AshaDii
Platinum Member
- Apr 16, 2011
- 16,190
- 18,076
Mkuu Zitto you sound really really proud kuwa watokea Kigoma na changes zake pia. Inapendeza. Kwa mara nyingine tena NASHUKURU kwa majibu ya swali lililo pita.
Swali linalofuata;
E. Zitto na Maoni juu ya Tanzania
Swali linalofuata;
E. Zitto na Maoni juu ya Tanzania
- Nini ni Dira ya Kabwe Zuberi Zitto kwa Tanzania?
- Kama leo ungechaguliwa kuwa rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya katiba ya sasa ukiwa amekuta maadui wale watatu (ujinga, umaskini na maradhi) wakineemeka hasa wakiwa wamepata mwenzao ufisadi, ungetumia jeshi gani/mbinu gani kupambana na maadui hawa?
- Kwanini Tanzania ni Maskini? Mkakati gani wa anaouona kuwa unaweza kutambua vipaumbele vya kuondokana na umasikini wa Tanzania?
- Kama kijana, umetembea nchi kadhaa duniani, kwa muono wako ni wapi wananchi, viongozi, serikali na taifa kwa pamoja tunakosea katika kulisongesha gurudumu la maendeleo Tanzania?
- Ikiwa ndani ya uwezo wako i.e tuchukulie umepata urais; ni njia gani ambayo unaweza kutumia kufuta na kumaliza Udini ambao unaanza kujidhihirisha kwenye siasa za Tanzania?