Itovanilo
JF-Expert Member
- Jul 30, 2018
- 2,314
- 5,138
Mwenyezi MUNGU tunusuru waja wako,
Tunahitaji huruma yako na ututie nguvu ili tuwe na mwisho mwema. Iko hivii, Jana ilikuwa ni siku ya furaha kiasi, nimemaliza kazi zangu ndogo ndogo ofisini kwangu. Nikaona ni muda sahihi wa kuondoka zangu hasa ukizingatia ni weekend kwahiyo masaa manne kwa Jana yalitosha kabisa.
Basi, wakati najiandaa kutoka Kuna Mmama aliingia, ni mgeni machoni pangu,ni mrefu wastani anaonekana ni mtu anayeutunza mwili wake huku akivisaliti vipodozi vyote. Tukasalimiana,huku nikimkaribisha kiti akae,wakati nikimtazama kwa umakini mama wa makamo (wengine humu ni bibi yenu kabisa)
Akaniuliza habari fulani zinazohusiana na kampuni yetu, Huku akiwa hakwepeshi macho. Yanayonihusu nilimjibu,makubwa nikamuelekeza sehemu husika,kwamba Kama yupo serious basi aje jumatatu.akajibu sawa.
Cha ajabu, Akatoa, bahasha fulani kwenye mkoba wake ,na kunikabidhi. Niligwaya kidogo maana ni kitu ambacho sikukitarajia,akasisitiza nipokee huku akitabasamu. Safari hii nikagundua yule mama ni mzuri,Tena mzuri sana.sijui usichana wake alikuwaje ni mweusi, lakini weusi flani mtamu.
Wakati hayo yakiendelea,mlango uligongwa tena, Safari hii akaingia secretary wetu,lakini nilishangaa yule secretary alivyoangaliana na yule mama,wote walitabasamu mno,bila kuongea chochote, Nikavunja ukimya,baada ya kumkaribisha naye akae,lakini akanijibu nilikuja kukuaga tu
Mimi sinaga subira ,yule dada alivyoondoka nikatamani kuona Nini kipo kwenye bahasha nilopokea, Kuangalia nikakuta pesa taslimu TSH laki mbili yaani zile noti za elfu mbili mbili ,kale kamkanda hakajachanwa lakini pia karatasi yenye namba za simu pamoja na kadi ya mualiko,
Kabla sijamuuliza chochote yule mama,nilijiuliza haya,
Huyu mama ni nani?
Anataka nini?
Pesa za nini
Kadi ya mwaliko je,naalikwa wapi?
Tumezoea tukipewa kadi sisi ndiyo watoaji wa pesa,
Inaendeleaa.....
Tunahitaji huruma yako na ututie nguvu ili tuwe na mwisho mwema. Iko hivii, Jana ilikuwa ni siku ya furaha kiasi, nimemaliza kazi zangu ndogo ndogo ofisini kwangu. Nikaona ni muda sahihi wa kuondoka zangu hasa ukizingatia ni weekend kwahiyo masaa manne kwa Jana yalitosha kabisa.
Basi, wakati najiandaa kutoka Kuna Mmama aliingia, ni mgeni machoni pangu,ni mrefu wastani anaonekana ni mtu anayeutunza mwili wake huku akivisaliti vipodozi vyote. Tukasalimiana,huku nikimkaribisha kiti akae,wakati nikimtazama kwa umakini mama wa makamo (wengine humu ni bibi yenu kabisa)
Akaniuliza habari fulani zinazohusiana na kampuni yetu, Huku akiwa hakwepeshi macho. Yanayonihusu nilimjibu,makubwa nikamuelekeza sehemu husika,kwamba Kama yupo serious basi aje jumatatu.akajibu sawa.
Cha ajabu, Akatoa, bahasha fulani kwenye mkoba wake ,na kunikabidhi. Niligwaya kidogo maana ni kitu ambacho sikukitarajia,akasisitiza nipokee huku akitabasamu. Safari hii nikagundua yule mama ni mzuri,Tena mzuri sana.sijui usichana wake alikuwaje ni mweusi, lakini weusi flani mtamu.
Wakati hayo yakiendelea,mlango uligongwa tena, Safari hii akaingia secretary wetu,lakini nilishangaa yule secretary alivyoangaliana na yule mama,wote walitabasamu mno,bila kuongea chochote, Nikavunja ukimya,baada ya kumkaribisha naye akae,lakini akanijibu nilikuja kukuaga tu
Mimi sinaga subira ,yule dada alivyoondoka nikatamani kuona Nini kipo kwenye bahasha nilopokea, Kuangalia nikakuta pesa taslimu TSH laki mbili yaani zile noti za elfu mbili mbili ,kale kamkanda hakajachanwa lakini pia karatasi yenye namba za simu pamoja na kadi ya mualiko,
Kabla sijamuuliza chochote yule mama,nilijiuliza haya,
Huyu mama ni nani?
Anataka nini?
Pesa za nini
Kadi ya mwaliko je,naalikwa wapi?
Tumezoea tukipewa kadi sisi ndiyo watoaji wa pesa,
Inaendeleaa.....