Mahusiano Forums: Read b4 u post

Invisible

Robot
Feb 11, 2006
9,075
7,878
Kwanza nikuombeni radhi nyote ambao mlikuwa mmeandika michango yenu na ikazimika ghafla. Ni kutokana na matatizo ya kiutendaji. Forum hii inahitaji mod mwenye busara kubwa kuwahudumia wanachama wake.

Tuliamua kuiweka offline kwa muda kuangalia uwezekano wa kuirejesha kwa mtizamo chanya ambao tunaamini mtatuelewa na kutilia maanani mapendekezo yetu.

Mapendekezo yetu yako hivi:

1. Kutakuwa na uchelewaji wa kutoa majibu moja kwa moja katika majukwaa (forums) mengi kutokana na uwingi wa michango inayoandikwa kila siku JF. Hivyo uwezekano wa kupata majibu ya haraka toka kwa viranja ama mods kama tulivyozoea kuwaita utakuwa mdogo. Tunaomba wanachama ambao wanajua nafsi zao ziko 'dedicated' katika kuwasaidia wenzao watusaidie kuwajibu na kuhakikisha kila kitu kinaenda salama. Hatutarajii matusi na kashfa kama ilivyotokea kwenye forum ya Dini. Heshimianeni.

2. MUHIMU SANA: Picha za uchi; video za uchi ama ngono hazitaruhusiwa hapa. Ukitaka kufanya mambo kama hayo tafadhali omba ruksa ya kutembelea Jukwaa la 'Mambo ya Kikubwa'. Huendi huko kirahisi bila kuomba kibali maalum na kuidhinishwa. Hatutamvumilia atakayeweka picha za uchi eneo hili ama video za ngono. Atafungiwa kwa muda usiopungua juma moja.

3. Lugha kali za mapenzi ikiwa ni pamoja na zile zisizokuwa na tafsida zitafutwa na mwanachama aliyetoa kauli husika atachukuliwa hatua kali ikiwa ni pamoja na kufungiwa. Sehemu za siri ziitwe hivyo na tusipende kuita koleo kuwa koleo. Ieleweke wazi kuwa hili ni jukwaa huru na wanatembelea watoto. Waonee huruma kuwaharibia maisha. Vinginevyo tutafunga moja kwa moja jukwaa hili kwa kukiuka kipengele hiki. Mtoto wa mwenzio si mkubwa mwenzio; mlee alinufaishe taifa.

Mwisho nawatakia mijadala myema na kuwatakia ufanisi katika kila mfanyalo katika mwaka 2008 na miaka ijayo.

Invisible
For JF Management
 
Naambiwa HII FORUM IFUTWE HARAKA SANA. Mnaafiki ama mnasemaje? Aidha nadhani ni vema nitoe muda wa siku 5 tupate maoni ya wengi. Vote accordingly. Kwa wale ambao hamjajisajili nitahakikisha nanyi mnaweza kupiga kura.

Naomba tutoe statement juu ya hoja hii kabla ya kuanzisha kura ya maoni.

Thanks
 
Please dont close this top admin...tunahita vitu tofauti tofauti hapa JF.Tunasoma kila kit katika JF.Na hii inatufanya tuwe compitent kwenye hoja yoyote unapokuwa mbele za watu na wewe unaweza changia...unaweza changia kwa kutokana na kuwa umesoma moja ya hoja zilizoletwa hapa JF...ukaongeza na mtizamo wako.

Topic moja au thread moja haiwezi fanya forom yote ifugwe....kama kufungwa basi ingefugwa ile ya wakubwa lakini iko pale.

Ni hayo tu.
Buswelu
 
JF imefikia hapa ilipo leo hii kutokana na kuwa na balanced mixture ya kila nyanja ya maisha.Kuna members najua walijoin hapa kwa ajili tu ya hii forum, tusitake JF iwe ni politiki, politiki tu!, it is certainly going to be boring.
 
Ifutwe? HAPANA wengi wanaongia hapa sio kwamba wanapenda Politiki wazee.Wengine hata kuingia kwenye baadhi ya forumn hawaingi wanaingia kwenye forumn wanazozipenda.

Kama kuna mtu anaona haifai kuwepo ni vema sana asiingie hapa.Ebwana masuala haya ni muhimu sana
 
Ifutwe? HAPANA wengi wanaongia hapa sio kwamba wanapenda Politiki wazee.Wengine hata kuingia kwenye baadhi ya forumn hawaingi wanaingia kwenye forumn wanazozipenda.

Kama kuna mtu anaona haifai kuwepo ni vema sana asiingie hapa.Ebwana masuala haya ni muhimu sana

Kama kuna kitu naheshimu ni mawazo ya wadau. Kuna watu wanadai hii forum ifutwe kwakuwa wana watoto wao hutembelea JF ama vipi na hii forum iwe na access maalum kama ilivyo kwa mambo ya kikubwa.

Wadau nahitaji kupata mawazo yenu. Binafsi niliwambia waliopendekeza hivyo kuwa si kila mtu anapenda Siasa ama udaku. Kuna watu wana matatizo kifamilia, kimapenzi na wengine wanatafuta wachumba :). Nikamshauri asitembelee hii link ama awazuie wanae kutembelea ukurasa huu na ikiwezekana awaondolee connection wanae.

Nakosa maamuzi kwakuwa yawezekana mtizamo wangu ni hasi. Tafadhali wadau naomba mawazo yenu juu ya nini kifanyike zaidi. Bado nasisitiza kutotumia maneno yasokuwa na tafsida. Tutambue tuna watoto wabishi wanaopenda kufatilia kila kitu na wao kwao huo ni uvumbuzi. Tuwalee, tutumie maneno yenye heshima na kamwe tusiweke picha za uchi hapa.

Nitafurahi tukijiheshimu.

Invisible
 
Kimsingi watu wanahitaji udhibiti mkubwa. na Mods wengi wanafanya kazi za kujitolea it's not an easy JOB. Wanaotafuta wachumba sawa..ila tuwe so strick...atakaekiuka maadili AFUTWE.

Nimeona baadhi ya Forums za wenzetu very inteesting, wana Ban hata IP, so they dont care....untill 6months wana-release IP. Accounts nyingi ukifanya kosa no msamaha kufungiwa then msamaha after 3months..utashika ADABU..Admin usiwe yule eti kama Yule " MKILA PESA ZA WANANCHI NTAWASEMA HADHARANI" sie hatuna muda. BAN IP, THEN BAN Account, reopen after 3months.
WATU WANAIBA FEDHA YA WANANCHI..then utasema wajirekebishe? Juma moja si adhabu..bora forum iwe na watu wachache ambao wapo serious..huu si UWANJA WA FISI.
 
Hii Forum iache iendelee lakini watu wanaweza kuzungumzia mahusiano, mapenzi na urafiki bila kutumia picha za uchi, matusi ya ndani ya nguo au video za ngono. Mtu akifanya hivyo basi apewe onyo na kufungiwa hilo juma moja na kama akirudia basi afungiwe mwezi mzima.
 
invisible iache iwepo kwa masharti hayo uliyoainisha hapo juu, la kama watu hawafuati hayo masharti ya kulinda heshima ya section hii hapo ndipo utalazimika kuchukua hatua kali.
 
Mimi nilidhani hii ni forum ambayo watu wanaomba ushauri pale ambapo wamefikwa shingoni, sasa mkiifuta itakuwa si haki kwa wengine. Na hao wanaoeka picha za ajabu waende kule kwenye mambo ya wakubwa. Na pia lugha iwe ya tafsida jamani tusiharibu watoto wadogo. kwa ushauri tu kwa wazazi wawawekee mipaka watoto wao, may be it cana help.
 
nnazzani imefahamika, kwa hiyo ataenda kinyume ameamua kujinyonga mwenyewe.

kazi iendeleeeeeeee
 
aiseee isifutwe kwa kuwa nimeshaona kuna watu hukabwa na matatizo hayo shingoni n at the end hupata suluhuisho if not ushauri toka humu humu JF so ibakie kwa kuzingatia masharti uliyoyatoa
 
aiseee isifutwe kwa kuwa nimeshaona kuna watu hukabwa na matatizo hayo shingoni n at the end hupata suluhuisho if not ushauri toka humu humu JF so ibakie kwa kuzingatia masharti uliyoyatoa

Well,

Nashukuru kwa maoni ya wengi. Nahani haina haja ya kuifuta hii forum kwakuwa wengi wanaunga mkono.

LAKINI:
Yale niliyoyaandika hapo awali yataongoza Mods kufanya kazi yao. Nilipoandika "unafungiwa kwa kipindi kisichopungua juma moja" nililenga kumaanisha kuwa inaweza kuwa ni kufungiwa moja kwa moja. I normally ban IP addresses once someone seem to be sturbon. Tatizo la kufungia IP huwa ni pale user anapokuwa kwenye shared IP hasa kwa wenzetu walio Tanzania... Kumfungia mmoja kwaweza kuwaondoa wengi sana.

Ahsante kwa wote waliotoa mapendekezo na maoni yao. Mnaweza kuongeza na tutayazingatia katika maamuzi.

Invisible
 
kwanza nikuombeni radhi nyote ambao mlikuwa mmeandika michango yenu na ikazimika ghafla. Ni kutokana na matatizo ya kiutendaji. Forum hii inahitaji mod mwenye busara kubwa kuwahudumia wanachama wake.

Tuliamua kuiweka offline kwa muda kuangalia uwezekano wa kuirejesha kwa mtizamo chanya ambao tunaamini mtatuelewa na kutilia maanani mapendekezo yetu.

Mapendekezo yetu yako hivi:

1. Kutakuwa na uchelewaji wa kutoa majibu moja kwa moja katika majukwaa (forums) mengi kutokana na uwingi wa michango inayoandikwa kila siku jf. Hivyo uwezekano wa kupata majibu ya haraka toka kwa viranja ama mods kama tulivyozoea kuwaita utakuwa mdogo. Tunaomba wanachama ambao wanajua nafsi zao ziko 'dedicated' katika kuwasaidia wenzao watusaidie kuwajibu na kuhakikisha kila kitu kinaenda salama. Hatutarajii matusi na kashfa kama ilivyotokea kwenye forum ya dini. Heshimianeni.

2. Muhimu sana: Picha za uchi; video za uchi ama ngono hazitaruhusiwa hapa. Ukitaka kufanya mambo kama hayo tafadhali omba ruksa ya kutembelea jukwaa la 'mambo ya kikubwa'. Huendi huko kirahisi bila kuomba kibali maalum na kuidhinishwa. Hatutamvumilia atakayeweka picha za uchi eneo hili ama video za ngono. Atafungiwa kwa muda usiopungua juma moja.

3. Lugha kali za mapenzi ikiwa ni pamoja na zile zisizokuwa na tafsida zitafutwa na mwanachama aliyetoa kauli husika atachukuliwa hatua kali ikiwa ni pamoja na kufungiwa. Sehemu za siri ziitwe hivyo na tusipende kuita koleo kuwa koleo. Ieleweke wazi kuwa hili ni jukwaa huru na wanatembelea watoto. Waonee huruma kuwaharibia maisha. Vinginevyo tutafunga moja kwa moja jukwaa hili kwa kukiuka kipengele hiki. Mtoto wa mwenzio si mkubwa mwenzio; mlee alinufaishe taifa.

Mwisho nawatakia mijadala myema na kuwatakia ufanisi katika kila mfanyalo katika mwaka 2008 na miaka ijayo.

Invisible
for jf management

najikumbusha tu
 
najikumbusha tu

Dena kweli wewe ni mfunyukuzi....umefukunyua uzi huu....kabla sijaona tarehe nilitaka kuzimia....kumbe ni uzi wa 2008....aaahhh......hasa niliposoma hapa.......Naambiwa HII FORUM IFUTWE HARAKA SANA.....na liyesema ni huyu....
avatar72_6.gif
 
Dena kweli wewe ni mfunyukuzi....umefukunyua uzi huu....kabla sijaona tarehe nilitaka kuzimia....kumbe ni uzi wa 2008....aaahhh......hasa niliposoma hapa.......Naambiwa HII FORUM IFUTWE HARAKA SANA.....na liyesema ni huyu....
avatar72_6.gif

Ha ha ha ha umenichekesha..................
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom