Hivi karibuni nilisoma katika tovuti ya Michuzi kuwa Waisraeli wanataka kusaidia miradi mbalimbali Tanzania. Kwa bahati mbaya niliandika maoni kama blog wa Michuzi lakini inaonekana Michuzi ni mtu wa system kwa hiyo maoni yangu ambayo nayaambatanisha hapa, akayatia kapuni.
Nikajaribu kumuomba ndugu Mjengwa katika blog yake nae pia hakuweza kuyaweka. Nikajua kuwa wote wanaganga njaa na hawako serious na kutoa forum kwa wananchi kutoa maoni yao. Haya hapa ndio maoni yangu kuhusu uhusiano wa Tanzania na Israel.
Kitu kimoja kinanishangaza sana kuhusu hawa Waisraili.Udhalimu wanaoufanya kwa wapalestina wanapata wapi utu wa kuja kusaidia miradi ya Tanzania? Hapa lipo neno.
Waisraili wanataka kudhibiti chanzo cha maji ya mto Nile ili kuwaadhibisha na kuwatia shindikizo watu wa Misri ambao uhai wao unategemea maji ya mto Nile. Walienda kwa Uganda na kufanikiwa. Huko walijenga bwawa kubwa linalotumia maji ya ziwa Victoria. Sasa wako Tanzania. Si kweli kuwa wana nia ya dhati ya kusaidia miradi, wana lao hawa. Wanachokitaka ni kuona maji ya Ziwa Victoria yanatumiwa sana ili kupunguza kina cha maji cha mto Nile na baadae kuifanya Misri ikose maji ya kutosha. Hii itawawezesha wao kuipiga kabari Misri ambayo kuna wakati hufurukuta ili kuwasaidia Wapalestina. Kwa mfano hivi karibuni Misri iliruhusu msafara wa misaada unaoelekea Gaza kupita nchini mwao. Jambo kama hili haliipendezi serikali ya Israel.
Kwahiyo uhusiano huu na Israel una neno. Najua ingekuwa ni kipindi cha mwalimu Nyerere na uhai wa Yasser Arafat wasingeweza kuja kuingia kirahisi Bongo kutokana na msimamo wa mwalimu. Lakini mwalimu Nyerere hatunae tena na Yasser Arafat pia kwahiyo Israel wameutumia huu mwanya.
Je, wadau wengine wanasemaje?
=========
Januari 2011:
July 2014:
Nikajaribu kumuomba ndugu Mjengwa katika blog yake nae pia hakuweza kuyaweka. Nikajua kuwa wote wanaganga njaa na hawako serious na kutoa forum kwa wananchi kutoa maoni yao. Haya hapa ndio maoni yangu kuhusu uhusiano wa Tanzania na Israel.
Kitu kimoja kinanishangaza sana kuhusu hawa Waisraili.Udhalimu wanaoufanya kwa wapalestina wanapata wapi utu wa kuja kusaidia miradi ya Tanzania? Hapa lipo neno.
Waisraili wanataka kudhibiti chanzo cha maji ya mto Nile ili kuwaadhibisha na kuwatia shindikizo watu wa Misri ambao uhai wao unategemea maji ya mto Nile. Walienda kwa Uganda na kufanikiwa. Huko walijenga bwawa kubwa linalotumia maji ya ziwa Victoria. Sasa wako Tanzania. Si kweli kuwa wana nia ya dhati ya kusaidia miradi, wana lao hawa. Wanachokitaka ni kuona maji ya Ziwa Victoria yanatumiwa sana ili kupunguza kina cha maji cha mto Nile na baadae kuifanya Misri ikose maji ya kutosha. Hii itawawezesha wao kuipiga kabari Misri ambayo kuna wakati hufurukuta ili kuwasaidia Wapalestina. Kwa mfano hivi karibuni Misri iliruhusu msafara wa misaada unaoelekea Gaza kupita nchini mwao. Jambo kama hili haliipendezi serikali ya Israel.
Kwahiyo uhusiano huu na Israel una neno. Najua ingekuwa ni kipindi cha mwalimu Nyerere na uhai wa Yasser Arafat wasingeweza kuja kuingia kirahisi Bongo kutokana na msimamo wa mwalimu. Lakini mwalimu Nyerere hatunae tena na Yasser Arafat pia kwahiyo Israel wameutumia huu mwanya.
Je, wadau wengine wanasemaje?
=========
Januari 2011:
Habari wa Jf,
Nimesikia Tanzania ilivunja uhusiano na Israel tangu 1960, jambo hili limenishtua kidogo kwa kufuatana na kitabu cha dini ninachokiamini kinasema ANAYEMBARIKI ISRAEL ANABARIKIWA NA UKIMLAANI UNALAANIWA NA MUNGU, nisaidieni jamani kwa anayejua kama tuna balozi hapa Tanzania.
Pole sana umepewa majibu laini sana ila ni kwamba kipindi fulani wakati wa utawala wa nyerere israel ilishambulia wapalestina sana na kuua watu wengi, sasa kwa vile nyerere alikua hapendi ukandamizani kama unaofanywa na marekani huko libya, alivunja uhusiano na israel kama inshara ya kupinga vitendo vyao dhidi ya wapalestina! Kabla ya hapo uhusiano ulikua safi sana, wao ndio waliojenga majengo ya maana ya zamani hapa dar es salaam kama kitega uchumi, jengo la ushirika, chuo kikuu cha dar es salaam na hospitali ya bugando mwanza!, sina uhakika na muhimbili ila nadhani ndio wenyewe! na ubalozi wao ulikua pale ubalozi wa marekani uliolipuliwa na magaidi ulipo! Shughuli zao za kijasusi kwa tanzania walitumia ubalozi wa marekani!
Waumini wa biblia wanasema tanzania ina laana kwani imeandikwa atakaemlaani israel amelaaniwa! Karibu sana
Serikali ya Nyerere ilivunja uhusiano na Israel mwaka 1967 kwa sababu Israel iliikalia Sinai Peninsula baada ya Six Day War.
Nasikia kabla ya hapo Israel walikuwa wametusaidia kwenye ujenzi wa majengo kadhaa likiwemo jengo la makao makuu ya Usalama wa Taifa to name the few.
Agosti 2012:With my little knowledge ubalozi wao ulikuwepo na ndiyo waliotujengea miundombinu kama ya AICC- kule Arusha; Bugando hospital MWanza na sehemu nyingi hasa public buildings na kulikuwepo na kampuni moja ikiitwa COSATA hii kampuni ni ya kiyahudi.
Ikumbukwe pia baada ya vile vita ya ^6 days war Wayahudi walikuja kumfuta JK na kumwuliza kama angependa kuuchimba mfereji wa kumwagilia kilimo cha mizabibu kule Dodoma na kumwagilia vijiji vya jirani basi wangeweza kuuchimba huo mfereji utakaomwaga maji yakitokea Lake Victoria kupitia Nyarugusu kote huko Igunga mpaka singida hadi Dom pia hata meli ndogo zingeweza kuutumia na kumaliza zogo la usafiri na samaki. Hata hivyo JK kushauriana na wakandarasi wake ndani ya ikulu walimweleza this is an issue kwani ziwa victoria liko mlimani na linamwaga maji kuelekea bondeni maana yake ukichimba mfereji kwa upande wa kusini unakausha Nile river and its tributaries na ndo mwi=sho wa Misri kwani Nile is Egypt and egypt is Nile.
Wamisri wakawa ndo victims wa vita vya 6 days war kwani they are one hosted that military base. Ndo hata juzi kama umeona wamisri walipoandamana kwenye ubalozi wao hata waliochukua nchi hawakusema kitu kwani wanajua kuna nini kitatokea wakiuvunja ule mkataba wa mwaka 1972. nao wayahudi hawajsema kama watauhamisha ubalozi wao kutoka Misri au la.. pengine kuna alieye na mpya zaidi kuhusu hii point ya Israili na egypt jamani atujuze..
Turudi kwenye point kule juu . Sisi ni taifa lisilofungamana na upande wowote, lina watu wake wenye dini tofauti na lenye kufuta haki za binadamu na halina dini kikatiba wala ubaguzi wa rangi. Mwaka 1975s bila kukosea kulitokea mauaji ya watoto wachanga wasiojua dini wala siasa waliuawa kule Gaza yaani mauaji ya kimbari yaliyo hitimishwa na majeshi ya Kiyahudi.
Wazee wakamfuata JK na kumwuuliza mbona sisi ni nchi ya watu isio na katiba ya dini na tunaheshimu nchi nyingine na zisizo fuata haki za binadamu siyo marafiki wetu? iweje hawa marafiki wetu wawauwe watoto wasio na dhambi na wasio jua dini wala siasa? kweli tuwakubali hawa watu??. Isareli haikujutia lile jaribio wala kuomba msamaha kwa watu Kipalestina.
Kambarage siku iliyofuata akina Butiku wakamweleza mzee chomoa ubalozi kule na waite Wapalestina. Ndo mpaka leo tunaitambua mamlaka ya kipalestina hapo Bongo.
Aprili 2013:Swali la Asumpta Mshana; ameuliza "Kwanini Tanzania haina balozi nchini Israel, ikizingatiwa kuwa watanzania wengi wanaenda Israel kwa masuala ya kiimani na kibiashara?"
Naibu waziri amejibu kuwa Tanzania ina balozi Israel, lakini anaiwakilisha kutoka Misri.
kaaazi kweli!
Asikofu Gamanywa leo kasema Tanzania haiwezi kufanikiwa kiuchumi na kisiasa sababu haina mahusiano mazuri na Israel. Kasema mataifa makubwa yote yana mahusiano mazuri na Israel ya kiuchumi.
Kayataja Marekani, China, Japan, India, Ujerumani, Urusi, Brazil, Uingereza, Ufaransa na Italia; lakini Tanzania haina hata balozi israel.
2% ya wamarekani ni wayahudi.
Ametoa ujumbe kwa serikali ya Tanzania kufungua mahusiano na Israel. Tuache kuingilia ugomvi wa Ishmael na Isaka sisi hautuhusu kasema Askofu.
=====
Askofu Gamanywa anasema tukiwa connected na Isaka, baraka za kiuchumi zitakuja.
Gamanywa anasema pigeni kelele na Israel lakini pataneni na Israel kiuchumi kama mataifa mengine ili Tanzania ifanikiwe.
Amesema Ishmail ni mwarabu na Isaka ndipo baraka zetu zilipo kutokana na mandiko katika biblia. Sisi ugomvi wa waarabu na wayahudi hautuhusu.
Tunachotakiwa ni kuinuka kiuchumi na hiyo haiwezekani bila kuwa na mahusiano mazuri na Israel. Waisrael wameahidiwa kuwa kichwa na sio mkia katika biashara.
July 2014:
TZ mnasema hakuna Balozi wa Israel na hapa kama picha inavyoonesha ni kwamba Balozi Seif Idi anamkabidhi zawadi ya mlango Balozi wa Israel nchini TZ baada ya kumaliza muda wake.