Mahakama yaruhusu Ukahaba, yasema makahaba wanayo haki ya kulindwa na katiba

moshingi

JF-Expert Member
Nov 15, 2011
278
92
Mahakama katika mji wa Toronto nchini Canada imetoa hukumu ya kihistoria ambayo huenda
ikazusha mjadala mkubwa kuhusiana na biashara kongwe kuliko zote duniani, "biashara ya ukahaba".
Hukumu hiyo imetolewa baada ya makahaba kuifungulia kesi serikali ya nchi hiyo wakitaka biashara
yao ihalalishwe na kuzuia ubaguzi dhidi yao. Mahakama katika hukumu yake imesema kuwa makahaba
wanastahili kupata ulinzi kikatiba, hawastahili kubaguliwa, na kwamba biashara yao ni halali-wanastahili
ulinzi toka serikalini na kwamba wanapaswa kulipa kodi kama wafanyabiashara wengine.Hata hivyo serikali
imepewa muda wa kukata rufaa kabla ya utekelezaji wa hukumu hiyo. Hukumu hii imekuja wakati ambapo
mkuu wa kanisa katoliki duniani Pope Benedict wa XVi akiendelea na ziara yake huko America. Kanisa hilo
limekuwa mstari wa mbele kuipinga biashara hiyo. (Source-Aljazeera). Je ndiyo tuseme ule upepo wa kuruhusu
vitendo vya ukahaba na ushoga umeanza kuvuma?
 
Ni heri BABA MTAKATIFU BENEDIKTI WA XVI umejiuzulu ili mambo haya yanapoendelea kutokea duniani
usilaumiwe....
 
Ni heri BABA MTAKATIFU BENEDIKTI WA XVI umejiuzulu ili mambo haya yanapoendelea kutokea duniani
usilaumiwe....

Kwaiyo katika ushoga utamlaumu? Maana yeye alikuwa papa...... Mambo mengine fikirieni kabla hamjaropokwa
 
Kwaiyo katika ushoga utamlaumu? Maana yeye alikuwa papa...... Mambo mengine fikirieni kabla hamjaropokwa

Mkuu kati yangu mimi na wewe nani ameropoka??? soma habari yenyewe, nilieleza kuwa kanisa katoliki limekuwa mstari wa mbele kuipinga biashara hiyo...ilikuwa wakati akifanya ziara yake huko America...ni baada ya mambo mengi kutokea
ambayo kwayo wapo watu wamemlaumu kama vile vitendo vya unyanyasaji watoto vilivyotendwa na baadhi ya watawa
kuvuja siri za kanisa baada ya muhudumu kumsaliti...ndiyo maana nikasema asije kulaumiwa pia kwa hili la ukahaba
kuwa na fikra pevu MKUU usikurupuke kutukana hovyo ipo siku utamtukana mkweo!!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom