introvert
JF-Expert Member
- Sep 21, 2010
- 1,372
- 2,416
Hakuna aliyetegemea uchaguzi uwe wa huru na haki. Lakini hakuna aliyetegemea wizi uwe wa wazi na wa kijinga hivi.
Chama Cha Mapinduzi, kama chama kikongwe barani Afrika, kimethihirisha hakipo tayari kuachia madaraka kwa njia ya sanduku la kura. Si Bara wala si Visiwani.
CCM si chama cha siasa tena, CCM ni mfumo uliyoishikilia nchi hii mateka. Hamna tofauti na CCP China, Putin’s Russia, Kim’s Korea, Castro’s Cuba, Lukashenko’s Belarus, n.k. Mifumo ya kisoshalisti na kikomunisti iliyoasisiwa na Mwalimu Nyerere.
CCM kwanza, Tanzania baadae. Wakuu wa vyombo vya dola pamoja na wakuu wa majeshi wapo kulinda kwanza maslahi ya Mwenyekiti wa CCM kisha CCM na mwisho Tanzania.
Kwao adui wa Mwenyekiti wa CCM ni adui wa Tanzania. Adui wa Chama ni adui wa Tanzania.
Huu uchaguzi ni kichekesho kingine kama ilivyokuwa 1995, 2000, 2005, 2010 na 2015. Mawakala wa vyama vya upinzani wanakamatwa na kutolewa kwenye vituo. Kura feki kwenye mabegi na maboksi zinaingizwa kujumuishwa kwenye mahesabu.
Haya yanasimamiwa na wakurugenzi, wakuu wa wilaya, wakuu wa Usalama wa Taifa na wakuu wa mikoa. Nani mnamdanganya?
Majeraha ya Uchaguzi huu, tofauti na miaka mingine, ni mpasuko mkubwa na kuhatarisha umoja wa nchi.
Watu wameenda kupiga kura ili roho zao ziwe na amani tu, haijalishi mtaiba kura zao au la! Hii ni chuki kubwa imepandwa.
Kibaya zaidi tofauti na watangulizi wa nyuma, Rais Magufuli hajui na hawezi kuunganisha Taifa kwa kauli na matendo yake na amezungukwa na wabinafsi wa hali ya juu.
Ni rahisi kushangilia na kusema wameshinda na kuwagaragaza wapinzani.
Ni rahisi kwa wachambuzi wa mambo ya siasa kusema "Upinzani bado sana" au "Upinzani haukujipanga". Unabaki kujiuliza, kwa mazingira haya unategemea upinzani ujipange vipi ili kuwe na haki.
Media zote zimefungwa mdomo. Hakuna uchambuzi, sharia ni kusoma kile watawala wanataka basi.
Mediocrity (Sabaya, Makonda, Mambosasa, Polepole, Kabudi et al) is the order of the day. Short-termism is the norm.
Ipi gharama ya ushindi huu kwa CCM? Kupasua umoja wa nchi? Kutumia silaha na nguvu kuhalalisha ushindi hakukupi ushindi bali kunakuongezea maadui.
Mfano leo hii Kusini kuna tishio la Ugaidi bado tena unawaibia hao watu haki yao ya kuchagua viongozi wanaowataka. Wakuu wa Usalama na Ulinzi wanategemea nini?
Inasikitisha haya yanafanywa na tume iliyoundwa na Majaji na Wasomi. Haya yanasimamiwa na Majenerali wa vyombo vya Ulinzi na Usalama. Hii yote ni kumfurahisha Mwenyekiti.
Imemchukua Baba wa Taifa zaidi ya miaka 20 na Watanzania wamepitia sacrifices nyingi kujenga Umoja katika nchi hii.
CCM Mpya chini ya miaka 5, inafanikiwa kuvunja hii legacy na kujisifu wao ni wazalendo.
Nchi inaingia kwenye giza kubwa na kuishi mawazo ya mtu mmoja tu ambaye si mwerevu.
Taifa linaelekea kwenye mpasuko mkubwa tokea tupate Uhuru.
Chama Cha Mapinduzi, kama chama kikongwe barani Afrika, kimethihirisha hakipo tayari kuachia madaraka kwa njia ya sanduku la kura. Si Bara wala si Visiwani.
CCM si chama cha siasa tena, CCM ni mfumo uliyoishikilia nchi hii mateka. Hamna tofauti na CCP China, Putin’s Russia, Kim’s Korea, Castro’s Cuba, Lukashenko’s Belarus, n.k. Mifumo ya kisoshalisti na kikomunisti iliyoasisiwa na Mwalimu Nyerere.
CCM kwanza, Tanzania baadae. Wakuu wa vyombo vya dola pamoja na wakuu wa majeshi wapo kulinda kwanza maslahi ya Mwenyekiti wa CCM kisha CCM na mwisho Tanzania.
Kwao adui wa Mwenyekiti wa CCM ni adui wa Tanzania. Adui wa Chama ni adui wa Tanzania.
Huu uchaguzi ni kichekesho kingine kama ilivyokuwa 1995, 2000, 2005, 2010 na 2015. Mawakala wa vyama vya upinzani wanakamatwa na kutolewa kwenye vituo. Kura feki kwenye mabegi na maboksi zinaingizwa kujumuishwa kwenye mahesabu.
Haya yanasimamiwa na wakurugenzi, wakuu wa wilaya, wakuu wa Usalama wa Taifa na wakuu wa mikoa. Nani mnamdanganya?
Majeraha ya Uchaguzi huu, tofauti na miaka mingine, ni mpasuko mkubwa na kuhatarisha umoja wa nchi.
Watu wameenda kupiga kura ili roho zao ziwe na amani tu, haijalishi mtaiba kura zao au la! Hii ni chuki kubwa imepandwa.
Kibaya zaidi tofauti na watangulizi wa nyuma, Rais Magufuli hajui na hawezi kuunganisha Taifa kwa kauli na matendo yake na amezungukwa na wabinafsi wa hali ya juu.
Ni rahisi kushangilia na kusema wameshinda na kuwagaragaza wapinzani.
Ni rahisi kwa wachambuzi wa mambo ya siasa kusema "Upinzani bado sana" au "Upinzani haukujipanga". Unabaki kujiuliza, kwa mazingira haya unategemea upinzani ujipange vipi ili kuwe na haki.
Media zote zimefungwa mdomo. Hakuna uchambuzi, sharia ni kusoma kile watawala wanataka basi.
Mediocrity (Sabaya, Makonda, Mambosasa, Polepole, Kabudi et al) is the order of the day. Short-termism is the norm.
Ipi gharama ya ushindi huu kwa CCM? Kupasua umoja wa nchi? Kutumia silaha na nguvu kuhalalisha ushindi hakukupi ushindi bali kunakuongezea maadui.
Mfano leo hii Kusini kuna tishio la Ugaidi bado tena unawaibia hao watu haki yao ya kuchagua viongozi wanaowataka. Wakuu wa Usalama na Ulinzi wanategemea nini?
Inasikitisha haya yanafanywa na tume iliyoundwa na Majaji na Wasomi. Haya yanasimamiwa na Majenerali wa vyombo vya Ulinzi na Usalama. Hii yote ni kumfurahisha Mwenyekiti.
Imemchukua Baba wa Taifa zaidi ya miaka 20 na Watanzania wamepitia sacrifices nyingi kujenga Umoja katika nchi hii.
CCM Mpya chini ya miaka 5, inafanikiwa kuvunja hii legacy na kujisifu wao ni wazalendo.
Nchi inaingia kwenye giza kubwa na kuishi mawazo ya mtu mmoja tu ambaye si mwerevu.
Taifa linaelekea kwenye mpasuko mkubwa tokea tupate Uhuru.