Mahakama yatoa Amri Askofu Mokiwa na Wenzake wakamatwe kwa kutotii mahakama!

Naomba kujua anapoabudu mheshimiwa judge!

Utamwonea Judge bure. Niliwahi kuongea na Jaji mmoja amaye kwa sasa ni mwenyeki wa baraza la maadili Tanzania . Baada ya Maongezi ya Muda mrefu na kutaka kujua jinsi mahakama za Tanzania zinavyotoa haki. Mmoja wetu akataka kujua kama wanasiasa hasa ikulu inahusika na kutoa haki mahamani. Alikataa sana, ila alipobanwa na kupewa baadhi ya facts mojawapo ikiwa kesi ya marehemu Ukiwaona. Alikubali kuwa ikulu huwa inaingilia hukumu na kutoa maelekezo nini kifanyike kwa mtuhumiwa au kesi husika.

Ila alisema kuna baadhi ya Majaji shupavu hukataa, ila sio wengi kwani ajira iko mikononi mwa Raisi.
 
Mkuu hao waumini wametumwa na Dr Mbena, ukiwaangalia wanatia huruma maana hata wengine hawana uhakika wa mlo wa jioni, kwa jeuri yao hata kesi ya wizi wa kuku hawawezipeleka mahakamani. Ni wachovu vibaya. Si akina manundu na Mhone? Wengine kuishi kwao hadi wategemee wake zao wawatoe

Hayo sasa ni matusi ambayo yanashusha hadhi ya mchango wako. Sema wewe ujuavyo hii issue ni kweli hotay kachakachua umri? Lakini kama kanisa lina katiba na waumini wameisoma wakaielewa hususan ambao walihusika moja kwa moja kwenye mchakato wa uchaguzi, basi kama kuna taratibu zimekiukwa mwenye kufanya tafsiri sahihi ni mahakama. Nina ushahidi kuwa baada ya uaskofu wa Marehemu Alpha Mohamed Dayosisi ya Mlima Kilimanjaro ina maaskofu wafanyi biashara hata za Condom. Hapo ndipo mgongano unapoanzia. Sema kweli kama huyo Hotay si mfanyabiashara? Nakusihii naona una dalili na dhamiri njema na kanisa watumishi wa hii Dayosisi waache unafiki waiheshimu Liturgia ya Kanisa Anglikana na Biblia mizozo itaisha.
 
Sielewi kwanini hadi sasa hajakamatwa na kufikishwa mahakamani; au yuko juu ya sheria? Mokiwa akamatwe mara moja haiwezekani tangu itolewe amri hakuna kiongozi wa Polisi aliyejitokeza kwenda kumtia pingu huku akiwaambia wapi yupo.
 
  • Thanks
Reactions: FJM
Sielewi kwanini hadi sasa hajakamatwa na kufikishwa mahakamani; au yuko juu ya sheria? Mokiwa akamatwe mara moja haiwezekani tangu itolewe amri hakuna kiongozi wa Polisi aliyejitokeza kwenda kumtia pingu huku akiwaambia wapi yupo.

Mzee wa kijijini polisi wamesema amri imetoka maneno na hakuna ushahidi wa amri yaani arresting Warrant so hawawezi mkamata ila sijui kama Mbowe ilitolewa au ilikuwa maneno lakini wakafanya kweli
 
Mahakama ilitoa amri ya kusimikwa kwa Askofu wa Dayosisi ya Kilimanjaro, alichofanya Askofu Mokiwa na wenzake ni kumsimika Askofu wa Kanisa la Anglikana Tanzania lakini hajasimikwa kuwa Askofu wa Dayosisi ya Kilimanjaro!! Kesi ikiisha kama atashinda basi atasimikwa kuwa Askofu wa Anglikana Dayosisi ya Kilimanjaro. Kwa sasa anabaki kuwa na cheo cha uaskofu bila kuwa na Dayaosisi kama vile kina Askofu Donald Mtetemela, Askofu John Ramadhani n.k.

Mahakama itaamrishaje mtu asimikwe kuwa askofu wa Dayosis? Kwa mamlaka ipi! Hii inatisha sasa.

Amandla......
 
Sakata la Askofu Mokiwa gumu kwa mahakama Send to a friend
Mwananchi: Friday, 17 June 2011 21:15
0diggsdigg

Mussa Juma, Arusha
SAKATA la kukamatwa kwa Askofu Mkuu wa Kanisa la Anglikana Tanzania, Dk Valentino Mokiwa na Askofu Stanley Hotay kutokana na uamuzi wa Jaji wa Mahakama Kuu, Kakusulo Sambo, linaonekana kuwa gumu kwa mahakama kutokana na kushindwa kutoa hati ya kukamatwa kwa askofu huyo.

Msajili wa Mahakama kuu Arusha, George Herbet, jana aliahidi angetoa maelezo juu ya kushindwa kutolewa kwa hati hiyo, lakini hata hivyo, hakupatikana ofisini na katibu muhtasi wake alisema alikuwa kwenye kikao kwa mkuu wa Mkoa wa Arusha.

"Msajili katoka Ofisini na kaenda kwenye kikao,"alisema Katibu Muhutasi huyo.Katibu huyo pia alisema hajaona hati hiyo na alishauri suala hilo kama lipo ni vyema kufuatiliwa kwa makarahani wa Mahakama Kuu, waliopo jirani na ofisi hiyo, ambao nao walieleza kuwa suala la hati hiyo msemaji mkuu ni Msajili Herbet.

Lakini baada ya msajili huyo kupigiwa simu yake ya mkononi mara kadhaa, hakupokea na haikujulikana mara moja kikao baina yake na Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Isdore Shirima kilihusu nini.

Jaji Sambo alitoa maamuzi ya kukamatwa kwa maaskofu hao kwa tuhuma za kudharau amri ya mahakama kuu, ambayo iliagiza kanisa hilo, kutomsimika Hotay kuwa askofu jumapili iliyopita kutokana na waumini watatu wa kanisa hilo kufungua kesi kupinga ushindi wake katika mchatakato wa kumpata Askofu wa kanisa hilo, Dayosisi ya Mount Kilimanjaro.

Askofu Mokiwa alieleza katika hafla hiyo, ambayo ilihudhuria na vigogo kdhaa wa mkoa wa Arusha, akiwepo mkuu wa mkoa Shirima kuwa, Askofu Hotay amesimikwa kama Askofu wa kanisa la Anglikana Tanzania na sio wa Dayosisi ya Mount Kilimanjaro na hivyo hawajavunja sheria.

Maaskofu hao, wameeleza wapo tayari kukamatwa kwani wanaamini hawajavunja sheria, katika kesi ya awali, maaskofu wa kanisa hilo, akiwepo Mokiwa ni washitakiwa wa kwanza na mshitakiwa wa pili alikuwa ni Hotay.

Hata hivyo, Katika maamuzi ya Jaji Sambo, alisema haikuhitaji elimu ya shahada kubaini kuwa maaskofu hao wamevunja amri ya mahakama kwani, kesi iliyopo Mahakamani ni kupinga Askofu Hotay asiapishwe kuwa Askofu kutokana na kudaiwa umri wake haijafikia na hivyo taratibu za awali zilikiukwa.

Kamanda wa polisi mkoani Arusha, Akili Mpwapwa, alisema kuwa bado walikuwa hawajapata hati ya kumkamata Askofu Mokiwa na Hotay na kama wakipata jeshi hilo halina kipingamizi cha kuwakamata

My Take: Kumbe na RC alishiriki hafla ya kuidharau mahakama!!!!!!!
 
Sielewi kwanini hadi sasa hajakamatwa na kufikishwa mahakamani; au yuko juu ya sheria? Mokiwa akamatwe mara moja haiwezekani tangu itolewe amri hakuna kiongozi wa Polisi aliyejitokeza kwenda kumtia pingu huku akiwaambia wapi yupo.

Mzee nasikia polisi ina warrant yako, dege la jeshi linakutafuta. Lol! hakamatwi mtu, wamekurupuka. Wanajua wakimkamata anaweza kusema watu wakimwona mkulu wapige yowe. Kama masaa 48 yaliwatia kiwewe tukalitewa majina ya kinigeria usidhani masihara. Dr. Mokiwa haombi kibali cha polisi kuhutubia.
 
Kuna mambo mengine wanasheria wetu wanonyesha kiwango chao cha elimu ni feki au ni kile cha kudesa tu. Hivi mtu kaenda shule kalipa ada yake kamaliza leo anatokea mtu mwingine kupinga mahakamani eti muzuieni asifanye mahafali. Ktk hali ya kawaida hili haliwezekani. Ni common sense. Mahakama inauwezo wa kumuzuia kufanya kazi endapo tu kama kuna la maana. lakini graduation ni haki. Uaskofu ni daraja kama watu wanavyopata degree ambayo mtu ameisotea darasani sasa mtu unakuja from no where eti hakuna graduation. ulikuwa wapi miaka yote hiyo jamaa anasomea? Mokiwa amewapa ukweli ile ni graduation na sio sherehe za mtu kuajiriwa na kupewa jimbo hivi huyu mwanasheria akili ipo kweli?namshauri aende shule tena.

Wanasheria wetu achaneni kutumiwa na watawala kufanikisha mambo yao. Kwani humukumbuki viapo vyenu kuwa mtatenda haki kwa mujibu wa sheria au mnatenda haki kwa mujibu wa maagizo. Hii dunia tunapita tu.
 
Mkuu umesema kweli, ukristo tatizo kwa serikali hii. Fuatilia sasa kuna maendeleo mengi sana na tena hawajifichi ziko habari nyingi tu zimetapakaa na zinaendelea kutapakaa juu ya juhudi hiyo.

Tunakotaka kwenda si kuzuri. jitazameni wenye mpango huo muache

Sheria ni msumeno, inakata huku na huku.
 
Sielewi kwanini hadi sasa hajakamatwa na kufikishwa mahakamani; au yuko juu ya sheria? Mokiwa akamatwe mara moja haiwezekani tangu itolewe amri hakuna kiongozi wa Polisi aliyejitokeza kwenda kumtia pingu huku akiwaambia wapi yupo.
Sababu zinatosheleza kukamatwa kwake??
 
Back
Top Bottom