Maisha Plus Tv Show ya Masoud Kipanya

TBC1 wamechemsha kwenda live hiki kipindi. Hehehehehehe ni matangazo kwa kwenda mbeleee
 
Pimbi,
Avatar yako ni kiboko....haha hahaha! Nahisi mafunzo yake yalikuwa ni balaa....
 
Sioni elimu yoyote katika maisha plus, isitoshe kunamapugufu mengi tu
 
Siku zote iwa nashindwa kuielewa Mitanzania mingi.
Jamaa amebuni kitu badala ya kumpa moyo na kumpa mawazo nini aboreshe nini kifanyike badala yake tunaanza kumponda ooh kapotea kwenye media ooh alifukuzwa kazi hii ya nini?Mitanzania bana ndo maana hatusongi mbele......watu wanaikosoa kwa kulinganisha na big brother wapi na wapi bana?Wale wana fweza au falanga mingi Kipanya ndo hivyo amejikusanya na makampuni watu mnaanza kumponda na kumkatisha tamaa.
Tabia hizi Mitanzania sijui itaacha lini?Wenzetu mtu akikosea anapewa moyo kwetu huku unachekwa.
 
Unajua watu wengi ni wepesi sana wa kukosoa,na siku zote huishia kuwa walalamishi tu huku wakiwa hawafanyi lolote.Wewe mpaka hivi sasa umeshabuni nini ili tuanze kukusifia.Na kama hauoni cha kujifunza na kipindi chenyewe kinakuboa wewe unaangalia cha nini.Au ndo akina ninyi ambao unakuta kipindi kizima unaangalia wapi kachemsha ili kesho ukalipoti JF.Sijui lini tutapenda vitu vyetu.Ebu tujifunze kutoka kwa wachina,pamoja na kelele zote za ubovu wa bidhaa za china,lakini wapi bwana karibia wafanya biashara wote wa china nje ya china wanauza bidhaa zao.Bado wangeweza kuuza bidhaa za nchi nyingine.
 
Naona Kijana Kipanya amejitahidi kufanya ubunifu. Kwa kweli kukusanya vijana wenye mfumo tofauti wa maisha (differing life styles) na kuwaweka pamoja katika maisha ya kijijini si jambo dogo. Naamini wale vijana watajifunza mengi kutokana na kuishi katika kijiji kile. Watakaporudi makwao watakuwa na jambo jipya katika kurekebisha mwelekeo wao wa maisha. Ni kweli kuna mapungufu mengi lakini sharti tufahamu kuwa mwanzo ni mgumu. Ni matumaini yangu atazidi kuboresha kadiri siku zinavyosonga mbele. Hata hivyo, ningemshauri aanze kufikiria kuboresha elimu yake. Tumpongeze, tusimkatishe tamaa
 
kipanya2bc.jpg

Masoud Kipanya, Mmoja wa waanzilishi wa Maisha Plus

Wakuu, lile shindano la Maisha Plus ndio linaelekea ukingoni.

Nani unabashiri ataibuka kidedea?

Washiriki hawa ambao wapo katika kijiji kilichotengenezwa na kina Masoud maeneo ya Geza Ulole, Kigamboni wanazidi kuonekana wakali zaidi huku Wengi wakielekea kuwakubali wakali watatu na wa nne akiwa anawanyemelea kwa karibu kabisa. Wakali wanaoangaliwa kwa karibu ni:

  1. Abdul (Kutoka Zanzibar)
  2. Charles (Kutoka Arusha)
  3. Upendo (Kutoka Mwanza)
  4. Teddy (Kutoka Dar)
Wengine kama Maulid na Steve si wa kubeza!
 
WanaJf,
Maisha Plus ni mbadala wa Big brothers kwetu wtz. Namshukuru Bw. Masood Kipanya kwa ubunifu wake wa kuleta show inayoonyesha maisha halisi ya mtz na kutuondolea aibu zilizokuwa zinafanywa ndani ya big brothers ambazo ni kinyume na maadili ya jamii ya ki-tz.

Mnasema hamjui madhumuni ya show ya Maisha Plus. Nilivyoona mimi ni kwamba, vijana wa ki-tz ambao wengi wao kwa sasa hawajui maisha halisi ya kijijini sasa wamewekwa kijijini ili kufahamu ni namna gani baba zao, mama zao na babu zao walivyoishi kijijini bila kuwa na simu, umeme, jiko la umeme/gas la kupikia, maji ya bomba na kulala kwenye nyumba duni ambazo nyoka na wadudu wengine kuingia ndani ya nyumba ni jambo la kawaida. Kumbukukeni, siku hizi vijana wanaoenda JKT ni wachache, kule ndiko vijana wangejifunza maisha ya kujitegemea lakini kwa sasa Jkt haipo, sasa Masood kabuni utaratibu huo ni mzuri na anastahili kupongezwa kwani haya ni matunda ya ubunifu wa mtz masood. Jambo lingine ambalo nimeliona ndani ya maisha plus, ni washiriki ku-demonstrate tabia zao halisi walizonazo. Mtu mpole utamuona pale, mmbea utamuona, mtukutu utamuona, mbunifu, mwenye busara, kiongozi anajionyesha wazi wazi kuliko ule uozo tunaoushabikia ndani ya big brothers. It is high time kupenda vitu vyetu wenyewe. I like that show.
 
kipanya2bc.jpg

Masoud Kipanya, Mmoja wa waanzilishi wa Maisha Plus

Wakuu, lile shindano la Maisha Plus ndio linaelekea ukingoni.

Nani unabashiri ataibuka kidedea?

Washiriki hawa ambao wapo katika kijiji kilichotengenezwa na kina Masoud maeneo ya Geza Ulole, Kigamboni wanazidi kuonekana wakali zaidi huku Wengi wakielekea kuwakubali wakali watatu na wa nne akiwa anawanyemelea kwa karibu kabisa. Wakali wanaoangaliwa kwa karibu ni:

  1. Abdul (Kutoka Zanzibar)
  2. Charles (Kutoka Arusha)
  3. Upendo (Kutoka Mwanza)
  4. Teddy (Kutoka Dar)
Wengine kama Maulid na Steve si wa kubeza!


Abdul kutoka zanzibar
 
Mie naona kile kinaweza kuwa kipindi kizuri tu kikiboreshwa,

Lakini Masudi ameonyesha upendeleo wa wazi kwa baadhi ya washiriki huku wengine akiwakandamiza LIVE! Nadhani TBC1 ikiwezekana watafute mwendeshaji mwingine ambae anaupeo kwani inaonekana Kipanya kunawashiriki wanamzidi upeo matokeo yake anawapiga vita. Angalia baadhi ya madudu aliyofanya:

1. Washiriki waliwapendekeza Charles na Stev watolewe na sms za watazamaji zikawaangukia kuwa watoke, badala ya kuwatoa kama ilivyofanya kwa wengine huko nyuma akawapeleka kula maisha hotel na kuwarudisha ili watazamaji wapige tena kura kuatoa watu wengine, kweli akafanikiwa kawabakisha watu waliokwisha kutolewa!

2. Abdul ametuhumiwa na washiriki wa kike kuwa ni mshirikina kwani baadhi yao walimuona akiwasha moto kimazingara.....Masoud amemyamazia wala hajamuuliza! kinyume chake anawauliza waomtuhumu!

3. Abdul alikutwa choo cha kike, then baadae ikakutwa hirizi, Masoud wala hajajisumbua kumuuliza abdul alikuwa anafanya nini choo cha kike alfajiri? alikuwa akioga!? angeulizwa.
Badala yake Masoud eti anawauliza watoto wa kike tu,... na baadae wanaume bila kumgusa Abdul.

4. Abdul alitaka kumpiga Upendo kwa kumtuhumu ushirikina, ilitakiwa atolewe kabisa kwenye kijiji kwani kudhuru mwili ni kosa la jinai, vipi ingetokea kweli akampiga na kumletea madhara? Abdul alionyesha kukosa uvumilivu hapa kabisa, basi angeonywa ili washiriki wajue kupiga mtu ni kosa, wala hakuna mtu mwenye haki ya kumpiga mwenzie.

Mwisho kabisa, wale vijana ni wadogo zetu, watoto wetu, wenzetu, n.k. Tuwe wazi tu kuchagua kijana aneonekana kweli anafaa kuwa mshindi, sio kuchagua mchekeshaji, mrembo n.k. Wale woote ni watanzania, tusiwabague kwa lolote lile.
 
Mie wakati wa usahili kuna wakati sikufurahia namna bwana masoud,Bonda na yule dada..walivyo kuwa wanauliza maswali...mengine yalikuwa si ya kujenga,mengine ni ya kiudalilishaji..na wakati kwa kuwa wao walikuwa wamechoka walikuwa wanafanya kama hawataki.Hii ni ubunifu wa masoud lakini haikuwa fair kuwafanyi vijana wale ambao walionekana wengine hawana kazi wanategemea bahati nasibu ya pale.Na kupata audiance.

Ubunifu pekee niliouona katika zile auditions ni kuonyesha ujinga wa Watanzania hasa kizazi kipya.Ilikuwa inatia aibu.I hope hii siyo reflection ya mwelekeo wa watanzania.Maswali yalikuwa ya kipuuzi lakini yalidhihirisha umbumbumbu wa Taifa ( vijana taifa la leo na kesho) .Tutafika?
 
WanaJf,
Maisha Plus ni mbadala wa Big brothers kwetu wtz. Namshukuru Bw. Masood Kipanya kwa ubunifu wake wa kuleta show inayoonyesha maisha halisi ya mtz na kutuondolea aibu zilizokuwa zinafanywa ndani ya big brothers ambazo ni kinyume na maadili ya jamii ya ki-tz.

Napata tabu sana mtu anapozungumzia maadili ya ki-tz. Unamaanisha nini hasa? Maaadili yetu ni yapi? Kuvaa vibwaya na magome ya miti, kutembea uchi kama wabarbaigi? Please naomba ufafanuzi....
 
WanaJf,
Maisha Plus ni mbadala wa Big brothers kwetu wtz. Namshukuru Bw. Masood Kipanya kwa ubunifu wake wa kuleta show inayoonyesha maisha halisi ya mtz na kutuondolea aibu zilizokuwa zinafanywa ndani ya big brothers ambazo ni kinyume na maadili ya jamii ya ki-tz.

Mnasema hamjui madhumuni ya show ya Maisha Plus. Nilivyoona mimi ni kwamba, vijana wa ki-tz ambao wengi wao kwa sasa hawajui maisha halisi ya kijijini sasa wamewekwa kijijini ili kufahamu ni namna gani baba zao, mama zao na babu zao walivyoishi kijijini bila kuwa na simu, umeme, jiko la umeme/gas la kupikia, maji ya bomba na kulala kwenye nyumba duni ambazo nyoka na wadudu wengine kuingia ndani ya nyumba ni jambo la kawaida. Kumbukukeni, siku hizi vijana wanaoenda JKT ni wachache, kule ndiko vijana wangejifunza maisha ya kujitegemea lakini kwa sasa Jkt haipo, sasa Masood kabuni utaratibu huo ni mzuri na anastahili kupongezwa kwani haya ni matunda ya ubunifu wa mtz masood. Jambo lingine ambalo nimeliona ndani ya maisha plus, ni washiriki ku-demonstrate tabia zao halisi walizonazo. Mtu mpole utamuona pale, mmbea utamuona, mtukutu utamuona, mbunifu, mwenye busara, kiongozi anajionyesha wazi wazi kuliko ule uozo tunaoushabikia ndani ya big brothers. It is high time kupenda vitu vyetu wenyewe. I like that show.


We can see you also like Masoon..!! Just kiddin...thanks kwa kutupa mwanga.
 
Ubunifu pekee niliouona katika zile auditions ni kuonyesha ujinga wa Watanzania hasa kizazi kipya.Ilikuwa inatia aibu.I hope hii siyo reflection ya mwelekeo wa watanzania.Maswali yalikuwa ya kipuuzi lakini yalidhihirisha umbumbumbu wa Taifa ( vijana taifa la leo na kesho) .Tutafika?


WoS

Unakumbuka swali lolote waliloulizwa hao vijana, just curios..iwapo unakumbuka naomba tuwekee. Thanks
 
WoS

Unakumbuka swali lolote waliloulizwa hao vijana, just curios..iwapo unakumbuka naomba tuwekee. Thanks

nakumbuka machache sana maana most were kind of silly
kwamfano yule kijana kutoka Zanziba alivyokuwa anaulizwa kuhusu afya yake na kwamba voice box yake iko wapi - imekaa sijui kushoto au miguuni...akawa anasema tu DUUH!na kuamini kila alichokuwa anaambiwa na akina Masoud.
Mwingine ni msichana aliulizwa something to the effect kuwa sura yake imekaa kuoneysha ana hasira.....
Mengine yalikuwa on vipaji na wengi walikuwa wanasema wanaweza kuimba au kuigiza....
maswali mengi yalikuwa on IQ na other silly stuff which you dont expect me to memorise...nijaza memory yangu ilhali I have so many other important stuff to save!
UMERIDHIKA?( I DONT EVEN KNOW WHY U R ASKING AU WHY IM EVEN ANSWERING YOU!)
 
Mie naona kile kinaweza kuwa kipindi kizuri tu kikiboreshwa,

Lakini Masudi ameonyesha upendeleo wa wazi kwa baadhi ya washiriki huku wengine akiwakandamiza LIVE! Nadhani TBC1 ikiwezekana watafute mwendeshaji mwingine ambae anaupeo kwani inaonekana Kipanya kunawashiriki wanamzidi upeo matokeo yake anawapiga vita. Angalia baadhi ya madudu aliyofanya:

1. Washiriki waliwapendekeza Charles na Stev watolewe na sms za watazamaji zikawaangukia kuwa watoke, badala ya kuwatoa kama ilivyofanya kwa wengine huko nyuma akawapeleka kula maisha hotel na kuwarudisha ili watazamaji wapige tena kura kuatoa watu wengine, kweli akafanikiwa kawabakisha watu waliokwisha kutolewa!

2. Abdul ametuhumiwa na washiriki wa kike kuwa ni mshirikina kwani baadhi yao walimuona akiwasha moto kimazingara.....Masoud amemyamazia wala hajamuuliza! kinyume chake anawauliza waomtuhumu!

3. Abdul alikutwa choo cha kike, then baadae ikakutwa hirizi, Masoud wala hajajisumbua kumuuliza abdul alikuwa anafanya nini choo cha kike alfajiri? alikuwa akioga!? angeulizwa.
Badala yake Masoud eti anawauliza watoto wa kike tu,... na baadae wanaume bila kumgusa Abdul.

4. Abdul alitaka kumpiga Upendo kwa kumtuhumu ushirikina, ilitakiwa atolewe kabisa kwenye kijiji kwani kudhuru mwili ni kosa la jinai, vipi ingetokea kweli akampiga na kumletea madhara? Abdul alionyesha kukosa uvumilivu hapa kabisa, basi angeonywa ili washiriki wajue kupiga mtu ni kosa, wala hakuna mtu mwenye haki ya kumpiga mwenzie.

Mwisho kabisa, wale vijana ni wadogo zetu, watoto wetu, wenzetu, n.k. Tuwe wazi tu kuchagua kijana aneonekana kweli anafaa kuwa mshindi, sio kuchagua mchekeshaji, mrembo n.k. Wale woote ni watanzania, tusiwabague kwa lolote lile.

Mkuu kabla hauja sema kitu kwanza fanyia utafiti hayo unayotaka kuyasemea, nadhani ungejifunza ni kitu kinachofanyika kabla haujaanza kuonesha madudu yako juu ya hii. Akina Charles na Sreve hawkutolewa ki ukweli kama unavyodai ila ilikuwa na fake eviction kuwapa mchecheto washiriki. Halafu haya masuala ya kishirikina huwa hayapewi nafasi sana kama unavyotaka, unafikiri Abdul angetolewa kwa kuwa kuna madai kuwa anajihusisha na mambo ya kishirikina ingeifundisha nini jamii. Na hata wanao waua vikongwe na maalbino kwa imani hizo za kishirikina huwa na visingizio hivyo hivyo. Samahani kama una kitu binafsi na masoud nilichokuwa nakiweka sawa ni hicho tu ila vita yako na masudi hainihusu na nadhani hapa si mahala muafaka.
 
Napata tabu sana mtu anapozungumzia maadili ya ki-tz. Unamaanisha nini hasa? Maaadili yetu ni yapi? Kuvaa vibwaya na magome ya miti, kutembea uchi kama wabarbaigi? Please naomba ufafanuzi....

Magehema,

Sijui kama umenielewa, kama unaifuatilia Maisha Plus show inajaribu kuonyesha uhalisia wa maisha ya ki-tz. Katika show hii maadili ambayo nimezungumzia ni mwenendo mzima unaoonyeshwa na washiriki pale kijijini. Hakuna vitendo vya aibu kama kufanya mapenzi hadharani, kutembea nusu uchi, kutumia lugha zisizostahili dhidi ya mshiriki mwenzake, hakuna uvivu kila mshiriki anajumuika na wenzake katika kuendesha maisha ya pale kijijini. Tofauti na show ya big brother ambayo ishara za ngono za wazi au pengine kufanya ngono ni sehemu ya show, kutembea uchi ni jambo la kawaida, ugomvi na matusi kwao kawaida. Vitu kama hivyo hutavikuta katika show ya maisha plus. Kuthamini utamaduni wetu ni pamoja na kufahamu tulikotoka, wazee wetu walivaa mavazi ya magome ya miti hili likionyeshwa pale maisha plus linawafundisha vijana wetu tulikotoka. hakuna anayetembea uchi kama ulivyosema. Najua tuko pamoja Mkuu Magehema
 
Back
Top Bottom