Jazzie
Member
- Jan 30, 2008
- 73
- 35
KOMBOLELA SHOW JUMAMOSI HII Desemba 4, 2010 @ 01:00pm - 02:00pm EST, 9:00pm -10:00pm East African Time
Kama wewe ni mfuatiliaji wa mambo ya kisiasa, mojawapo wa mambo yametokea siku za karibuni ni uanzishaji wa matawi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) nje ya mipaka ya Tanzania kama vile India, Uingereza, n.k. Kujiunga na chama chochote ni haki ya kikatiba ya kila Mtanzania, kwa hiyo uanzishaji wa matawi ya chama chote chote cha siasa nje ya Tanzania sio kosa, hasa uanzishaji wa matawi unapokuwa hauvunji sheria ya nchi hizo za nje.
Tatizo, pengine ni hisia kwamba waanzishaji haya matawi ya chama nchi za nje, hasa ya CCM, ni wasaliti wa watanzania wengi ambao ni masikini. Hilo linatokana na matarajio kwamba Mtanzania ambaye amefanikiwa kutoka nje ya nchi amepanuka kimtazamo na kwamba mtu ambaye amepanuka kimtazamo na ana ujasiri, hawezi kukiunga mkono CCM, chama ambao kimekuwa madarakani muda mrefu bila kuleta maendeleo ya kweli kwa mtanzania masikini.
Radio Mbao kupitia Kombolela Show itakuwa na mahojiano na Maina Owino ambaye ni Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) tawi la Uingereza ili kufahamu mtazamo wake juu ya uanzishaji wa matawi ya CCM nchi za nje.
Jiunge kusikia mazungumzo kupitia hapa: Radio Mbao ili usikose uhondo!
Kama wewe ni mfuatiliaji wa mambo ya kisiasa, mojawapo wa mambo yametokea siku za karibuni ni uanzishaji wa matawi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) nje ya mipaka ya Tanzania kama vile India, Uingereza, n.k. Kujiunga na chama chochote ni haki ya kikatiba ya kila Mtanzania, kwa hiyo uanzishaji wa matawi ya chama chote chote cha siasa nje ya Tanzania sio kosa, hasa uanzishaji wa matawi unapokuwa hauvunji sheria ya nchi hizo za nje.
Tatizo, pengine ni hisia kwamba waanzishaji haya matawi ya chama nchi za nje, hasa ya CCM, ni wasaliti wa watanzania wengi ambao ni masikini. Hilo linatokana na matarajio kwamba Mtanzania ambaye amefanikiwa kutoka nje ya nchi amepanuka kimtazamo na kwamba mtu ambaye amepanuka kimtazamo na ana ujasiri, hawezi kukiunga mkono CCM, chama ambao kimekuwa madarakani muda mrefu bila kuleta maendeleo ya kweli kwa mtanzania masikini.
Radio Mbao kupitia Kombolela Show itakuwa na mahojiano na Maina Owino ambaye ni Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) tawi la Uingereza ili kufahamu mtazamo wake juu ya uanzishaji wa matawi ya CCM nchi za nje.
Jiunge kusikia mazungumzo kupitia hapa: Radio Mbao ili usikose uhondo!