Maige awashukia viongozi wa Tanapa

Rutashubanyuma

JF-Expert Member
Sep 24, 2010
219,422
911,172
Maige awashukia viongozi wa Tanapa


na Hellen Ngoromera


amka2.gif
WAZIRI wa Maliasili na Utalii, Ezekiel Maige, amewakemea viongozi wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) na kuwataka kuepuka matumizi ya fedha yasiyoendana na shughuli za uhifadhi hasa ufanyaji wa safari za nje zisizo na tija. Alikemea pia ununuzi wa magari ya kifahari na kusema anataka kuona ununuzi wa magari unafanyika hasa kwa magari ya porini pekee.
Maige alisema hayo jana jijini Dar es Salaam mbele ya waandishi wa habari muda mfupi baada ya kumaliza kufanya kikao cha pamoja na bodi ya TANAPA.
“Epukeni matumizi ya fedha yasiyoendana na uhifadhi, safari za nje na posho za ajabu ajabu, msiruhusu pia ununuzi wa magari ya kifahari,” alisema Waziri Maige.
Kwa mujibu wa waziri huyo, haimwingii akilini kumwona kiongozi wa wizara akishiriki kwenye maonyesho kwa wiki mbili katika nchi fulani bila manufaa na kwamba hali hiyo inamkera.
Badala yake aliitaka TANAPA kuelekeza nguvu zake kuajiri askari wengi wa wanyamapori ili kuongeza tija katika utendaji kazi wa askari hao katika kudhibiti majangili.
Aliwataka pia kupitia upya rasilimali walizonazo pamoja na pia kuweka mipango thabiti ya muda mfupi kupambana na vitendo vya ujangili.
 
Maige awashukia viongozi wa Tanapa


na Hellen Ngoromera


amka2.gif
WAZIRI wa Maliasili na Utalii, Ezekiel Maige, amewakemea viongozi wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) na kuwataka kuepuka matumizi ya fedha yasiyoendana na shughuli za uhifadhi hasa ufanyaji wa safari za nje zisizo na tija. Alikemea pia ununuzi wa magari ya kifahari na kusema anataka kuona ununuzi wa magari unafanyika hasa kwa magari ya porini pekee.
Maige alisema hayo jana jijini Dar es Salaam mbele ya waandishi wa habari muda mfupi baada ya kumaliza kufanya kikao cha pamoja na bodi ya TANAPA.
“Epukeni matumizi ya fedha yasiyoendana na uhifadhi, safari za nje na posho za ajabu ajabu, msiruhusu pia ununuzi wa magari ya kifahari,” alisema Waziri Maige.
Kwa mujibu wa waziri huyo, haimwingii akilini kumwona kiongozi wa wizara akishiriki kwenye maonyesho kwa wiki mbili katika nchi fulani bila manufaa na kwamba hali hiyo inamkera.
Badala yake aliitaka TANAPA kuelekeza nguvu zake kuajiri askari wengi wa wanyamapori ili kuongeza tija katika utendaji kazi wa askari hao katika kudhibiti majangili.
Aliwataka pia kupitia upya rasilimali walizonazo pamoja na pia kuweka mipango thabiti ya muda mfupi kupambana na vitendo vya ujangili.

Maige naye kumbe wamo.Ila tusubiri tuone,isije ikawa maneno matupu yasiyo na tija kama ADNIP.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom