Maisha hayako fair, kuna muda unakutana na mwanamke ana sifa zote unazotaka lakini Single Mother

Kuna mambo yanaumiza sana moyo, unakutana na mdada unajisemea huyu ndiye niliyekuwa namuota siku zote, sifa zote unazopenda anazo pengine unamueleza hisia zako naye anakuelewa. Lakini kinachotokea unakuta kashazalishwa na mbaya zaidi baba mtoto bado yupo hai😃😃

Kuna muda mpaka unatamani ubebe kimya kimya tu, ila ukitafakari zaidi unaona ni heri nusu shari kuliko shari kamili.
Amini kweli kabisa
 
Nina story yakufurahisha sana kuhusu mm, natumai itakusaidia kufanya maamuzi sahihi.
Kwa bahati mbaya sana mama yangu mzazi alifariki nkiwa mdogo sana, mzee akaoa mke mwingine alikua na watoto wa2 tayari, na mm wa3.
Miaka kama mi5 mbele mzee akavuta, maisha yakaendelea.
Kuna jamaa nlianza kumuona anakuja kumtembelea mama yangu wa kambo, nlipokujaga kuuliza kwa watoto wake wakasemaga ni mzee wao.
Sikuwah kumuona jamaa kipind chote mzee alipokuaga hai.
Hadi pale alipofariki.
Mama bado yupo, jamaa bado yupo.

Kila la kheri mkuu.
 
Ila kweli Mkuu umenena vizuri, ukijiuliza haya maswali unaweza kufanya vizuri
Hata ukipata majibu keep this in ur mind "Vikojoleo havinuniani hata kama wao waliachana kwa mtiti mzito" hata ipite miaka mingi kiasi gani midamu wote wako hai watakuja kukumbushia tu tena wanaweza fufua penzi upyaaaa, wewe labda ndio umeoa kumbe baba mtoto anakuja kua mchepuko wake wa nje ya ndoa..
 
Kubishana na mtu anayejiita kambi ya fisi ni kujidhalilisha! Wewe endelea kuwa mlezi mzuri wa watoto wa wenzio maana uwezo wa kupata wa kwako huna! Wanawake wanaojitunza na kujithamini wapo wengi
Naona umishiwa hoja bwashee hadi umehamia kwenye jina, hii ni kawaida kwa watu wengi wenye akili za kitoto, nakutakia ukuaji mwema sana.

Kuoa single mother anaye jitambua ni akili ya kiutu uzima, lishike hilo.
 
Kuna mambo yanaumiza sana moyo, unakutana na mdada unajisemea huyu ndiye niliyekuwa namuota siku zote, sifa zote unazopenda anazo pengine unamueleza hisia zako naye anakuelewa. Lakini kinachotokea unakuta kashazalishwa na mbaya zaidi baba mtoto bado yupo hai😃😃

Kuna muda mpaka unatamani ubebe kimya kimya tu, ila ukitafakari zaidi unaona ni heri nusu shari kuliko shari kamili.
Sikuambii huyo ni mke mwema ama mbaya mchunguze tabia yeye kama yeye.
Naona wadau wengi wakisema hao single mothers hawafai kwa hoja :
1. Hakuna mwanaume anaacha wife material
2. Atakumbushia na baba mtoto wake.
Ina maana wanaume wote huwa hawadanyanyi kwenye mahusiano? Mfano ana wanawake 3 wote wana tabia njema pengine kazaa na 2 mwisho akioa 1 hao wawili walobaki na aliwadanyanya why wahukumiwe life time?
Mwanamke au mwanaume yeyote ambaye sio bikra ukikutana naye kama hana msimamo binafsi ataendelea na ma ex zake hata kama hawajazaa.
Zipo kesi nyingi wanawake walioolewa bila kuwa single mothers hapo awali wana cheat na exs wao, wapenzi wapya n.k.
NB Mwanamke au mwanaume yoyote katika makuzi anaweza kukosea katika mahusiano hasa ya ujanani akazaa/kuzalisha mtu na mahusiano yale yasifanikiwe. Hii haimfanyi asifae kuwa mke/mume bora people learn,change and move on.
Malaya ni malaya tu awe amezaa au hajazaa
Usimpotoshe mwenzako,we hujiulizi kwa nn baba wa mtoto kamshindwa?
 
Back
Top Bottom