Ben Zen Tarot
JF-Expert Member
- Dec 13, 2014
- 3,905
- 6,691
Kweli hakuna anayefurahia kuachwa. Mapenzi yanauma, wakati mwingine hasira zinaweza kutuongoza katika kufanya maamuzi lakini suala la msingi linalopaswa kuzingatia ni kujidhibiti. Lazima tujifunze kudhibiti hasira zetu.
Kuachwa au kuachana siyo mwisho wa maisha. Kweli mnaweza kuwa mmewekeza nguvu, ndugu na hata marafiki katika uhusiano wenu lakini endapo imetokea mmeshindwa kuendelea na safari kwa namna moja au nyingine basi hakuna budi kushukuru na kuliacha lipite.
Usimuone mwenzako kama adui bali chukulia kama changamoto katika maisha yako kwani hujui pengine ni nini kingetokea kama ungeendelea na safari hiyo. Yawezekana Mungu amekuepusha na jambo lingine zito huko mbeleni.
Mshukuru yeye, usiwachukie marafiki, usiwakasirikie ndugu zake wala yeye mwenyewe. Mchukulie kama tu alikuwa mpenzi wako. Mheshimu maana pia anazo siri zako nyingi. Anakujua vizuri hivyo kama itakupendeza pia muombee mafanikio.
Muombe naye akuombee pia wewe katika safari yako. Kama una shida ambayo unaona yeye anaweza kuwa msaada kwako, mueleze. Kama atakuwa ni muungwana anaweza kukusaidia. Zungumza na marafiki na ndugu zake kama vile hakuna kitu chochote kilichotokea.
Yawezekana hili likakushinda katika kipindi cha awali lakini jipe moyo. Baadaye utaweza. Msalimie ukimuona barabarani. Hii inakufanya uonekane mstaarabu hata kwa ndugu zake hivyo itakuwa jambo jema pia kwao hata kuweza pia kufufua upya penzi lenu.
Kuna fursa ambazo anaweza kukupa au wewe ukampa hata kama mmetengana. Weka uhusiano pembeni, ruhusu moyo wako uwe katika hali ya urafiki. Urafiki utakupa fursa nyingi na endapo yeye au wewe utampata mwenza basi mtaambizana.
Kila mmoja atakuwa huru na hapo kidogo mawasiliano yanaweza kupungua ili kuepuka migogoro na wenza wenu wapya lakini inapowezekana mnaweza kusalimiana. Hayo ndiyo maisha na hakuna sababu ya kuwekeana chuki katika dunia hii iliyojaa nafasi nyingi maishani.
Kuachwa au kuachana siyo mwisho wa maisha. Kweli mnaweza kuwa mmewekeza nguvu, ndugu na hata marafiki katika uhusiano wenu lakini endapo imetokea mmeshindwa kuendelea na safari kwa namna moja au nyingine basi hakuna budi kushukuru na kuliacha lipite.
Usimuone mwenzako kama adui bali chukulia kama changamoto katika maisha yako kwani hujui pengine ni nini kingetokea kama ungeendelea na safari hiyo. Yawezekana Mungu amekuepusha na jambo lingine zito huko mbeleni.
Mshukuru yeye, usiwachukie marafiki, usiwakasirikie ndugu zake wala yeye mwenyewe. Mchukulie kama tu alikuwa mpenzi wako. Mheshimu maana pia anazo siri zako nyingi. Anakujua vizuri hivyo kama itakupendeza pia muombee mafanikio.
Muombe naye akuombee pia wewe katika safari yako. Kama una shida ambayo unaona yeye anaweza kuwa msaada kwako, mueleze. Kama atakuwa ni muungwana anaweza kukusaidia. Zungumza na marafiki na ndugu zake kama vile hakuna kitu chochote kilichotokea.
Yawezekana hili likakushinda katika kipindi cha awali lakini jipe moyo. Baadaye utaweza. Msalimie ukimuona barabarani. Hii inakufanya uonekane mstaarabu hata kwa ndugu zake hivyo itakuwa jambo jema pia kwao hata kuweza pia kufufua upya penzi lenu.
Kuna fursa ambazo anaweza kukupa au wewe ukampa hata kama mmetengana. Weka uhusiano pembeni, ruhusu moyo wako uwe katika hali ya urafiki. Urafiki utakupa fursa nyingi na endapo yeye au wewe utampata mwenza basi mtaambizana.
Kila mmoja atakuwa huru na hapo kidogo mawasiliano yanaweza kupungua ili kuepuka migogoro na wenza wenu wapya lakini inapowezekana mnaweza kusalimiana. Hayo ndiyo maisha na hakuna sababu ya kuwekeana chuki katika dunia hii iliyojaa nafasi nyingi maishani.