Naja naja
JF-Expert Member
- Sep 13, 2016
- 747
- 1,452
Maisha yanazidi kunichachia kila kukicha, nimetafuta sana kazi bila mafanikio yoyote mpaka ninahisi nimerogwa.
Mtaani thamani yangu imeshuka mno maaana nilipiga hatua kidogo ya kielimu ila nikakosa mtu wa kuniendeleza baada ya kufiwa na mama (baba yupo ila ni baba jina) hivyo nikakata tamaa ya kuandika barua ya ku-postpone maana nilishawahi ku-postpone lakini mambo hayakwenda vizuri hivyo nikaamua kuacha chuo.
Kwa sasa nahitaji angalau kupata kazi niingize japo elfu 7 kwa siku.
Mawazo ya kujiua yananiandama mara kwa mara ila ninapingana nayo kiume. Nina imani ipo siku nitafanikiwa.
Mtaani thamani yangu imeshuka mno maaana nilipiga hatua kidogo ya kielimu ila nikakosa mtu wa kuniendeleza baada ya kufiwa na mama (baba yupo ila ni baba jina) hivyo nikakata tamaa ya kuandika barua ya ku-postpone maana nilishawahi ku-postpone lakini mambo hayakwenda vizuri hivyo nikaamua kuacha chuo.
Kwa sasa nahitaji angalau kupata kazi niingize japo elfu 7 kwa siku.
Mawazo ya kujiua yananiandama mara kwa mara ila ninapingana nayo kiume. Nina imani ipo siku nitafanikiwa.