je parle
JF-Expert Member
- Nov 28, 2018
- 1,876
- 3,616
Watazania tuna roho za tamaa sana katika biashara zetu.kila mtu anataka utajiri kupitia hela ya mwenzake. wakulima wanapandisha bei za bidhaa hovyo hovyo pasipo sababu lengo tu wanajua hakuna mtu atakemea .ukija kwa madalali wa bidhaa na wao ni hivyo hivyo yaani kila mtu anajipangia chake matokeo yake anaeumia ni mtumiaji wa mwisho inauma sana.
Leo nimeenda gengeni kununua viazi vitamu nimeuziwa viwili 500 nimeshangaa sana kidogo nizimie.imefika wakati bora ule kwa mama ntilie tu. Hali ni mbaya mtaani kama unakula kwenu kuwa na heshima sana nchi ishaingia njaa hii, ila kama una hela nzuri huwezi kuona chochote zaidi ya kujionea sawa tu.
Kingine jana nimepanda gari Kariakoo za vikindu naambiwa kugeuka nayo 1300 nikabidi nimwambie konda nipe hela yangu nishuke siwezi kubali huu upuuzi mana mtafanya kama ndio desturi yenu na itazoeleka kila siku mtakuwa mnafanya haya mauza uza. Japo nilikuwa na kama laki 2 hivi mfukoni ila nilishuka kwa kuwa niliwa feel sana abiria ambao hawana hiyo hela. Hili pia serikali la kuliingilia kati abiria wanateseka sehemu ya mia tano unaenda kwa buku.
Mfano Mbagala gari hata kama ishafika kariakoo kugeuka nayo hadi mbagala ni 1000 wakati tunajua nauli halali ni 500. Hili tatizo linafanyika hapa mataa ya kamata hapa na gerezani. Huu ni uhuni wa makondakta na madereva wao kutaka utajiri kwa abiria ambao wanaunga unga maisha.
Naunganisha picha ya viazi vitamu vya jero nilivyouziwa sokon.inamaana ukitaka kula vizuri ununue vya buku 3. Wakati mwaka mmoja nyuma tulikuwa tunanunua mia tano .tatzo ni nini mazao yamekataa au tamaa za madalali?
Nimeumizwa sana na maisha kuwa magumu
Leo nimeenda gengeni kununua viazi vitamu nimeuziwa viwili 500 nimeshangaa sana kidogo nizimie.imefika wakati bora ule kwa mama ntilie tu. Hali ni mbaya mtaani kama unakula kwenu kuwa na heshima sana nchi ishaingia njaa hii, ila kama una hela nzuri huwezi kuona chochote zaidi ya kujionea sawa tu.
Kingine jana nimepanda gari Kariakoo za vikindu naambiwa kugeuka nayo 1300 nikabidi nimwambie konda nipe hela yangu nishuke siwezi kubali huu upuuzi mana mtafanya kama ndio desturi yenu na itazoeleka kila siku mtakuwa mnafanya haya mauza uza. Japo nilikuwa na kama laki 2 hivi mfukoni ila nilishuka kwa kuwa niliwa feel sana abiria ambao hawana hiyo hela. Hili pia serikali la kuliingilia kati abiria wanateseka sehemu ya mia tano unaenda kwa buku.
Mfano Mbagala gari hata kama ishafika kariakoo kugeuka nayo hadi mbagala ni 1000 wakati tunajua nauli halali ni 500. Hili tatizo linafanyika hapa mataa ya kamata hapa na gerezani. Huu ni uhuni wa makondakta na madereva wao kutaka utajiri kwa abiria ambao wanaunga unga maisha.
Naunganisha picha ya viazi vitamu vya jero nilivyouziwa sokon.inamaana ukitaka kula vizuri ununue vya buku 3. Wakati mwaka mmoja nyuma tulikuwa tunanunua mia tano .tatzo ni nini mazao yamekataa au tamaa za madalali?
Nimeumizwa sana na maisha kuwa magumu