Mukulu wa Bakulu
JF-Expert Member
- Aug 12, 2014
- 4,052
- 12,906
Shilole aangua kilio baada ya mahakama kutoa hukumu kumtaka alipe million 14 za kitanzania kwa Mary Musa.
Mwaka 2017 katika mkesha wa Pasaka Shilole alilipwa mil.3 akatumbuize huko Mbagala lakini alishindwa kutokea kwa wakati hivyo mashabiki kupandwa na hasira na kuharibu Mali ukumbini Hapo.
Mary alifungua kesi kuomba alipwe fidia lakini Shilole akawa anapuuza wito wa mahakama.
Shilole ametakiwa kutoa pesa hizo ndani ya wiki moja la sivyo Mali zake zitashikiliwa.
Crediti: GPL
------------
Safi sana Mahakama, ni wakati sasa wa wanasanaa wetu kujua umuhimu wa kuheshimu sheria na kuheshimu mikataba.