Maisha magumu sana ila nina imani ipo siku nitafanikiwa

Naja naja

JF-Expert Member
Sep 13, 2016
747
1,452
Maisha yanazidi kunichachia kila kukicha, nimetafuta sana kazi bila mafanikio yoyote mpaka ninahisi nimerogwa.

Mtaani thamani yangu imeshuka mno maaana nilipiga hatua kidogo ya kielimu ila nikakosa mtu wa kuniendeleza baada ya kufiwa na mama (baba yupo ila ni baba jina) hivyo nikakata tamaa ya kuandika barua ya ku-postpone maana nilishawahi ku-postpone lakini mambo hayakwenda vizuri hivyo nikaamua kuacha chuo.

Kwa sasa nahitaji angalau kupata kazi niingize japo elfu 7 kwa siku.

Mawazo ya kujiua yananiandama mara kwa mara ila ninapingana nayo kiume. Nina imani ipo siku nitafanikiwa.
 
Nenda Kwa wasabato kajiunge na uinjilist wa vitabu upate mtaji ukomae mtaa , miez miwili ni mingi ukikomaa unakuwa na one mill up to 2millio.. ila uwe mcheshi, mchangamfu , mtu wa kuombea watu na biblia ujue kuifunua funua. Acha ujinga wa kutaka kujiua
 
Usichoke kupambana jaribu kila sehemu kuomba ujitolee hata kwa wauza chipsi, wajenzi wa nyumba, na fani zote za chini utapewa chakula cha siku ukizoeleka utaanza kulipwa kwa siku na hatimae utapata uzoefu na utasimama mwenyewe. Usikate tamaa maisha yana mapito mno
 
Toa kwanza hilo liavatar lako limekaa kishetanishetani that's why mishe zako zinagoma.

Usikate tamaa jishushe fanya kazi yoyote halali ndo shida vijana mlioingia darasani mnachagua sana kazi za kufanya.

Tafuta hta mishe za kusaidia mafundi kujenga naamini huwezi kukosa elfu 30 per week fanya hta kwa miezi 3 au 4.

Baada ya hapo utakuwa umepata mtaji uza mitumba, genge n.k

Never give up.
 
Ushauri wangu ni do not despair. Maisha ndio haya haya. Maisha yalivyo, Laiti Mungu angetuonesha matatizo ya wengine unaweza kusema Mungu amekupendelea sana kwa hayo ya kwako machache au nafuu.

Fanya moyo wako mgumu kaka. Omba Mungu na endelea kutafuta fursa na kupambana kwa kila namna itakayowezekana. Though the sorrow may last for the night, his joy comes in the morning.

I wish ningekua na namna ya kukusaidia yoyote ile. Ila chonde chonde, jitie nguvu. One day you'll look back and be amazed at how far God has gotten you from.

Hizi ndio ushuhuda. Unafikiri watu wasingekua wanapitia matatizo, wangekua wanapata wapi ya kusimulia ukuu wa Mungu maishani mwao?
 
Pole mkuu, ndio ukubwa huo.

Amka asubuhi kama unaenda kazi, tembea kwa miguu popote unapoenda.

Jaribu kujichangaya na watu na sikiliza stori zao za kimaisha hata muuza mihogo utapata uamko fulani.

Watu wanatoka vijijini wanakuja kujichanganya mjini, na wanajikimu.

Mimi nilikuwa miaka hiyo hata nina shilingi mia ya mihogo naweka kambi nasilikiliza stori za maisha.

Weka uso wa mbuzi, kama ikibidi mvagabae baba, mpe laivu kutoka kichwani kwako kama mtaelewana poa, lakini umejaribu
Usikate tamaa
 
Siku moja nilienda Temeke hospital nikiwa hoi nachechemea mguu. Baada ya kwenda kwenye sehemu ya foleni kumuona daktari niliacha mara moja kuchechemea. Maana nilikutana na watu wenye vyuma miguuni,Miguu imevimba,wamekatika miguu. Wengine bodaboda wanaletwa naona. Bila kwenda kumuona daktari nilijikuta natembea vizuri wala sisikii maumivu. Na nilirudi home kabisa maana niliona mimi siumwi natania/nadeka.

Huku kuna padri anapenda kusema ukiona umejisahau au umekata tamaa nenda Hospital ya Mount Meru Wodi namba sita. Utakachokiona utajifunza. Ni Wodi ya Wagonjwa wa TB na Kansa.

So my point is pinned to the fact that. No matter what you're going through Never loose focus and never give up. Jitahidi kufurahi na ulichonacho. Kidogo hicho kinachokuliza kuna mtu anakitamani hakipati. Kuna mtu anatamani hata angeweza kupost uzi kama ww ulivyoweza ila kashindwa. Afya yako uliyonayo hapo ni mafanikio makubwa sana kwako maana Maisha ni Afya na sio pesa.

Kila siku Ukiamka asubuhi ukavuta pumzi ikaingia na kutoka mpaka jioni bila msaada wala shida yoyote basi wewe ni moja ya matajiri wakubwa waliopo duniani. Najua hutanielewa na kuniona mbabaishaji/Machi noo ila ndio ukweli maana tumezoea kuyapima mafanikio kwa vile vitu vinavyoweza shikika (Material things).

Embrace what you have.. Happily
 
YouTube channel..
Website
Jiajiri kwenye technology
YouTube zinasajiliwa. Akianzisha channel bila hata hela ya kula atapata wapi content, na hao viewers idadi ya kuanza kulipwa atafikisha lini. Kwanza YouTube channel hailipi kibongobongo hapa labda uunganishe na kitu kingine kama Shilawadu na channel yao.

Hii ni long term solution ngumu sana. Wengi uishia kutangaza kwa wino mwekundu usisahau kusubscribe.
 
Maisha yanazidi kunichachia kila kukicha ,nimetafuta sana kazi bila mafanikio yoyote mpaka ninahisi nimerogwa .

Mtaani thamani yangu imeshuka mno maaana nilipiga hatua kidogo ya kielimu ila nikakosa mtu wa kuniendeleza baada ya kufiwa na mama ,(baba yupo ila ni baba jina) hivyo nikakata tamaa ya kuandika barua ya kupostpone maana nilishawahi ku postpone lakini mambo hayakwenda vizuri hivyo nikaamua kuacha chuo.
Kwa sasa nahitaji angalau kupata kazi niingize japo elfu 7 kwa siku .

Mawazo ya kujiua yananiandama mara kwa mara ila ninapingana nayo kiume nina imani IPO siku nitafanikiwa.
Acha kumuita baba ako baba jina akati we mwenyewe unapambana na huna direction.
 
Acha kudanganya wenzio, mtu hana hela ya kula atapata wapi hela bibble
Kule kila kitu unapewa bure ni wewe Tu na mguu na njia na utakula vinono vya watu mpak ukimbie, kwenye dini kuna hela kinyama
 
Back
Top Bottom