Wanaachaje kwa mfano? Ila nakuwa na shaka na ukaribu wa Kiangi na huyu Mtoto wa Mahita, katika namna ya kwamba ukaribu wao, je Kiangi hakuingia kwenye ajira ya polisi wakati wa IGP Mahita akiwa madarakani? na je ni vigezo gani vilitumika kumpandisha mpaka cheo alichonacho cha ACP?Kwa Mlolongo wa kesi ya Mbowe na wenzake jinsi ambavyo imeibua hisia za watanzania kua iko siasa na chuki ndani yake, nimelazimika kuuliza maswali haya kwa sababu kadha wa kadha ikiwemo kuwapiga na kuwaumiza walinzi wa Mbowe na wenzinge haijulikani walipo hivi sasa.
Najua kabisa bila shaka kua IGP mstaafu mzee Mahita ni kada kindaki Ndaki wa CCM, ana mtoto wake ni Mbunge viti maalumu CCM na aliwahi kua DC anaitwa Mboni mahita, napateje shaka kua Ispekta Mahita Omari Mahita aliyewateua walinzi wa Mbowe si kada wa CCM?
Ramadhani Kingai kuna siku aliyekua mbunge wa Arusha Godbless alisema wakiwa Arusha aliwahi kumtisha akamwambia kuwe yeye Kingai ni Kada wa CCM, kipindi hicho akiwa RCO Arusha, Kingai huyu huyu si ndiye alimwambia Mbowe hachomoki kwenye kesi yake?
Najaribu kuunganisha dots, huu ni ugaidi wa aina gani? Hakuna chuki za kisiasa kweli hapa? Huu upigaji wa vijana wa watu ambao mpaka sasa kwa mtiririko wa ushaidi wao inaonesha hawajawahi kuvunja sheria yeyote ya nchi, hawakuwahi kutekeleza tukio lolote linalohatarisha amani ya nchi. Walipigwa kiasi walikua wanaenda kumlinda Mbowe?
Unampigaje na kumuimiza mtu hajatekeleza tukio lolote hata kama unamhisi? Hivi ikibainika hawa vijana hawakuwahi kufanya tukio lolote baya,Kingai na wenzake watawalipa nini? Kwanini walitoka nje ya ubinadamu kiasi hicho?