MAHAKAMANI KISUTU: Puto la Boss wa IPTL tumboni limeisha muda wake, linaweza kugeuka sumu

real G

JF-Expert Member
Feb 7, 2013
5,227
5,287
MAHAKAMANI KISUTU: Puto la Boss wa IPTL tumboni limeisha muda wake, linaweza kugeuka sumu

Wakili wa mmiliki wa IPTL, Harbinder Singh Sethi ameieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwa Puto lililopo tumboni mwa Seth limeisha muda wake na asipobadilishwa litamsababishia kifo.

Katika kesi hiyo, mbali na Sethi mshtakiwa mwingine ni James Rugemarila ambao wanakabiliwa na mashtaka 12 ya uhujumu uchumi na kutakatisha fedha.

Hayo yameelezwa na wakili wa Seth, Alex Balomi mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi baada ya Mwendesha Mashtaka wa TAKUKURU, Leornad Swai kueleza upelelezi wa kesi hiyo haujakamilika na wanaomba iahirishwe.

Baada ya kueleza hayo, Wakili Balomi amedai kwa mujibu amri ya Mahakama mteja wake Seth alipelekwa kufanyiwa vipimo Hospitali ya Taifa Muhimbili, lakini hadi leo hajapatiwa majibu ya vipimo wala kupatiwa matibabu.

Amedai kuwa mshtakiwa huyo ana Puto tumboni na limeisha muda wake, hivyo linapaswa kubadilishwa mwishoni mwa mwezi October.

>>>"Kama hilo balloon halitabadilishwa linaweza kugeuka sumu na kuondoa uhai wake, hivyo daktari aliyechukua vipimo anapaswa kumpatia."

Aidha, amedai kuwa wanaomba upelelezi ukamilike kwani upande wa mashtaka unaonekana umezembea sana na watuhumiwa wanateseka jela bila sababu.

Hata hivyo, Wakili Swai amedai kuwa Seth alipelekwa Hospitali October 13, 2017 na alipokea matibabu kutokana na vipimo vya daktari, lakini majibu ni siri ya Daktari na mshtakiwa, sio vya kuongelea Mahakamani.

Kuhusu suala la upelelezi wanaendelea kufanyia kazi.

Baada ya kueleza hayo, Hakimu Shaidi amesema Mahakama ilitoa amri kwamba Seth apelekwe Hospital na amepelekwa, hivyo daktari amekamilisha kazi yake, Mawakili wanaweza kwenda kuulizia kuhusu vipimo vyake akisema upande wa mashtaka ufanye unavyoweza kuhakikisha upelelezi unakamilika na kuahirisha kesi hadi November 10, 2017.

Chanzo: Millard Ayo
 
Wanatengeneza mazingira ya kumtorosha kwa kisingizio cha kwenda kutibiwa nje ya nchi wallahi.
 
STH.jpg


Dar es Salaam. Wakili Alex Balomi ameieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwa mshtakiwa Harbinder Sethi licha ya kupelekwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili na kuchukuliwa vipimo hadi sasa bado hajapa majibu wala matibabu yoyote na afya yake inazidi kudhoofika.

Ameeleza hayo leo Ijumaa mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi mara baada ya Wakili wa Serikali Mwandamizi, Kishenyi Mutalemwa kudai upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika na akaomba ipangiwe tarehe nyingine.

Kishenyi baada ya kueleza hayo, Wakili Balomi alieleza kuwa kwa kiasi fulani upande wa mashtaka umetekeleza amri ya Mahakama kwa kumpeleka Muhimbili na kuchukuliwa vipimo lakini hajapewa majibu na wala hajatibiwa hadi sasa.

Ameeleza kuwa lile puto alilowekewa tumboni Sethi linatakiwa kubadilishwa mwishoni kwa mwezi huu, lisipobadilishwa litageuka kuwa sumu na kuhatarisha uhai wake.

Amesema daktari aliyechukua vipimo ampatie majibu ili aweze kujua hali ya afya yake ikoje.

Wakili Kishenyi baada ya kutolewa kwa maelezo hayo amesema kuwa wao wamekwishatekeleza amri ya mahakama, hawana cha kufanya zaidi kwa sababu majibu ni siri ya magonjwa na daktari.

Mwendesha Mashtaka Mwandamizi wa Takukuru, Leonard Swai yeye naye ameeleza kuwa suala la majibu ni suala la magonjwa na daktari.

Baada ya kutolewa kwa maelezo hayo, Hakimu Shaidi amesema amri ya Mahakama imetekelezwa ambapo mshtakiwa alipelekwa Muhimbili na siyo jukumu la Mahakama kuingilia kazi ya daktari hivyo alishauri mawakili wa upande wa utetezi wafuate utaratibu.

Kesi imeahirishwa hadi Novemba 10, 2017 kwa ajili ya kutajwa na kuusisitiza upelelezi ukamilishwe.


Mwananchi
 
Back
Top Bottom