Mahusiano ya Kimataifa: Rais Magufuli amefungua balozi mpya katika nchi 8 ikiwemo Israel, Mungu ambariki sana!

JPM ameleta magomvi na nchi majirani.

CHADEMA itarejesha mahusiano mema na majirani zetu ili BIASHARA zimeweze kushamiri.
Alichofanya JPM kwa hao majirani ni kukataa ukondoo.

Sasa chadema wengi kwa vile wanapenda ukondoo ndio maana wanaona ni ugomvi
 
Kwa ufupi kabisa kwa wale CHADEMA pamoja na Tundu Lisu mnaodai Rais Magufuli amefifisha mahusiano na dunia nataka niwakumbushe tu Rais Magufuli amefungua balozi katika nchi nane duniani ikiwemo Israel.

Tunapokosoa jambo tuwe tunaweka na uhalisia wa ukosoaji siyo kukurupuka.

Hata Ethiopia alikoishi Simon wa Kirene imefungua ubalozi wake Tanzania awamu hii ya Rais Magufuli.

Mungu wa mbinguni mbariki Rais Magufuli.

Maendeleo hayana vyama!
Hawa jamaa inje ya kunadi matusi, hawana Sera mwaka huuu...

Wao walitaka magufuli ashinde kujipendekeza kwenye maiki za wazungu, ndo wangeona kuwa diplomasia ya kimataifa imeimalikaa
 
..Jpm ametugombanisha na majirani zetu wa sadc na eac.

..Jpm anatukana marafiki zetu wa muda mrefu wa ulaya na america.

..ni kweli amefungua balozi 8 mpya, lakini ameharibu mahusiano yetu na nchi na jumuiya lukuki za kimataifa.

..kufungua ofisi za ubalozi ni jambo moja, kuwa na mahusiano mazuri na nchi mbalimbali ni jambo tofauti.
Anafungua balozi nyingi ili apate mahali wa kuwaficha wabaya wake wanaomkosoa
kuna haja gani kuwa na balozi ambazo huna mahusiano ya kiitifaki?
 
..matokeo yake anaua biashara mpaka za waTz.
Kama ni kufa kwa biashara chache kwa ajili ya kukataa ukondoo wacha zife!

Hata yule mgombea aliekuja na beberu wake tunamungalia tu! Tutamfundisha oktoba hii kama hii nchi ni huru.
 
Kama ni kufa kwa biashara chache kwa ajili ya kukataa ukondoo wacha zife!

Hata yule mgombea aliekuja na beberu wake tunamungalia tu! Tutamfundisha oktoba hii kama hii nchi ni huru.

..ccm mna hoja za bora tukose wote.

..hao wachache wangeweza kusaidia wengine wengi.
 
Ameuwa na kuwapoteza wengi sana, hasa wale anao tofautiana nao na hajawai omba msamaa, hivyo anapaswa abidhiwa kisawa sawa
 
..ccm mna hoja za bora tukose wote.

..hao wachache wangeweza kusaidia wengine wengi.
Ni national interest zaidi!

Unapoona mchina ana vimbiana na USA unafikiri hafikirii habari ya raia wake?
 
Kwa ufupi kabisa kwa wale Chadema pamoja na Tundu Lisu mnaodai Rais Magufuli amefifisha mahusiano na dunia nataka niwakumbushe tu Rais Magufuli amefungua balozi katika nchi nane duniani ikiwemo Israel.

Tunapokosoa jambo tuwe tunaweka na uhalisia wa ukosoaji siyo kukurupuka.

Hata Ethiopia alikoishi Simon wa kirene imefungua ubalozi wake Tanzania awamu hii ya Rais Magufuli.

Mungu wa mbinguni mbariki Rais Magufuli.

Maendeleo hayana vyama!
Jinga letu jingine hili, kufungua ubalozi siyo sifa Bali iwe kwa mahitaji ya wakati kwa sababu uendeshaji wake ni gharama kubwa kwa nchi. Kuna balozi zetu nyingine ni mizigo tu kwa Taifa kwa kuwa zimefunguliwa katika nchi zisizo na maslahi makubwa kwa nchi yetu au wafanyakazi wake ni dhaifu kama hawa wanaoteuliwa Serikalini kwa upendeleo. Mleta mada hakutaja hizo nchi 8 lakini ametaja Israel ambayo nchi yetu ingekuwa imenufaika sana kama ubalozi ungefunguliwa miaka 30/40 iliyopita. Hapohapo Mashariki ya Kati kuna balozi zetu nyingi zingefaa kuwa kwingineko kwenye fursa na sababu nyingi zaidi, mfano Amerika Kusini nchi nyingi muhimu tuna Ubalozi mmoja. Rais wetu mpendwa alipoingia tu madarakani aligawa kwa Balozi za nchi za nje Hati Miliki za viwanja vya kujenga Balozi zao Dodoma haijulikani ngapi tayari zimehamia ila kuna Balozi hapa ofisi zao zikiwa nchi jirani. Kusifu kwa kusifu tu ni ujinga mpaka unafanya anayesifiwa aonekane mjinga.
 
JPM ameleta magomvi na nchi majirani.

CHADEMA itarejesha mahusiano mema na majirani zetu ili BIASHARA zimeweze kushamiri.
Haiwezekani ufiwe na mtu kama Mkapa(R.I.P) halafu hakuna jirani hakuna wa mbali na nchi was declared COVID-19 free
 
Ndani ya hii miaka mitano nchi imeongeza idadi kubwa ya wajinga, waoga, watu wa kujipendekeza na watu wasiojiamini. Hili ni tatizo kubwa mno mtu kutaka asujudiwe peke yake na sauti yake iwe ni amri na sheria.

Yatosha sasa !!
 
Kwa ufupi kabisa kwa wale CHADEMA pamoja na Tundu Lisu mnaodai Rais Magufuli amefifisha mahusiano na dunia nataka niwakumbushe tu Rais Magufuli amefungua balozi katika nchi nane duniani ikiwemo Israel.

Tunapokosoa jambo tuwe tunaweka na uhalisia wa ukosoaji siyo kukurupuka.

Hata Ethiopia alikoishi Simon wa Kirene imefungua ubalozi wake Tanzania awamu hii ya Rais Magufuli.

Mungu wa mbinguni mbariki Rais Magufuli.

Maendeleo hayana vyama!
Simoni wa Kirene hakuishi Ethiopia acha udanganyifu. Simon of Cyrenaica alikuwa ni mtu wa Pwani ya Libya. I think ni maeneo around Sirte ya sasa.
 
Ni kweli ameiwezesha na Tanzania kutoa misaada kwa nchi mbali mbali, donors country
Wakati wa Maafa ya mafuriko, Msumbiji na Zimbabwe tulitoa msaada. Hata China alipopatwa na Corona tulitoa msaada, sema China mwenyewe akasema tutamsaidia muda mwingine kwa wakati huo alikuwa anaweza kukabili janga hilo. Nadhani, mnakumbuka balozi wa china alivyotoa shukrani kwa Tanzania kwa kuonyesha utayari wa kuwasaidia. Tanzania siyo ya kisport sport, ujue!
 
Kwa ufupi kabisa kwa wale CHADEMA pamoja na Tundu Lisu mnaodai Rais Magufuli amefifisha mahusiano na dunia nataka niwakumbushe tu Rais Magufuli amefungua balozi katika nchi nane duniani ikiwemo Israel.

Tunapokosoa jambo tuwe tunaweka na uhalisia wa ukosoaji siyo kukurupuka.

Hata Ethiopia alikoishi Simon wa Kirene imefungua ubalozi wake Tanzania awamu hii ya Rais Magufuli.

Mungu wa mbinguni mbariki Rais Magufuli.

Maendeleo hayana vyama!
Naona unajitahidi kupost, endelea kukaza nuts labda inaweza saidia
 
Kwa ufupi kabisa kwa wale CHADEMA pamoja na Tundu Lisu mnaodai Rais Magufuli amefifisha mahusiano na dunia nataka niwakumbushe tu Rais Magufuli amefungua balozi katika nchi nane duniani ikiwemo Israel.

Tunapokosoa jambo tuwe tunaweka na uhalisia wa ukosoaji siyo kukurupuka.

Hata Ethiopia alikoishi Simon wa Kirene imefungua ubalozi wake Tanzania awamu hii ya Rais Magufuli.

Mungu wa mbinguni mbariki Rais Magufuli.

Maendeleo hayana vyama!
Huko si alikuwa anawatafutia ndugu zake kazi za kufanya.
 
Unasema nchi nane halafu unaishia kutaja Israel! Hivi unadhani ubalozi ndio mahusiano?? Hata US ina mahusiano ya kibalozi na Zimbabwe lakini ndio inaongoza nchi zinazoiwekea vikwazo!!!
 
Kwahiyo akihitaji kuwasiliana na rais wa ufaransa itabidi ajifunze Kwanza kifaransa. Na akihitaji kuwasiliana na viongozi wa china itabidi ajifunze kichina Kwanza?

kweli Tanzania tuanahitaji jambo la ziada Kwenye elimu yetu maana haitufunzi kufikiri
Nyerere aliwahi kusema '' kiingereza ndicho kiswahili cha dunia'' Ukijua kuwasiliana kiingereza utaweza kuwsiliana na wengine pia hata kama hawaongei kiingereza.
Ni hivi tuna kiswahili, halafu kuna Wachina. Ili tuwasiiane kutakuwa na mkalimani anayejua kiingereza. Umeelewa?
 
..hivi lile zoezi la kuzifanya nchi za Sadc zizungumze Kiswahili limefikia wapi?

..ndiyo maana tunasisitiza kwamba kufungua ofisi za ubalozi ni jambo moja, lakini kuwa na mahusiano mema, na kutumia fursa za kidiplomasia ni jambo lingine.

..Mara ya kwanza Jpm kwenda kusini mwa Afrika alikusanya kamusi za Kiswahili na kwenda kumbwagia Raisi Ramaphosa akimtaka ajifunze Kiswahili!! Badala ya kuzungumzia fursa za kiuchumi na kibiashara yeye amedata kwenye kuficha madhaifu yake ya lugha.
Hoja ya kufunga balozi inatumika sana kuziba pengo ambalo kila mmoja analijua, tumepwaya sana katika diplomasia. Hatuhitaji kuwa na balozi tunahitaji kuwa na diplomasia.

Kuna hoja ya ubalozi wa Israel. Ubalozi wa Israel ulifunguliwa kwa ''hoja za kiimani'' si kiuchumi.
Ukitaka kujua hilo mfuatilie kwa ukaribu Gwajima na kauli zake. Gwajima anaamini sana katika Israel na kuitukuza sana. Hakuna anayeeleza kwanini tumerudisha uhusiano na Israel, kwa faida gani.

Israel ni nchi ndogo sana, na kwa wasiojua ni ndogo kuliko mkoa wa Morogoro. Sasa unaposikia watu wa liinchi likubwa kama Tanzania wanajinasuibu na kufungua ubalozi ni kutukana akili zetu.
 
Back
Top Bottom