Mahakama ya Kisutu yawahukumu wezi wa EPA, Maranda na Farijala miaka 22 jela

ByaseL

JF-Expert Member
Nov 22, 2007
2,225
247
Habari kutoka Mahakama ya Kisutu inasema Maranda na Farijala wamefungwa jumla ya miaka kwa wizi wa EPA. Wakitoka wanalipa pesa walizokwapua

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu imemhukumu mfanyabiashara Rajabu Maranda na binamu yake, kifungo cha miaka mitano jela kwa makosa sita, likiwemo la kujipatia sh. bilioni 1.8 kupitia akaunti ya EPA. Maranda na binamu yake Farijala Hussein, pia wameamriwa kulipa fedha hizo, vinginevyo mali zao zitakamatwa na kufilisiwa. Hukumu hiyo ilitolewa jana na jopo la mahakimu watatu waliosikiliza kesi hiyo ya kujipatia fedha mali ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT), kupitia akaunti ya EPA.

Akisoma hukumu hiyo kwa saa mbili, Hakimu Ilvin Mugeta, alisema washitakiwa wametiwa hatiani katika makosa sita kati ya manane waliyoshitakiwa. Miongoni mwa makosa waliyotiwa hatiani ni ya kughushi, kuwasilisha hati za uongo na kujipatia ingizo la fedha kwa njia za udanganyifu. Mahakimu Mugeta, Saul Kinemela na Phocus Bampikya, waliyafuta mashitaka mawili ya kula njama kwa nia ya kutenda kosa na wizi. Kwa mujibu wa Mugeta, walipitia ushahidi uliotolewa mahakamani na kuridhika na upande wa mashitaka kuwa, washitakiwa walitenda makosa hivyo kuwahukumu kila mmoja kutumikia kifungo cha miaka 21 jela.

Hata hivyo, Hakimu Mugeta alisema washitakiwa watatumika vifungo vya miaka mitano jela kila mmoja, kwa kuwa adhabu hizo zitatumikiwa kwa pamoja. Hakimu Mugeta alisema kwa mujibu wa Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai iliyotumika kuwatia hatiani, mahakama inawaamuru washitakiwa kurudisha fedha walizojipatia kwa mwenye mali, vinginevyo mali zao zitakamatwa na watafilisiwa. Alisema watuhumiwa wana uhuru wa kukata rufani. Awali, Wakili Mkuu wa Serikali Boniface Stanslaus aliiomba mahakama itoe adhabu kali kwa washitakiwa kwa kuzingatia kiasi kikubwa cha fedha kilichochukuliwa na madhara yaliyotokea kwa wananchi.

Stanslaus aliiomba mahakama itumie mamlaka yake kupitia kifungu cha 358 (1) cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai kutoa amri kwa watuhumiwa kurudisha fedha hizo BoT. Wakili anayewatetea washitakiwa hao, Majura Magafu, alidai kifungu cha 358 kama kilivyorekebishwa mwaka 2009 kinaangukia chini ya makosa ambayo yapo ukurusa wa 27 wa Sheria ya Kanuni ya Adhabu. Alidai makosa hayo ni ya kughushi, hivyo ombi la kurudisha fedha halistahili na mahakama iangalie vifungu hivyo.

Majura aliiomba mahakama isitoe amri ya washitakiwa kurudisha fedha kwa kuwa serikali kama itaona kuna haja ya kurudisha, wanaweza kufanya mchakato wa kuzirudisha. Aliiomba mahakama iwaonee huruma wateja wake, kwani ni makosa yao ya kwanza na hawajawahi kutiwa hatiani kwa makosa ya jinai. Majura alidai washitakiwa wanategemewa na familia zao na kwamba, ukiangalia makosa yaliyotendeka, kuna namna moja au nyingine kuwa yalifanyika kwa kutokujua au kuelekezwa na vyombo husika.

Alidai 'Deed of Assignment' zilipelekwa BoT na walihakikishiwa kwa mawasiliano na hatimaye walitoa fedha. Alidai kuna watu walishiriki kuwapotosha washitakiwa. Magafu alidai washitakiwa wanasumbuliwa na magonjwa ya figo na wamekuwa wakipelekwa hospitali mara kwa mara kwa matibabu. Wakili huyo alidai kwa mamlaka waliyopewa mahakimu wanaweza kuwaachia huru washitakiwa, baada ya kuwatia hatiani au kwa masharti wasifanye kosa lolote kwa kipindi cha miezi isiyozidi 12.

Hakimu Mugeta alisema kwa kuzingatia uzito wa makosa, washitakiwa hawastahili kusamehewa. Baada ya hukumu kusomwa, Magafu alidai wateja wake hawajaridhika, hivyo watakata rufani. Washitakiwa hao wanadaiwa kughushi, kuwasilisha hatia za uongo na kujipatia ingizo la sh. bilioni 1.8 mali ya BoT kwa njia ya udanganyifu wakonyesha kuwa, Kampuni ya Kiloloma and Brothers imepewa idhini ya kukusanya deni la kampuni ya BC Cars Export ya Mumbai, India.

Maranda na Hussein wanakabiliwa na kesi nyingine tatu za EPA, zikiwa ni miongoni mwa kesi kadhaa za EPA zilizofunguliwa katika Mahakama ya Kisutu. Kesi hizo zinawakabili wafanyabiashara maarufu na waliokuwa watumishi wa BoT.

Ndugu, jamaa na washitakiwa wengine wanaokabiliwa na kesi za EPA walikuwa miongoni mwa watu waliofika mahakama jana kusikiliza hukumu hiyo iliyoanza kusomwa saa 4.10 asubuhi. Baada ya hukumu kusomwa, baadhi ya ndugu na jamaa wa washitakiwa waliangua vilio. Saa 9.13 mchana washitakiwa walipandishwa kwenye gari lenye namba za usajili SCN 90008K lililokuwa na askari wawili wenye silaha na kupelekwa gereza la Ukonga. Wakati washitakiwa hao wakipanda kwenye gari, vilio na simanzi vilitawala mahakamani, huku baadhi ya ndugu wakiwa wamekusanyika kwenye makundi.

Fedha za EPA zawatupa jela
 
Habari kutoka Mahakama ya Kisutu inasema Marando na Farijala wamefungwa jumla ya miaka kwa wizi wa EPA. Wakitoka wanalipa pesa walizokwapua

Hukumu hiyo inawahusu wao wenyewe au hata wale walirudisha kama Jeetu Patel?
 
Mhhh kuna porojo hapa nadhani hii ni kuwafunga watu macho baada ya miezi miwili wanakata rufaa na kuachiwa,sijui kama kitu hapa.....
 
Mkuu hapo Juu ni Maranda sio Marando
Hii ni kubwa sana sana na walipaswa kupewa kifungo kikubwa zaidi maana hii ni uhujumu uchumi
 
Habari kutoka Mahakama ya Kisutu inasema Marando na Farijala wamefungwa jumla ya miaka kwa wizi wa EPA. Wakitoka wanalipa pesa walizokwapua

Nini maana ya Jumla? Je ina maana kila mmoja amefungwa miaka 11 jela?
 
I hope ni habari za kweli

CHADEMA watanasema hao jamaa wameonewa

What a shame kwa Chama kama Chadema , angehukumiwa Chenge na Lowasa pia wangesema wanaonewa na Kikwete

Damned if do damned if you dont!!
 
Waache wafungwe tu, si wangesema waliowatuma hizo hela?Maana tunajua wao walitumika tu kukwapua hela za EPA
 
magazeti yao ya uhuru, habari leo na jamba leo yamekosa cha kuandika kwa siku kadhaa mfululizo. naona sasa wameamua kuyatengenezea headlines.

kama jeetu patel hajafungwa, hiyo hukumu ni batili.
 
they knew what they were doing and got exactly what they were looking! tusibiri na hao wahindi
 
walau!isije ikatokea appeal,na wangelipa hela b4 going to jail,just incase wanafia huko!tunahitaji sheria ya china,mafisadi wapate death penalty!
 
I hope ni habari za kweli

CHADEMA watanasema hao jamaa wameonewa

What a shame kwa Chama kama Chadema , angehukumiwa Chenge na Lowasa pia wangesema wanaonewa na Kikwete

Damned if do damned if you dont!!
Habari za kuzinduka toka usingizini. Enjoy your snap
 
I hope ni habari za kweli

CHADEMA watanasema hao jamaa wameonewa

What a shame kwa Chama kama Chadema , angehukumiwa Chenge na Lowasa pia wangesema wanaonewa na Kikwete

Damned if do damned if you dont!!
Unapenda sana kudandia treni kwa mbele
 
Back
Top Bottom