Petro E. Mselewa
JF-Expert Member
- Dec 27, 2012
- 10,195
- 25,513
Mahakama Kuu ya Tanzania iliyokuwa chini ya jopo la Majaji watatu (Profesa John Ruhangisa,Winfrida Korosso na Lugano Mwandambo) imemwondolea Mkurugenzi wa Mashtaka nchini mamlaka ya kutoa adhabu isiyokatiwa rufaa kwa mshtakiwa anayekiri makosa ya kimtandao.
Kutokana na uamuzi huo uliobatilisha kifungu cha 50 cha Sheria ya Makosa ya Mtandao, Mahakama imeipa Serikali miezi 12 kukifanyia marekebisho kifungu hicho. Hatahivyo, Mahakama Kuu ya Tanzania imehalalisha vifungu vingine vyote vya Sheria hiyo ambavyo pia vimekuwa vikilalamikiwa na wadau wa matumizi ya mitandao na teknolojia ya habari.
Uamuzi huo wa Mahakama Kuu ya Tanzania umetolewa kwenye kesi ya kikatiba nambari 32 ya 2015 iliyofunguliwa na Wakili wa Kujitegemea Jebra Kambole. Wakili Msomi Kambole alikuwa akipinga vifungu vya 4,5,6,7,8,9,10,11,14,19,21,22,31,33,34,35,37,38 na 50 vilivuodaiwa kukiuka haki ya mtu kuwasiliana na haki ya mtu kusikilizwa zinazotolewa na Katiba ya nchi. Shauri hilo lilikuwa dhidi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali.
Chanzo: Mwananchi la leo, uk. 1 &3.
JAMII LEO
======
Dar es Salaam. Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) ameondolewa mamlaka ya kutoa adhabu isiyokatiwa rufaa kwa mshtakiwa anayekiri makosa ya kimtandao.
Uamuzi huo umetolewa na Mahakama Kuu,umeipa Serikali miezi 12 kukifanyia marekebisho kifungu cha 50 cha Sheria ya Makosa ya Mtandao kilichobatilishwa.
Hata hivyo, mahakama hiyo imehalalisha vifungu vingine vyote vya sheria hiyo, ambavyo pia vimekuwa vikilalamikiwa na wadau wa matumizi ya mitandao na teknolojia ya habari.
Uamuzi huo umetokana na kesi ya kikatiba, iliyofunguliwa na Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu (THRDC), Kituo cha Msaada wa Sheria na Haki za Binadamu (LHRC)na mashirika mengine.
Katika hukumu iliyotolewa na majaji Profesa John Ruhangisa, Winfrida Korosso na Lugano Mwandambo, Mahakama ilibatilisha Kifungu cha 50 cha sheria hiyo, lakini ikaridhia vingine kuwa ni halali.
Chanzo: Mwananchi
Kutokana na uamuzi huo uliobatilisha kifungu cha 50 cha Sheria ya Makosa ya Mtandao, Mahakama imeipa Serikali miezi 12 kukifanyia marekebisho kifungu hicho. Hatahivyo, Mahakama Kuu ya Tanzania imehalalisha vifungu vingine vyote vya Sheria hiyo ambavyo pia vimekuwa vikilalamikiwa na wadau wa matumizi ya mitandao na teknolojia ya habari.
Uamuzi huo wa Mahakama Kuu ya Tanzania umetolewa kwenye kesi ya kikatiba nambari 32 ya 2015 iliyofunguliwa na Wakili wa Kujitegemea Jebra Kambole. Wakili Msomi Kambole alikuwa akipinga vifungu vya 4,5,6,7,8,9,10,11,14,19,21,22,31,33,34,35,37,38 na 50 vilivuodaiwa kukiuka haki ya mtu kuwasiliana na haki ya mtu kusikilizwa zinazotolewa na Katiba ya nchi. Shauri hilo lilikuwa dhidi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali.
Chanzo: Mwananchi la leo, uk. 1 &3.
JAMII LEO
======
Dar es Salaam. Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) ameondolewa mamlaka ya kutoa adhabu isiyokatiwa rufaa kwa mshtakiwa anayekiri makosa ya kimtandao.
Uamuzi huo umetolewa na Mahakama Kuu,umeipa Serikali miezi 12 kukifanyia marekebisho kifungu cha 50 cha Sheria ya Makosa ya Mtandao kilichobatilishwa.
Hata hivyo, mahakama hiyo imehalalisha vifungu vingine vyote vya sheria hiyo, ambavyo pia vimekuwa vikilalamikiwa na wadau wa matumizi ya mitandao na teknolojia ya habari.
Uamuzi huo umetokana na kesi ya kikatiba, iliyofunguliwa na Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu (THRDC), Kituo cha Msaada wa Sheria na Haki za Binadamu (LHRC)na mashirika mengine.
Katika hukumu iliyotolewa na majaji Profesa John Ruhangisa, Winfrida Korosso na Lugano Mwandambo, Mahakama ilibatilisha Kifungu cha 50 cha sheria hiyo, lakini ikaridhia vingine kuwa ni halali.
Chanzo: Mwananchi