Mahakama yatupa hoja za serikali; Bunge laachiwa

Sasa hivi CCM wanajua kuwa watu hawawataki, wanasoma magazeti, Jamii Forum na wanajua wakitoa mwanya tu wamekwisha na mwisho wao utakuwa mashakani hivyo tuna kazi ndugu zangu! Ila milango yote ikifungwa ni lazima kutatokea machafuko!!!God forbit.
 
Ajaribu avenues nyingine nje ya Bongo kama vile African court of Justice
 
Omarilyas,
MNkuu shukran sana, tena nashangaa wewe umeyaweka wazi na hukupata rabsha za wanaoogopa vivuli vyao wenyewe.. Hizi habari za mgombea binafsi ni Ujinga mtupu ikiwa hao wagombea wenyewe hawana Itikadi wanayosimamia isipokuwa vichwa vya watu na sijui vision..Hatuwezi kujenga demokrasia kwa kuchagua watu tunaowapenda isipokuwa demokrasia imeundwa kwa misingi ya itikadi.

Mara nyingi kama sio zote nchi zenye wagombea binafsi husimamia aidha Mazingira, dini, au hata reformist kwa nchi zenye vyama viwili vikuu..Na lazima mgombea binafsi asimame kwa ideology na sii mradi twende. As to say, there must be a Political and social phylosophy (ideology) behind which distinguishes from rival ideologies..

Sasa tumtazame mtu kama Mtikila, huyu ni mchungaji sijui anasimamia ideology ipi kama sio Udini au Uzawa..Hakatazwi kuunda chama kinachosimamia maslahi ya dini au Uzawa lakini do we real need this kind of democracy ktk mazingira yetu?.

Je, wale wangine watakao jitokeza watasimamia itikadi zipi ikiwa leo tumeanza na mmoja ktk nchi ambayo kwa zaidi ya miaka 20 tumepigana kuondoa matabaka ya dini na Ukabila, tena basi kwa makosa makubwa kabisa ya muundo wa Demokrasiua tunaifanya haki kuwa ni ya mgombea binafsi ambaye hana itikadi badala ya haki hiyo kuwa ya wananchi kuchagua mgombea anayewakilisha itikadi.
Ama kweli tumevamia demokrasia.
 
Jaji Mkuu ni Brigedia Jenerali Agustine Ramadhani, Rais wa nchi ni Luteni kanali JeyKei , Katibu mkuu wa sisiem ni Luteni Makaamba, katibu mkuu msaidizi ni Kapteni kuuchika, mwezi ni kampeni Chileghati .Sasa hapo unatarajia nini? Na bajeti iliyopita wamepatiwa salary hike!!!!!


Tunataka mabadiliko kwa mdomo tu....never on Earth likatokea hilo!!!!
 
[COLOR="#ffff00"]Tupate hukumu yenyewe kikamilifu; mimi sidhani kama majaji 7 wanaweza kutoa hukumu ya kijinga hivyo. Kuna conflict katika katiba maana upande mmoja inampa ,wananchi haki ya kuchaguliwa na upande mwingine inamnyang'anya haki hiyo kwa kumlazimisha kitu ambacho labda ni kinyume na matakwa yake (kujiunga na vyama vya siasa). Je conflict hiyo wameizungumziaje?[/COLOR]
Je wamesema mahakama kuu haikuwa na uwezo wa kusikiliza kesi inayohusu masuala ya katiba? na kama ni hivyo masuala hayo yapelekwe mahakama gani maana hatuna mahakama ya katiba! Huwezi kusema hayo yapelekwe bungeni maana uamuzi wa wabunge ndiyo ulileta conflict hiyo na hivyo mwananchi yeyote aliyekuwa -aggrived na maamuzi ya bunge hawezi tena kwenda bungeni- bali mahakamani.
Kuna ,mambo mengi yanayohitaji ufafanuzi katika hukumu hiyo.

Kama kweli mahakama imesema suala ni la kisiasa - je kesi ya kisiasa ipelekwe mahakama gani?

Ni hatari sana - watu wamepoteza imani na polisi, wamepoteza imani na mahakama hasa za chini na sasa wakipoteza imani na mahakama ya juu kabisa! itakuwa hatari zaidi ya kile mahakama ya rufaa ilichokiogopa - eti hakuna nchi inaongozwa na mtu huru/binafsi maana ni vizuri mtu binafsi akaingia kwa kupigiwa kura kuliko ukimzibia njia ya kura akaamua kuingia kwa njia ya mtutu! Tusijidanganye eti TZ hiyo haiwezekani, hata enzi za Obote hakuna aliyewazia hilo, enzi za Kenyatta na Moi hakuna akliwazia hilo - lakini yakatokea.!

Ili kuweza kuuweka mjadala huu uwe wa kisomi zaidi nimepost hukumu ya mgombea binafisi katika Jukwaa la Sheria. Nenda kaisome kwanza hukumu halafu ndio tuijadili kama ulivyoomba. Link ni https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...inafsi-hii-hapa-mtikila-vs-ag.html#post956173
 
Wagombea huru hata huko ilikoanzia hii democrasia tunayoiiga ni wachache sana tena kwenye ngazi ya UBUNGE tu. Sisi tunataka kuuparamia utaratibu huu kichwakichwa bila maandalizi yoyote, uelewa wa watu wetu bado mdogo. Mnataka kurudisha masultani, watemi na wafalme kwa mlango huu? Acheni hizo.
Tujipange vizuri kwanza kwenye mambo ya kuchagua na kuchaguliwa. Wagombea huru wabaki kwenye mambo ya uchumba tu kwanza. Hata kugombea uongozi YANGA ni lazima uwe MWANACHAMA!

Mgombea binafsi wa uraisi kwa sasa ni hatari zaidi. Atachunguzwa na nani kabla ya kuruhusiwa kugombea. Utambana vipi na kwa kanununi zipi? Kuna hatari kubwa ya mafisadi kujiunga na kuinunua nchi kwa bei poa na wakiipata hawahitaji zaidi ya kipindi kimoja kusaini mikataba mizito itayotufanya watumwa kwa miaka mingi. Kwa sasa tutaowapata ni vibaraka wa masultani na makabaila wakuu duniani ili wamilikishwe rasilimali zetu kwa kasi ya kutisha. Kama mwamkumbuka 'Jumanne' na kashfa ya OIC haiwi gumu kuelewa hili. Hata Nyerere aliwahi kueleza hofu yake juu ya mgombea binafsi asiye na chama. Ule msemo "Nionyeshe rafiki yako nitakuambia tabia yako" ndo unasaidia kuichambua tabia ya mgombea kwa kuzingatia tabia za chama kinachomfadhili.
 
josey 1979 anaandika:

MAHAKAMA KUU YA TANZANIA, leo imetoa hukumu yake katika kesi ya kikatiba iliyofunguliwa na Mchungaji Mtikila akitaka wagombea Urais binafsi waruhusiwe. Wakitoa hukumu yao leo, jopo la majaji saba likiongozwa na Jaji Mkuu wa Tanzania, Augustina Ramadhani, wamesema kuwa shauri hilo ni la kisiasa zaidi na lilipaswa kujadiliwa Bungeni na kwamba Mahakama haina mamlaka ya kuamua suala hili.Mtikila hakuridhika na uamuzi huo na badala yake amedai atakata rufaa na ataiomba Mahakama izuie Uchaguzi Mkuu ujao hadi hapo shauri lake litakapopatiwa ufumbuzi. Ameahadi kwenda hata Mahakama ya Afrika Mashariki kama ikibidi kufanya hivyo. Shauri hili lilivuta hisia za wanasiasa wengi na hukumu yake ilikuwa ikisubiriwa kwa hamu kwani ni ya kihistoria

je, una uhakika kweli uamuzi huo umetolewa na MAHAKAMA KUU YA TANZANIA?
 
nijuavyo ni mahakama ya rufaa ya tanzania ndiyo iliyosimamia kesi hiyo.

kapongo anaandika, inter alia;
Nilidhani Mahakama ndiyo chombo pekee cha kutoa haki...

hii si kweli. mahakama siyo chombo cha kutoa haki; ni chombo cha kutoa haki kwa mujibu wa sheria. ni kwa sababu hiyo ya "kwa mujibu wa sheria." inawalazimu baadhi ya majaji kutoa hukumu kinyume cha dhamira zao. hivyo tusilaumu sana. jaji ramadhani namfahamu sana anavyotetea kuhusu haki za binadamu na za kiraia. ni sheria tu imechukua mkondo na bahati mbaya mahakamu kuu ya tanzania ndio mahakama ya juu tanzania na maamuzi yake yanafunga (binding) mahakama zote hapa tanzania na maamuzi ya mahakama ya afrika mashariki (kama ipo) haiifungi mahakama ya rufaa ya tanzania isipokuwa tu pale mahakamu kuu ya tanzania itakapoamua kufuata hukumu za mahakama ya afrika mashariki (kama ipo) kwa hiyari yake. tungoje na tuone!
 
Si alishatamka waziri Marmo kwamba hakuna mgombea binafsi. CJ na jopo lake wamepiga mhuri tu amri ya waziri! LONG LIVE TANZANIA AND ITS POLITICS!!!!!!!
Watawala wetu wakumbuke kitu kimoja kuwa hiyo ruling ya kupinga mgombea binafsi inaweza kuwa LEGAL but not LEGITEMATE!! Maana yake ni kwamba watu hawaikubali!!
 
huwa sikosi maneno kirahisi lakini kwa sasa nazuia maneno yote yanayonijia kichwani ili nipate kusoma hiyo hukumu labda mahakama itanishawishi kuona mtiririko wao wa mantiki umekuwaje kwani kusema ni ya "kisiasa" kunanifanya niulize kesi za ubunge kwanini zinapelekwa mahakamani?
 
Wagombea huru hata huko ilikoanzia hii democrasia tunayoiiga ni wachache sana tena kwenye ngazi ya UBUNGE tu. Sisi tunataka kuuparamia utaratibu huu kichwakichwa bila maandalizi yoyote, uelewa wa watu wetu bado mdogo. Mnataka kurudisha masultani, watemi na wafalme kwa mlango huu? Acheni hizo.
Tujipange vizuri kwanza kwenye mambo ya kuchagua na kuchaguliwa. Wagombea huru wabaki kwenye mambo ya uchumba tu kwanza. Hata kugombea uongozi YANGA ni lazima uwe MWANACHAMA!

Unanikumbusha mambo ya CCM. Ukitilia mkazo, watakwambia Siasa na demokrasia imekomaa nchini. Pale ambapo hawataki watasema nchi zetu hizi mambo bado.

Haya unayoyaita ni kuparamia, ni kipi hatuparamii? mbona mishahara ya wabunge tunasema iwe kama 'wenzetu' wa nchi za madola? Leo hii tunatumia windows 7 sawa na mtu wa US na France bila kujali kwamba kuna watu hawajawahi hata kuona chombo kiitwacho kompyuta! Hayo tunaparamia.

Lakini ukisema tume huru, mgombea binafsi, kubadilishwa kwa katiba, nk. hapo tena unaambiwa usiige walioendelea. Dunia hii hatuna muda wa kujifunza polepole. Huu ni wakati wa kupuruzwa, upende usipende utakwenda.
 
Ebu niwaulizeni mnaotaka hii sheria ya mgombea binafsi...
Tuseme mathlan sheria hii ingepitishwa... Na wananchi elfu, laki au millioni uwezo wa kupiga kura wakiamua wao kujiandikisha kama wagombea Binafsi - itakuwaje?..
Maanake sheria mnayoitaka inaruhusu mgombea binafsi na sidhani kama kuna kiwango cha haki kwa idadi ya wagombea wala kukataza wengine wasifanye hivyo..Ni wapi kikomo wa hiyo haki ya mgombea binafsi kwa wananchi wake kwa sababu huwezi sema baadhi ya watu tu ndio wanaruhusiwa wengine wakae pembeni..Je, gharama zake pia zitachukuliwa na nani?..
 
Hivi ninyi mliodhani kwamba mahakama itaruhusu mgombea binafsi mlikuwa mnafikiria nini? Mimi nilijua ingekuwa hivyo kwa sababu ifuatayo:-

  • Aliyetoa uhuru wa kuchagua na kuchaguliwa ni katiba
  • Aliyeminya uhuru wa mgombea binafsi ni katiba ingekuwa sheria it could have been different
Anayetunga sheria na kurekebisha sheria kwa mujibu wa katiba ni Bunge! Mahakama inatumia katiba kutoa haki, haki imetolewa na kuminywa na katiba yenyewe... swali mahakama inge base wapi kutoa huyo mgombea binafsi... please think.

Kila la kheri na mijadala yenu ya hisia zaidi kuliko ukweli.
 
hakuna mahakama nyingine juu yake.. ndio uamuzi wa mwisho.. ila ningependa kupata details na reasoning yao. Inawezekana ameshinda kwenye hoja ya uwezo wa mahakama kutengua kipengele cha Katiba na siyo hoja ya wagombea binafsi au itarudishwa kesi mahakama Kuu.. kupitia tena.
Unajua mwanakijiji, raha ya Tanzania ni kwamba Mahakama ni za serikali, jeshi la serikali, polisi wa serikali, bunge la serikali na hata katiba ni ya serikali. Majaji wote wameteuliwa na Rais, na Kikwete anajua wazi kwamba akisimama mgombea binafsi tu amekwisha. Unafikiri angekubali huo upuuzi wa mgombea binafsi? Atakuwa amewaagiza tu akina Augustino Ramadhani na washirika wake kwamba hii kesi iishie hapa.
 
Ebu niwaulizeni mnaotaka hii sheria ya mgombea binafsi...
Tuseme mathlan sheria hii ingepitishwa... Na wananchi elfu, laki au millioni uwezo wa kupiga kura wakiamua wao kujiandikisha kama wagombea Binafsi - itakuwaje?..
Maanake sheria mnayoitaka inaruhusu mgombea binafsi na sidhani kama kuna kiwango cha haki kwa idadi ya wagombea wala kukataza wengine wasifanye hivyo..Ni wapi kikomo wa hiyo haki ya mgombea binafsi kwa wananchi wake kwa sababu huwezi sema baadhi ya watu tu ndio wanaruhusiwa wengine wakae pembeni..Je, gharama zake pia zitachukuliwa na nani?..

Kama sheria ingepitishwa, taratibu za ugombeaji pia zingepitishwa. Mbona CCM huwa wanagombea watu hata 10 au ishirini halafu baadaye wanachujwa? Hata katika hili kungewekwa utaratibu wa kuwachuja hadi kubaki labda mgombea binafsi mmoja atakayecompete na wagombea wa vyama nk.
 
Mzee Mwanakijiji,

Sijaisoma hukumu wala kuipata lakini kwa vyovyote vile issue itakuwa mahakama haiwezi kutengua kifungu cha katiba, bali inaweza kutengua sheria ambayo haiendani na katiba.
 
Mzee Mwanakijiji,

Sijaisoma hukumu wala kuipata lakini kwa vyovyote vile issue itakuwa mahakama haiwezi kutengua kifungu cha katiba, bali inaweza kutengua sheria ambayo haiendani na katiba.

ndio maana nareserve comment hadi nijue mtiririko wao wa hoja uko vipi lakini kama ni kuwa ni suala la "kisiasa" basi kuna upuuzi wa hali ya juu katika fikra. Natumaini tutapata hiyo hukumu muda si mrefu.
 
Unajua mwanakijiji, raha ya Tanzania ni kwamba Mahakama ni za serikali, jeshi la serikali, polisi wa serikali, bunge la serikali na hata katiba ni ya serikali. Majaji wote wameteuliwa na Rais, na Kikwete anajua wazi kwamba akisimama mgombea binafsi tu amekwisha. Unafikiri angekubali huo upuuzi wa mgombea binafsi? Atakuwa amewaagiza tu akina Augustino Ramadhani na washirika wake kwamba hii kesi iishie hapa.

Sidhani

Mix with yours
 
Mgombea binafsi wa uraisi kwa sasa ni hatari zaidi. Atachunguzwa na nani kabla ya kuruhusiwa kugombea. Utambana vipi na kwa kanununi zipi? Kuna hatari kubwa ya mafisadi kujiunga na kuinunua nchi kwa bei poa na wakiipata hawahitaji zaidi ya kipindi kimoja kusaini mikataba mizito itayotufanya watumwa kwa miaka mingi. Kwa sasa tutaowapata ni vibaraka wa masultani na makabaila wakuu duniani ili wamilikishwe rasilimali zetu kwa kasi ya kutisha. Kama mwamkumbuka 'Jumanne' na kashfa ya OIC haiwi gumu kuelewa hili. Hata Nyerere aliwahi kueleza hofu yake juu ya mgombea binafsi asiye na chama. Ule msemo "Nionyeshe rafiki yako nitakuambia tabia yako" ndo unasaidia kuichambua tabia ya mgombea kwa kuzingatia tabia za chama kinachomfadhili.

Mafisadi waliopo sasa wametokana na kugombea binafsi? yes tunawajua mpaka marafiki zao na la kufawanya hatuna!!!! tusijiingize hofu zisizo na sababu wakati hata sasa uuzaji wa nchi kwa manyang'au unafanywa na watu walio katika vyama....si busara kuwa na negative attitude kiasi hiki.
Mix with yours
 
Back
Top Bottom