Mahojiano ya Mh. Joseph Mbilnyi aka Sugu na Blog ya Dewji

Lucchese DeCavalcante

JF-Expert Member
Jan 10, 2009
5,471
733
Mheshimiwa Joseph Mbilinyi, Mbunge wa Jimbo la Mbeya Mjini, awali ya yote mimi nikiwa mwakilishi wa Blog ya Mohammed Dewji, Mo blog, ninachukua nafasi hii kukupa pongezi kwa kuaminiwa na wananchi wa jimbo lako, Hongera sana.
MO BLOG : Unawezaje kuizungumzia safari yako ya siasa mpaka hapa ulipofikia katika hatua ya kuwa Mbunge wa Jimbo la Mbeya Mjini?
MH SUGU: Kwanza ninachukua nafasi hii kuwashukuru wapiga kura wa Jimbo langu la Mbeya Mjini kwa kuniamini na kunichagua kwa kura nyingi kama ulivyosikia, lakini pia kazi hii ya uchaguzi kwangu na kwa wananchi wa Mbeya mjini imeandika Historia mpya, ambayo hakuna anayeweza kuivuruga.
Nikushukuru pia kwa kunipongeza kwa hatua hiyo, lakini pili ninaomba kukueleza kwamba hatua hii, sio siasa kwangu, bali ni harakati ya miaka 15 il.iyopita kupitia muziki, ambapo walizungumza na kulalamikia mambo kadhaa kuhusu Taifa yalizungumzwa.
Kimsingi ni kuwa tumeamua kuhamisha jukwaa la madai ya msingi kutoka katika muziki mpaka kwenye siasa, ambayo harakati zake zinaonekana kukubalika na kutekelezwa, na chombo hicho ni Bunge, hivyo jukwaa limehamia rasmi Bungeni.
Awali mambo yale ya muziki yalionekana kuwa ya kihuni tuliyazungumza kwenye majukwaa ya muziki, na waliopaswa kuyatekeleza hawakuchukua hatua kwa kuamini ni kama madai ya wahuni, lakini kwa sasa wajue kwamba mambo hayo ni rasmi katika chombo cha kutunga sheria, kwa maana tutayazungumza na kutaka hatua za kuchukuliwa kulingana na mahitaji ya jamii, kwani kwa pamoja hatukuzungumza mambo ya vijana ni malalamiko na mahitaji ya jamii kuhusu maendeleo.....


Fuatilia mahojiano zaidi kwa kutembea link hiii
 
Uongozi bora ni kusikiliza wapiga kura, na ukiona kiongozi asiye na nafasi ya kupata maelezo ama mawazo ya wapigakura wake, basi huyo ni dikteta, na hatua hiyo kwangu kwa aina hiyo yeyote haitawezekana na nitaendelea kujifunza kutoka kwa watu wengine ndani ya CHADEMA na nje ya chama changu.

Hivi katika wabunge waliotoka bungeni huyu alikuwepo au alikacha move kama Zitto ?
 
MH SUGU: Suala la Maralia kwanza nataka kuweka wazi, na kuhakikisha hilo sio wazi ni kazi iliyokuwa tayari na mimi nimenyang’anywa kazi ikiwa tayari na mikataba yote ikiwa tayari, kwa haki suala hilo bado bichi na halijaisha hata kidogo, na katika suala hili nataka kusimamia usemi wa Rais Jakaya Kikwete kwamba KWENYE VITA VYA HAKI USHINDI NI LAZIMA, na kwa hali hiyo nataka kuonyesha jamii kwamba malalamiko yangu ni ukweli na sitanii hata kidogo.

Na kutokana na hali hiyo, kipimo kwamba ninaweza kufanyakazi kama Mbunge kwa mafanikio na kukidhi kiu ya wananchi walionichagua ni pamoja na kutetea haki zangu binafsi, na hili la MALARIA HAIKUBALIKI, litakuwa miongoni mwa mambo ya msingi.

Nitalifuatilia mpaka kieleweke ili jamii ijue kwamba nilikuwa na lalamikia haki na sio suala la uongo..........hapo kwa red anamzungumzia raisi gani??
 
MH SUGU: Suala la Maralia kwanza nataka kuweka wazi, na kuhakikisha hilo sio wazi ni kazi iliyokuwa tayari na mimi nimenyang'anywa kazi ikiwa tayari na mikataba yote ikiwa tayari, kwa haki suala hilo bado bichi na halijaisha hata kidogo, na katika suala hili nataka kusimamia usemi wa Rais Jakaya Kikwete kwamba KWENYE VITA VYA HAKI USHINDI NI LAZIMA, na kwa hali hiyo nataka kuonyesha jamii kwamba malalamiko yangu ni ukweli na sitanii hata kidogo.

Na kutokana na hali hiyo, kipimo kwamba ninaweza kufanyakazi kama Mbunge kwa mafanikio na kukidhi kiu ya wananchi walionichagua ni pamoja na kutetea haki zangu binafsi, na hili la MALARIA HAIKUBALIKI, litakuwa miongoni mwa mambo ya msingi.

Nitalifuatilia mpaka kieleweke ili jamii ijue kwamba nilikuwa na lalamikia haki na sio suala la uongo..........hapo kwa red anamzungumzia raisi gani??

Yule Rais wa JMT ambaye hamtambui, aliwalk out alipokuwa anatoa hotuba ya ufunguzi wa bunge la 10, ambapo karika bunge hilo Sugu anaingia kama mbunge kwa mara ya kwanza. Kimsingi Sugu anamtambua Kikwete kama Rais, ni shetani tu alimpitia, si unajua tena mambo ya ugenini. Wenzie wenyeji kina Zitto au Shibuda walijua kucheza karata zao.
 
alikuwepo pia!

Kasema

Uongozi bora ni kusikiliza wapiga kura, na ukiona kiongozi asiye na nafasi ya kupata maelezo ama mawazo ya wapigakura wake, basi huyo ni dikteta, na hatua hiyo kwangu kwa aina hiyo yeyote haitawezekana na nitaendelea kujifunza kutoka kwa watu wengine ndani ya CHADEMA na nje ya chama changu.

Alipata ridhaa ya wapiga kura wake kama falsafa yake hapo juu inavyojiuza ? Au ndo longolongo za siasa tu?
 
Hayupo kwenye JF, tulipokuwa Dom juzi niliwashauri baadhi ya wabunge wa CHADEMA akiwemo yeye kujiunga JF, akashangaa kidogo, alidhani JF ni taasisi ya bima kama vile ppf, nikamwelewesha kuwa JF wapo GREAT THINKERS kibao wanatoa challenge nzuri. Nikawapa web.
 
hayupo kwenye jf, tulipokuwa dom juzi niliwashauri baadhi ya wabunge wa chadema akiwemo yeye kujiunga jf, akashangaa kidogo, alidhani jf ni taasisi ya bima kama vile ppf, nikamwelewesha kuwa jf wapo great thinkers kibao wanatoa challenge nzuri. Nikawapa web.

safi sana hope wapo njiani kujunga humu.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom