BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,790
- 288,139
Posted Date::10/16/2007
Mahakama yaamru serikali kumlipa mfanyabiashara Sh15bilioni
Na Frederick Katulanda, Mwanza
Mwananchi
MAHAKAMA imeiamuru Serikali kuilipa kampuni ya Mansoor Oil Industries Ltd (MOIL) ya jijini Mwanza jumla ya Sh14.7bilioni
kutokana na uamuzi uliotolewa na Waziri wa Ujenzi wakati huo John Pombe Magufuli wa kuvunja kituo cha mafuta cha kampuni hiyo.
Uamuzi huo umetolewa na Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza katika kesi ya madai namba 2 ya mwaka 2002 ambapo
kampuni hiyo ilikuwa ikiwashitaki Waziri Magufuli, Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (wakati
huo) Brigedia Hassani Ngwilizi, Mwanasheria Mkuu wa Serikali Andrew Chenge pamoja na Halmashauri ya Jiji la Mwanza.
Katika kesi hiyo madai ya kampuni hiyo ya MOIL kwa serikali yalikuwa jumla ya Sh.18bilioni kutokana na kuvunjiwa kituo hicho cha mafuta kilichokuwa kimejengwa katika kiwanja namba 178 Kitalu A eneo la Kirumba kando ya barabara ya Makongoro.
Katika madai hayo, kampuni hiyo iliomba kulipwa kiasi cha Sh 593milioni kama thamani ya jengo ambalo lilibomolewa kwa amri ya Waziri Magufuli, Sh13.4 bilioni ikiwa ni kiasi cha faida ambacho ingekipata katika kipindi cha miaka 33 ambacho ilitarajiwa kufanya biashara na Sh 4 bilioni kama hasara ya jumla ya mradi huo.
Katika hukumu hiyo iliyotolewa Agosti 30, mwaka huu na Hakimu Mfawidhi H. Mushi kwa niaba ya Jaji Lawrence Mchome, mahakama ilisema baada ya kusikiliza pande zote ikiwa ni pamoja na kupitia vielelezo na ushahidi mbalimbali iliridhika na hivyo kutoa uamuzi kuwa mlalamikaji anapaswa kulipwa fidia katika madai yake.
Katika hukumu hiyo, Mahakama imesema kwamba mdai alikuwa na vibali halali vinavyoruhusu kuendesha shughuli zake katika eneo hilo, na kwa mujibu wa sheria, Rais ndiye alikuwa na uwezo wa kubatilisha vibali hivyo na si waziri.
Mahakama iliamuru Serikali Kuu kwa niaba ya washitakiwa watatu ambao ni Waziri Magufuli, Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za mitaa (wakati huo) Brigedia Hassani Ngwilizi, Mwanasheria Mkuu wa Serikali Andrew Chenge kulipa fidia kama ifuatavyo.
Kuilipa kampuni hiyo kiasi cha fidia ya Sh 490 milioni badala ya Sh 593 milioni alizoomba, kumlipa Sh13.4 bilioni kama fidia ya faida ambayo angepata katika kipindi cha miaka 33 na kumlipa kiasi cha Sh 730 milioni ambacho ni sehemu ya Sh 4 bilioni, aliyoomba kama hasara ya jumla katika mradi huo wa kituo cha mafuta.
Katika hukumu hiyo, mahakama imemwondoa mlalamikiwa mmoja ambaye ni Halamshauri ya Jiji la Mwanza kwa kuwa
hakuhusika na uvunjaji wa kituo hicho.
Pia mahakama imeamuru serikali kumlipa mdai huyo kiasi cha asiliamia 17 ya madai yake ya hasara ya
jumla ya Sh730 milioni kwa mwaka tangu siku jengo hilo lilipobomolewa Juni 21, 2001 hadi siku ya hukumu ilipotolewa.
Makahama imeamuru kulipwa kwa mdai huyo tena kiasi cha asiliamia hizo 17 ya Sh13.4 bilioni kwa mwaka ambayo ni madai yake ya hasara kutoka siku jengo lilipobomolewa hadi siku ya hukumu.
Kituo hicho kilibomolewa wakati tayari kikiwa kimekaguliwa na Halmashauri ya Jiji la Mwanza na kutoa hati ya umiliki wa kiwanja hicho Na. 033005/167 ya muda wa miaka 33 pamoja na hati ya kuruhusu ujenzi wa kituo hicho na Na. 00785.
Katika kesi hiyo MOIL ilikuwa ikitetewa na mawakili Salum Magongo na Paulin Rugaimukamu wote wa
jijini Mwanza wakati serikali ilikuwa ikitetewa na mawakili Michael Kamba na Edwin Kakolaki.
Mahakama yaamru serikali kumlipa mfanyabiashara Sh15bilioni
Na Frederick Katulanda, Mwanza
Mwananchi
MAHAKAMA imeiamuru Serikali kuilipa kampuni ya Mansoor Oil Industries Ltd (MOIL) ya jijini Mwanza jumla ya Sh14.7bilioni
kutokana na uamuzi uliotolewa na Waziri wa Ujenzi wakati huo John Pombe Magufuli wa kuvunja kituo cha mafuta cha kampuni hiyo.
Uamuzi huo umetolewa na Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza katika kesi ya madai namba 2 ya mwaka 2002 ambapo
kampuni hiyo ilikuwa ikiwashitaki Waziri Magufuli, Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (wakati
huo) Brigedia Hassani Ngwilizi, Mwanasheria Mkuu wa Serikali Andrew Chenge pamoja na Halmashauri ya Jiji la Mwanza.
Katika kesi hiyo madai ya kampuni hiyo ya MOIL kwa serikali yalikuwa jumla ya Sh.18bilioni kutokana na kuvunjiwa kituo hicho cha mafuta kilichokuwa kimejengwa katika kiwanja namba 178 Kitalu A eneo la Kirumba kando ya barabara ya Makongoro.
Katika madai hayo, kampuni hiyo iliomba kulipwa kiasi cha Sh 593milioni kama thamani ya jengo ambalo lilibomolewa kwa amri ya Waziri Magufuli, Sh13.4 bilioni ikiwa ni kiasi cha faida ambacho ingekipata katika kipindi cha miaka 33 ambacho ilitarajiwa kufanya biashara na Sh 4 bilioni kama hasara ya jumla ya mradi huo.
Katika hukumu hiyo iliyotolewa Agosti 30, mwaka huu na Hakimu Mfawidhi H. Mushi kwa niaba ya Jaji Lawrence Mchome, mahakama ilisema baada ya kusikiliza pande zote ikiwa ni pamoja na kupitia vielelezo na ushahidi mbalimbali iliridhika na hivyo kutoa uamuzi kuwa mlalamikaji anapaswa kulipwa fidia katika madai yake.
Katika hukumu hiyo, Mahakama imesema kwamba mdai alikuwa na vibali halali vinavyoruhusu kuendesha shughuli zake katika eneo hilo, na kwa mujibu wa sheria, Rais ndiye alikuwa na uwezo wa kubatilisha vibali hivyo na si waziri.
Mahakama iliamuru Serikali Kuu kwa niaba ya washitakiwa watatu ambao ni Waziri Magufuli, Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za mitaa (wakati huo) Brigedia Hassani Ngwilizi, Mwanasheria Mkuu wa Serikali Andrew Chenge kulipa fidia kama ifuatavyo.
Kuilipa kampuni hiyo kiasi cha fidia ya Sh 490 milioni badala ya Sh 593 milioni alizoomba, kumlipa Sh13.4 bilioni kama fidia ya faida ambayo angepata katika kipindi cha miaka 33 na kumlipa kiasi cha Sh 730 milioni ambacho ni sehemu ya Sh 4 bilioni, aliyoomba kama hasara ya jumla katika mradi huo wa kituo cha mafuta.
Katika hukumu hiyo, mahakama imemwondoa mlalamikiwa mmoja ambaye ni Halamshauri ya Jiji la Mwanza kwa kuwa
hakuhusika na uvunjaji wa kituo hicho.
Pia mahakama imeamuru serikali kumlipa mdai huyo kiasi cha asiliamia 17 ya madai yake ya hasara ya
jumla ya Sh730 milioni kwa mwaka tangu siku jengo hilo lilipobomolewa Juni 21, 2001 hadi siku ya hukumu ilipotolewa.
Makahama imeamuru kulipwa kwa mdai huyo tena kiasi cha asiliamia hizo 17 ya Sh13.4 bilioni kwa mwaka ambayo ni madai yake ya hasara kutoka siku jengo lilipobomolewa hadi siku ya hukumu.
Kituo hicho kilibomolewa wakati tayari kikiwa kimekaguliwa na Halmashauri ya Jiji la Mwanza na kutoa hati ya umiliki wa kiwanja hicho Na. 033005/167 ya muda wa miaka 33 pamoja na hati ya kuruhusu ujenzi wa kituo hicho na Na. 00785.
Katika kesi hiyo MOIL ilikuwa ikitetewa na mawakili Salum Magongo na Paulin Rugaimukamu wote wa
jijini Mwanza wakati serikali ilikuwa ikitetewa na mawakili Michael Kamba na Edwin Kakolaki.