Mpemba Mimi
JF-Expert Member
- Jul 6, 2013
- 1,449
- 2,059
Pale kwake Kigamboni hayuko kweli?? Sidhani kama huyu jamaa katoweka, wakati ana nyumba yake pale Kigamboni...
Uwe na uso wa AIBUMachadema cjui yakoje yanapenda chuki sana!!!
kesi itafutwa.Siku ya kesi ni 2/3/2022 maswali yako yote yatajibiwa
Kwa kuwa ANATUMIA KINGA ya Mwendazake KESI ITAFUTWAkesi itafutwa.
hakuna cha maana hapo.
nani kakwambia kuna kesi hapo?Kwa kuwa ANATUMIA KINGA ya Mwendazake KESI ITAFUTWA
Sent from my SM-J600F using JamiiForums mobile app
Fingerprints nazo amefoji?Labda hajapitia kwenye vituo vya immigration. Au yupo nchini kizuzini.Au atajitokeza pale atakapobanwa na mkono wa sheria.
Watamtangaza kwa jina lipi! Daud Bashite au Paul Makonda na kama kesi ni ya Paul Makonda haendi mahakamani kwa sababu jina si lake, na kama Daud Bashite haendi mahakamani kwa sababu jina si lake.Mahakama ya Kinondoni leo Jumanne imetoa amri ya kutangazwa gazetini, nyumba aliyoishi Masaki na au kijijini kwao Kolomije kwa aliyekuwa mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda ili apate taarifa za kesi iliyofunguliwa dhidi yake na Mwandishi wa Habari, Saed Kubenea. Kesi itatajwa 2 Machi 2022.
Pia soma > Paul Makonda ashindwa kufika Mahakamani katika kesi inayomkabili. Kesi yaahirishwa hadi 08 Feb 2022
Shauri hilo limetajwa kufuatia Mahakama hiyo kushindwa kusikiliza hapo awali baada ya shughuli kuingiliana.
----
Akizungumza mahakamani hapo Leo Wakili wa upande wa waleta maombi Nyaronyo Kicheere, ameeleza kwamba wameshindwa kumpata mjibu maombi namba 3 ambaye ni Paul Christian Makonda kwa kuwa Masaki alikokuwa anakaa amekwishahama na namba yake ya simu haipatikani na hivyo kuiomba Mahakama hiyo iwapatie hati ya kumsaka maeneo mbalimbali.
Aidha wameomba kupewa hati za wito ambazo zitapelekwa alipokuwa akifanyia kazi kwa mara ya mwisho, kwenye nyumba aliyokuwa anaishi kwa mara ya mwisho, maeneo anayotembelea mara kwa mara na nyingine iwekwe katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, nyingine ipelekwe bandarini, Kolomije, Misungwi mkoani Mwanza na ya mwisho ipelekwe kwenye gazeti la Kiswahili na la kingereza.
Wakili ameongeza kuwa lengo la kufanya hivyo ni kutaka mjibu maombi hayo ambaye ni Paul Makonda apate taarifa juu ya uwepo wa kesi hiyo mahakamani.
Kwa upande wake Hakimu wa mahakama hiyo Aron Ryamuya, ameeleza kuwa hoja ya kwenda kubandika hati hizo katika viwanja vya ndege na bandarini ni kinyume cha sheria na ni uchafuzi wa mazingira na badala yake akakubali matangazo hayo yapelekwe kwenye nyumba yake ya Masaki aliyokuwa akiishi, kwenye gazeti na kijijini kwao Koromije pekee.
Kesi hiyo namba 1 ya mwaka 2022, imeahirishwa hadi Jumatatu ya Machi 2, 2022.
Chanzo: EATV
Wewe unprejudiced ndiyo inahitaji tiba kwa kuona kuwa ilikuwa kitu cha kawaida kwa Makonda kufanya aliyoyafanya na Mkuu wa Nchi akaona sawa tu.JPM kawazidi sana. Kafa Lakini mnateseka sana kama ma x. JPM alikuwa Rais sio mchungaji au yesu au mtume. Kama kumbukumbu yangu iko Sawa. Makonda aliibuliwa bunge la Katiba. ( Sijui JPM alihusika)...
Bashite hawezi pumua kaamuza wengi hata kubenea akishindwa watainuka wengineNa lazima atatokea shujaa mwingine kama Kubenea wa kutaka kujua uchunguzi uliishia wapi.
kuhusu mataga mwenzangu sabaya alizingua mwenyewe, alimdharau saa 100, comrade Bashite yeye ni rafiki wa Mama, Sabaya tungekuwa naye leo tunakula pesa za chama lakini yeye kiburi kilimponza, lakini hata hivo bado analindwa si unaona mali zake mpaka leo hazijauzwa wala kutaifishwaangekua above the law mahakama isingetoa hati hiyo ,ujue asipoudhuria tena mahakamni itaonekana ameidharau mahakama na mahakama itatoa warrant of arrest.
Mlikuwa mnamdanganya hivyohivyo mfungwa sabaya
mtakuja kukimbia post zenu hapo baade