, unalalama tu kwa ufinyu wa kufikiri. Na kama umegundua uhaba wa huduma fulani, hiyo ndo fursa ichangamkie.

Magulio yapo kila mahali hadi Dar, na utamaduni wa kununua mahitaji na kuhifadhi wakati ukilenga gulio lijalo mbona poa sana, mijini watu huifadhi kwenye ma-freezer na jokofu! Sio kila leo ununue nyanya, vitunguu, mchele... Kha! Kwani wewe umetokea jamii gani ambayo ina kila fursa!?

Ukisikia sehemu ina mzunguko wa pesa unadhani ni za kuokota, lazima ufanye kazi haswaa.

Wakiboine!! Chwekamu
 
Amesema maisha ni magumu kulinganisha na fursa zilizopo kwenye wilaya nyingine. Suala la uvumilivu linakujajje mkuu?
Wilaya zipi alizolinganisha? Mbona ulinganifu wake ni too general? Anazijua Hali za wilaya zingine?
 
Back
Top Bottom