Mahakama yaamuru balozi wa zamani Italia kujiibu mashtaka ya ufisadi

Semanao

JF-Expert Member
Jul 25, 2007
208
16

Na Tausi Ally

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam, imetupilia mbali ombi la upande wa utetezi katika kesi ya uhujumu uchumi inayomkabili aliyekuwa Balozi wa Tanzania nchini Italia, Profesa Costa Ricky Mahalu na mwenzake la kutaka kesi hiyo ifutwe, badala yake imepanga ianze kusikilizwa Januari 28, mwaka huu .


Hakimu Mkazi Mkuu Mfawidhi wa mahakama hiyo, Sivangilwa Mwangesi alisema jana kuwa hoja zilizotolewa na upande wa utetezi kutaka kesi hiyo ifutwe haina msingi.


Alisema sheria hailazimishi maelezo ya mlalamikaji kuonyesha kosa kama ulivyodai upande wa utetezi bali kosa huonekana wakati wa upelelezi.


Awali wakili Cathbert Tenga anayemtetea Mahalu na mwenzake aliiomba mahakama ifute hati ya mashitaka akidai kuaw ni ya bandia kwa madai kuwa maelezo ya mlalamikaji yaliyowasilishwa mahakamani hapo haionyeshi kosa.


Alidai maelezo ya mlalamikaji ndiyo msingi wa kuandaa makosa ya kumpeleka mtu mahakamani na yaliyopo mahakamani hayaonyeshi kosa hivyo hati iliyopo mahakamani ni feki.


Hoja ya wakili huyo iliungwa mkono na wakili mwnzake Alex Mgongolwa anayewatetea washitakiwa hao ambaye alisisitiza kuwa ni lazima hati ya mashitaka iandaliwe kwa kutumia maelezo ya malalamikaji.


Mgongolwa alidai kuwa mlalamikaji August Chami anadai kuwa Agosti 3, 2004 akisikiliza redio, alisikia Naibu Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje na Ushirikiano wa Kimataifa akieleza Bungeni kuwa, taarifa ya Mkaguzi Mkuu wa Mahesabu ya Serikali (CAG) inaonyesha kwamba alipoenda kukagua ubalozi wetu wa Rome Italia hakukuta hati yoyote inayohusiana na ununuzi wa jengo lililonunuliwa na wizara hiyo.


Alidai kuwa baada ya Chami kusikia mjadala huo alimwandikia kiongozi wake(RCB) na kumweleza wasiwasi wake juu ya kutoonekana kwa hati hizo ndio sababu akafanya uchunguzi.


Pia Mgongolwa aliiomba Mahakama iangalie ripoti ya maswali na majibu ya majadiliano ya kikao cha 39 cha Agosti 3, 2004 cha Bunge kilichoanza saa tatu asubuhi mbele ya aliyekuwa Spika wa Bunge Pius Msekwa ili ijilidhishe.


Washtakiwa hao wanadaiwa kuhujumu uchumi kwa kuisababishia hasara serikali ya Euro 2,065,827.60 wakati wakiwa maofisa wa ubalozi wa Tanzania nchini Itali na keshi hiyo ilifunguliwa mwaka jana.
 
Kama Mahalu hana kosa si wasubiri awe exonerated na mahakama. Kilicho feki ni risiti alizotoa kama vielelezo vya kunua jengo la ofisi.

Mahalau angekuwa muungwana aamue aibe tu pesa za serikali na akamwacha mke wa staff mwenziwe haya yoote yasingemfika.

Fisadi, fisadi tu, hata mkewe mfanyakazi wa chini yake hakatizi.
 
Kama Mahalu hana kosa si wasubiri awe exonerated na mahakama. Kilicho feki ni risiti alizotoa kama vielelezo vya kunua jengo la ofisi.

Mahalau angekuwa muungwana aamue aibe tu pesa za serikali na akamwacha mke wa staff mwenziwe haya yoote yasingemfika.

Fisadi, fisadi tu, hata mkewe mfanyakazi wa chini yake hakatizi.

Ebo! ina maana chanzo cha hii skendo ni hiyo ishu?????
 
Ebo! ina maana chanzo cha hii skendo ni hiyo ishu?????

Mwe mwe, gwe nyambala, utifiki malafyale.

With all due respect kwa mafisadi, huwa wanajisahau na hasa wakishanogewa. Aliye lipua bomu ni mume wa mama aliyekuwa mhasibu ubalozini Italy ambaye huyu ngosha Mahalu aliaamua kumkandamiza kisukuma huyu bibie wakati huhuo akimtumia kumuvuzisha ma millioni ya euros kwenda offshore account na baadaye kuchonga risiti kibongo. Basi mwanamume baada ya kumkabili mama ikabidi mama atubu na kukubali kuwa shahidi.
 
Ina maana bila hivyo tungekuwa tumeshaliwa?????? Kazi kweli kweli!!!!!
 
Na Haki Itendeke Kwa Kuwa Watu Walishaanza Kuzusha Hapa Na Hukumu Wametoa Kuwa Wana Ushahidi Wa Kinachoendelea Kuwa Ni Mchezo Mchafu.na Mahakama Iachwe Ifanye Kazi Yake
 
Profesa wa sheria anaenda kuchonga receipts? Kweli ukiwa fisadi inafika mahali unaona kama kila kitu mali yako.

Jamaa alivyokuwa mlimani, alikuwa anajifanya dini ile mbaya, kumbe anazengea wake za wenzake?
 
Mimi yangu macho sina la kusema kwa sasa ila bidii kufuatilia kesi hii na mwenendo wake .Itaishia kweli ?
 
Na swali..members wengi humu wamekuwa wakisema HELA ZETU zinaibiwa serikalini...nauliza lini hizi hela zilikuwa zetu? Hivi nani kati yetu anaweza kwenda mtaani na kumweleza muuza karanga kwamba hela zake zimeibiwa BOT au kwengine kokote?? This government has not been known to empower anyone but itself?? Ndo maana hadi leo hii tunategemea misaada..juzijuzi nimeona govt spokesperson wa Kenya akisema foreign countries are there as partners nothing more and shud not mix themselves in kenyan affairs...wakati sisi raisi wetu will do anyhthing to please the so called investors?? (US released 600million usd after BOT report??)Kwakweli nadhani sasa ntabalisha msimamo wangu coz sikumbuki benefits zozote toka serikalini...wacha wale walio kitengo...lets stop pointing fingers and tukubali kwamba ni serikali nzima imeoza...and if we want change we shud think of changing the whole govt and the way it works...maoni tuu
 
YETU MACHO JAMANI KAMA SERIKALI ILIWEZA KUMFIKISHA HUYU BALOZI MAHAKAMANI INASUBIRI NINI KUWAFIKISHA HAO AKINA JEETU NA KAGODA AMBAO WAMEKUNYWA PESA KIBAO.KWELI MCHEZO MCHAFU TZ HAUWEZI KWISHA KABISA
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom