Mahakama ya kadhi hii hapa!

kilimasera

JF-Expert Member
Dec 2, 2009
3,068
266
SHEIKH mkuu wa Tanzania, Mufti Issa bin Shaaban Simba amedai kuwa serikali imekubali kuirejesha Mahakama ya Kadhi nchini na kwamba mchakato wake ulisimama kupisha uchaguzi mkuu.

Mufti Simba alisema hayo jana alipokuwa akitoa salamu za mwaka mpya wa Kiislaamu wa 1432AH na akaweka bayana kuwa kipaumbele kikubwa kwa Waislamu katika mwaka huo ni kuona Mahakama ya Kadhi inaanza kazi na serikali kuitambua siku ya maadhimisho ya mwaka mpya wa Kiislamu kwa kuifanya iwe ya mapumziko.

“Mchakato wa Mahakama ya Kadhi unaendelea na umefikia mahala pazuri kwa sababu serikali imeshakubali kuirejesha," alisema Mufti Simba.

Kauli hiyo ya Mufti Simba imetolewa baada ya makamu wa rais, Dk Mohamed Gharib Bilal kueleza Novemba 17 wakati akijibu salamu za Baraza Kuu la Waislamu kuwa Waislamu nchini wataona matunda mazuri ya kilio chao hivi karibuni.
“Kuhusu Mahakama ya Kadhi, insha-Allah Mungu tutawafikisha kuona matunda mazuri muda si mrefu,” alisema Dk Bilal.
Kilio cha Waislamu kudai Mahakama ya Kadhi kiliongezeka katika miaka miwili iliyopita wakati walipoanza kuishambulia serikali kwa kushindwa kutekeleza ahadi ya chama tawala ya kuwaanzishia chombo hiyo kwa madai ni sehemu ya ilani yake ya uchaguzi wa mwaka 2005.

Baada ya mvutano wa muda mrefu na viongozi wa dini ya Kiislamu, serikali ilitoa taarifa kuwa Mahakama ya Kadhi itaundwa nje ya mfumo wa sheria za nchi na kuunda kamati ya kushughulikia utekelezaji wa maazimio hayo.
Akizungumza na wanahabari ofisini kwake jijini Dar es Salaam jana, Mufti Simba aliwatoa wasiwasi Waislaamu wote nchini kuhusu Mahakama ya Kadhi akieleza kuwa mchakato wake ulisimama kupisha uchaguzi.
“Mchakato wa Mahakama ya Kadhi ulisimama kwa sababu baadhi ya watu ambao tulikuwa nao katika mazungumzo walikuwa wanagombea,” alisema Mufti Simba.

“Kilichobaki ni kuweka mfumo mzuri ambao utaendesha mahakama hiyo. Kwa hiyo siku chache zijazo majopo yote mawili yatarudi mezani kumalizia mchakato na hatimaye mahakama ianze kufanya kazi.”
Hata hivyo, mufti Simba alisema kuwa Waislaamu hudai mambo yao kistaarabu na kwamba hakuna haja ya kuweka shinikizo kwa maandamano, migomo na mabango.

Kuhusu mapumziko siku ya maadhimisho ya mwaka mpya wa Kiislaamu, Mufti Simba alisema tayari wameshaiandikia serikali kuomba jambo hilo kama ilivyo kwa sherehe za maadhimisho ya miaka mingine.
Aliwataka Waislaamu kuijali siku hiyo na kufanya maadhimisho mbalimbali katika ngazi ya taifa, kanda, mkoa, wilaya, kata na hata msikiti, ikiiwa ni pamoja na kupamba nyumba zao na sehemu zao za kazi kuashiria sherehe hizo.

“Ili serikali iweze kutusikia na kutufikiria, lazima sisi wenyewe tuonekane tunaihitaji hiyo siku. Ombi tayari tumelifikisha serikalini na tunaamini serikali italishughulikia,” alisema Mufti Simba.
Mufti alisema mapumziko katika sikukuu ya mwaka mpya wa Kiislaam yangekuwapo, lakini kulikuwa na makosa mwanzoni.
“Miaka ya nyuma; wazee wetu kabla sisi hatujaja, waliulizwa wataje sikukuu za Waislaam, wakasema ni Idd Kubwa na Idd ndogo pamoja na siku ya Maulidi ya kuzaliwa kwa Mtume Muhammad (S.A.W). Wakaisahau siku ya mwaka mpya wa kiislaamu,” alibainisha Mufti Simba.

Mufti aliwata Waislaamu kuingia katika mwaka mpya wa 1432 ambao ulianza jana kwa kuwajibika katika kujitafutia maendeleo na sio kutegemea wafadhili katika kila jambo.
Aliwataka Waislaam kuhama kutoka katika maovu na kuhamia katika kufanya mema na kushiriki katika kazi za ujenzi wa taifa.

Aliwaombea dua viongozi wa nchi, akiwemo Rais Jakaya Kikwete, Makamu wake na baraza lote la mawaziri na kuwataka kuihamisha Tanzania kutoka katika hali iliyopo sasa ya kiuchumi na kuipeleka kwenye maendeleo mazuri.
 
SHEIKH mkuu wa Tanzania, Mufti Issa bin Shaaban Simba amedai kuwa serikali imekubali kuirejesha Mahakama ya Kadhi nchini na kwamba mchakato wake ulisimama kupisha uchaguzi mkuu.

Mufti Simba alisema hayo jana alipokuwa akitoa salamu za mwaka mpya wa Kiislaamu wa 1432AH na akaweka bayana kuwa kipaumbele kikubwa kwa Waislamu katika mwaka huo ni kuona Mahakama ya Kadhi inaanza kazi na serikali kuitambua siku ya maadhimisho ya mwaka mpya wa Kiislamu kwa kuifanya iwe ya mapumziko.

"Mchakato wa Mahakama ya Kadhi unaendelea na umefikia mahala pazuri kwa sababu serikali imeshakubali kuirejesha," alisema Mufti Simba.

Kauli hiyo ya Mufti Simba imetolewa baada ya makamu wa rais, Dk Mohamed Gharib Bilal kueleza Novemba 17 wakati akijibu salamu za Baraza Kuu la Waislamu kuwa Waislamu nchini wataona matunda mazuri ya kilio chao hivi karibuni.
"Kuhusu Mahakama ya Kadhi, insha-Allah Mungu tutawafikisha kuona matunda mazuri muda si mrefu," alisema Dk Bilal.
Kilio cha Waislamu kudai Mahakama ya Kadhi kiliongezeka katika miaka miwili iliyopita wakati walipoanza kuishambulia serikali kwa kushindwa kutekeleza ahadi ya chama tawala ya kuwaanzishia chombo hiyo kwa madai ni sehemu ya ilani yake ya uchaguzi wa mwaka 2005.

Baada ya mvutano wa muda mrefu na viongozi wa dini ya Kiislamu, serikali ilitoa taarifa kuwa Mahakama ya Kadhi itaundwa nje ya mfumo wa sheria za nchi na kuunda kamati ya kushughulikia utekelezaji wa maazimio hayo.
Akizungumza na wanahabari ofisini kwake jijini Dar es Salaam jana, Mufti Simba aliwatoa wasiwasi Waislaamu wote nchini kuhusu Mahakama ya Kadhi akieleza kuwa mchakato wake ulisimama kupisha uchaguzi.
"Mchakato wa Mahakama ya Kadhi ulisimama kwa sababu baadhi ya watu ambao tulikuwa nao katika mazungumzo walikuwa wanagombea," alisema Mufti Simba.

"Kilichobaki ni kuweka mfumo mzuri ambao utaendesha mahakama hiyo. Kwa hiyo siku chache zijazo majopo yote mawili yatarudi mezani kumalizia mchakato na hatimaye mahakama ianze kufanya kazi."
Hata hivyo, mufti Simba alisema kuwa Waislaamu hudai mambo yao kistaarabu na kwamba hakuna haja ya kuweka shinikizo kwa maandamano, migomo na mabango.

Kuhusu mapumziko siku ya maadhimisho ya mwaka mpya wa Kiislaamu, Mufti Simba alisema tayari wameshaiandikia serikali kuomba jambo hilo kama ilivyo kwa sherehe za maadhimisho ya miaka mingine.
Aliwataka Waislaamu kuijali siku hiyo na kufanya maadhimisho mbalimbali katika ngazi ya taifa, kanda, mkoa, wilaya, kata na hata msikiti, ikiiwa ni pamoja na kupamba nyumba zao na sehemu zao za kazi kuashiria sherehe hizo.


"Ili serikali iweze kutusikia na kutufikiria, lazima sisi wenyewe tuonekane tunaihitaji hiyo siku. Ombi tayari tumelifikisha serikalini na tunaamini serikali italishughulikia," alisema Mufti Simba.
Mufti alisema mapumziko katika sikukuu ya mwaka mpya wa Kiislaam yangekuwapo, lakini kulikuwa na makosa mwanzoni.
"Miaka ya nyuma; wazee wetu kabla sisi hatujaja, waliulizwa wataje sikukuu za Waislaam, wakasema ni Idd Kubwa na Idd ndogo pamoja na siku ya Maulidi ya kuzaliwa kwa Mtume Muhammad (S.A.W). Wakaisahau siku ya mwaka mpya wa kiislaamu," alibainisha Mufti Simba.

Mufti aliwata Waislaamu kuingia katika mwaka mpya wa 1432 ambao ulianza jana kwa kuwajibika katika kujitafutia maendeleo na sio kutegemea wafadhili katika kila jambo.
Aliwataka Waislaam kuhama kutoka katika maovu na kuhamia katika kufanya mema na kushiriki katika kazi za ujenzi wa taifa.

Aliwaombea dua viongozi wa nchi, akiwemo Rais Jakaya Kikwete, Makamu wake na baraza lote la mawaziri na kuwataka kuihamisha Tanzania kutoka katika hali iliyopo sasa ya kiuchumi na kuipeleka kwenye maendeleo mazuri.

Safii ziku za kupumzika ziko chache sana tuletewe na hiyo!
 
Mi nawatakia kila la heri ktk kufanikisha hili la mahakama ya kadhi kwa ndugu zetu waislam.nadhani mahakama hiyo ikitumiwa vizuri itawanufaisha waislamu wote na wala haitagusa maslahi ya wakristo.
Ila msije mkataka nchi hii ijiunge na jumuiya ya kiislam oic.hapo ndipo hatutakubali kwani itakuwa sawa na kutusilimisha watanzania wote wakati idadi ya wakristo ni kubwa zaidi hapa tz.
All ze best.
 
Mi nawatakia kila la heri ktk kufanikisha hili la mahakama ya kadhi kwa ndugu zetu waislam.nadhani mahakama hiyo ikitumiwa vizuri itawanufaisha waislamu wote na wala haitagusa maslahi ya wakristo.
Ila msije mkataka nchi hii ijiunge na jumuiya ya kiislam oic.hapo ndipo hatutakubali kwani itakuwa sawa na kutusilimisha watanzania wote wakati idadi ya wakristo ni kubwa zaidi hapa tz.
All ze best.
unakubali mahakama ya kadhi unakataa OIC sikuelewi mkuu kama nakubali basi kila kitu kifanyike! hata OIC sioni tatizo kabisa!
 
Mimi ni kafiri,nailipa kodi serikali yangu,vyanzo vyangu vya mapato ni kama ufugaji na uuzaji wa nyama ya nguruwe,nalipwa riba na mabenki mbalimbali ambapo nakatwa kodi kwa kipato hiki,pia natengeneza na kuuza pombe za kienyeji ambazo pia hutozwa kodi.Mahakama ya kadhi ianzishwe,lakini sitarajii kadhi awe analipwa mshahara kwa kutumia fedha za mimi kafiri.Naamini serikali yangu ni secular government(is not bias in favour of any religion),hivyo sitarajii ijiingize kwenye mambo ya kidini,ikifanya hivyo itakuwa ni kichekesho na itakuwa ni serikali ya kiislamu na itapaswa kuondoka au kuondolewa madarakani mara moja.Mimi ni mfia dini na nipo teyari kufa kwa ajiri ya kutetea dini yangu.


TANZANIA BILA MAHAKAMA YA KADHI INAWEZEKANA HATA KAMA RAIS NA MAKAMU WAKE WOTE NI WAISLAMU :llama::llama::llama:
 
TANZANIA BILA MAHAKAMA YA KADHI INAWEZEKANA HATA KAMA RAIS NA MAKAMU WAKE WOTE NI WAISLAMU :llama::llama::llama:[/QUOTE]

kwani mahakama si zipo kibao kuna tofauti gani kati ya mahakama ya kadhi na mahakama za kawaida
 
kwani mahakama si zipo kibao kuna tofauti gani kati ya mahakama ya kadhi na mahakama za kawaida[/QUOTE]

Mahakama ya kadhi ni maalumu kwa ajiri ya kutatua migogoro ya miradhi,ndoa na mambo mengine yanayowahusu waamini wa dini ya kiislamu,na hutoa maamuzi yake kwa kutumia sheria na miongozo ya kiislamu.Wakati mahakama za kawaida husuluhisha migogoro mbalimbali kwa kutumia katiba mama na sheria mabalimbali zinazotoa miongozo ya namna ya kuongoza nchi na raia wake bila kujali dini zao.
 
Halafu si watataka POLISI na MAGEREZA ya kiislamu vinginevyo hizo mahakama za kiislamu zitafanyaje kazi bila POLISI na MAGEREZA?watuhumiwa watakamatwa vipi?watafungwa wapi?ikiwa mtuhumiwa siyo muislamu inakuwaje?....mimi sielewi hii kitu umuhimu wake
 
Udini mtupu unaonyeshwa na serikali.je wakatoliki wakitaka mahakama inayotumia canon laws itakuwaje? IN SHORT KIKWETE NI MDINI NA ANAPALILIA UDINI.
sasa kwanini walisitisha hizi ishu za mahakama ya kadhi mpaka uchaguz upite? its bkoz wanajua wanachofanya sio sawa na wangeadhibiwa kwa hilo. im bored by Vasco Dagama etal..
 
kwani mahakama si zipo kibao kuna tofauti gani kati ya mahakama ya kadhi na mahakama za kawaida

Mahakama ya kadhi ni maalumu kwa ajiri ya kutatua migogoro ya miradhi,ndoa na mambo mengine yanayowahusu waamini wa dini ya kiislamu,na hutoa maamuzi yake kwa kutumia sheria na miongozo ya kiislamu.Wakati mahakama za kawaida husuluhisha migogoro mbalimbali kwa kutumia katiba mama na sheria mabalimbali zinazotoa miongozo ya namna ya kuongoza nchi na raia wake bila kujali dini zao.[/QUOTE]
Mwana mie navyofahamu hapa tanzania raia tunaishi kwa ushirikiano kama kitu kimoja na tunaingiliana bila kujali dini na kuoana pia bila kujali dini sasa ikatokea ndoa ya mkristu na muislam wakaoana then ikatokea matatizo uliyoainisha itakuwaje sasa hapo!pia jela ya hii mahakama itakuwa wapi?na ninani atakaehusika na kukamata washtakiwa na pia kudhibiti nidhamu ya washtakiwa??
 
Mwana mie navyofahamu hapa tanzania raia tunaishi kwa ushirikiano kama kitu kimoja na tunaingiliana bila kujali dini na kuoana pia bila kujali dini sasa ikatokea ndoa ya mkristu na muislam wakaoana then ikatokea matatizo uliyoainisha itakuwaje sasa hapo!pia jela ya hii mahakama itakuwa wapi?na ninani atakaehusika na kukamata washtakiwa na pia kudhibiti nidhamu ya washtakiwa??[Originally posted by KILIMASERA]

Wao hawana jela ni kuchapana bakora,kukatana mikono na kuuana mara unapobainika kuwa umetenda kosa na hukumu hutolewa mara moja.Kuhusu ndoa za mseto,hapo ndiyo utata utakapojitokeza!yaani hivi ni vitu vya ajabu na ni vema wangevianzisha bila kuihusisha serikali.
 
kwani mahakama si zipo kibao kuna tofauti gani kati ya mahakama ya kadhi na mahakama za kawaida

Mahakama ya kadhi ni maalumu kwa ajiri ya kutatua migogoro ya miradhi,ndoa na mambo mengine yanayowahusu waamini wa dini ya kiislamu,na hutoa maamuzi yake kwa kutumia sheria na miongozo ya kiislamu.Wakati mahakama za kawaida husuluhisha migogoro mbalimbali kwa kutumia katiba mama na sheria mabalimbali zinazotoa miongozo ya namna ya kuongoza nchi na raia wake bila kujali dini zao.

Kwani bila hiyo mahakama hayo masuala yanashughulikiwa vipi?
 
TANZANIA BILA MAHAKAMA YA KADHI INAWEZEKANA HATA KAMA RAIS NA MAKAMU WAKE WOTE NI WAISLAMU :llama::llama::llama:

kwani mahakama si zipo kibao kuna tofauti gani kati ya mahakama ya kadhi na mahakama za kawaida[/QUOTE]
Mahakimu wake wamebobea kwenye masuala ya kumjua Allah.
 
Halafu si watataka POLISI na MAGEREZA ya kiislamu vinginevyo hizo mahakama za kiislamu zitafanyaje kazi bila POLISI na MAGEREZA?watuhumiwa watakamatwa vipi?watafungwa wapi?ikiwa mtuhumiwa siyo muislamu inakuwaje?....mimi sielewi hii kitu umuhimu wake
ikiwa mtuhumiwa siyo muislamu inakuwaje?
 
Kwani bila hiyo mahakama hayo masuala yanashughulikiwa vipi?[Originally posted by SAFARI NI SAFARI]

Kwa kawaida yangeshughulikiwa na mahakama hizi za kawaida na kwa muda mrefu yamekuwa yakishughulikiwa na mahakama hizihizi za kawaida.Kwa mfano kwa suala la miradhi ili kutambua uwepo wao serikali ilizigawanya sheria katika makundi matatu nayo ni sheria za kimila,sheria za kiislamu na sheria za kiserikali.Katika kutoa hukumu sheria za kiislamu za mirathi zimekuwa zikitumika ikibainika mhusika alikua muislamu na alikuwa anaishi maisha yake kwa kuzingatia sheria za kiislamu.Mimi sijui hawa jamaa wanatafuta nini?nafikiri lengo lao nchi hii iwe ya kiislamu!
 
SHEIKH mkuu wa Tanzania, Mufti Issa bin Shaaban Simba amedai kuwa serikali imekubali kuirejesha Mahakama ya Kadhi nchini na kwamba mchakato wake ulisimama kupisha uchaguzi mkuu.

Mufti Simba alisema hayo jana alipokuwa akitoa salamu za mwaka mpya wa Kiislaamu wa 1432AH na akaweka bayana kuwa kipaumbele kikubwa kwa Waislamu katika mwaka huo ni kuona Mahakama ya Kadhi inaanza kazi na serikali kuitambua siku ya maadhimisho ya mwaka mpya wa Kiislamu kwa kuifanya iwe ya mapumziko.

"Mchakato wa Mahakama ya Kadhi unaendelea na umefikia mahala pazuri kwa sababu serikali imeshakubali kuirejesha," alisema Mufti Simba.

Kauli hiyo ya Mufti Simba imetolewa baada ya makamu wa rais, Dk Mohamed Gharib Bilal kueleza Novemba 17 wakati akijibu salamu za Baraza Kuu la Waislamu kuwa Waislamu nchini wataona matunda mazuri ya kilio chao hivi karibuni.
"Kuhusu Mahakama ya Kadhi, insha-Allah Mungu tutawafikisha kuona matunda mazuri muda si mrefu," alisema Dk Bilal.
Kilio cha Waislamu kudai Mahakama ya Kadhi kiliongezeka katika miaka miwili iliyopita wakati walipoanza kuishambulia serikali kwa kushindwa kutekeleza ahadi ya chama tawala ya kuwaanzishia chombo hiyo kwa madai ni sehemu ya ilani yake ya uchaguzi wa mwaka 2005.

Baada ya mvutano wa muda mrefu na viongozi wa dini ya Kiislamu, serikali ilitoa taarifa kuwa Mahakama ya Kadhi itaundwa nje ya mfumo wa sheria za nchi na kuunda kamati ya kushughulikia utekelezaji wa maazimio hayo.
Akizungumza na wanahabari ofisini kwake jijini Dar es Salaam jana, Mufti Simba aliwatoa wasiwasi Waislaamu wote nchini kuhusu Mahakama ya Kadhi akieleza kuwa mchakato wake ulisimama kupisha uchaguzi.
"Mchakato wa Mahakama ya Kadhi ulisimama kwa sababu baadhi ya watu ambao tulikuwa nao katika mazungumzo walikuwa wanagombea," alisema Mufti Simba.

"Kilichobaki ni kuweka mfumo mzuri ambao utaendesha mahakama hiyo. Kwa hiyo siku chache zijazo majopo yote mawili yatarudi mezani kumalizia mchakato na hatimaye mahakama ianze kufanya kazi."
Hata hivyo, mufti Simba alisema kuwa Waislaamu hudai mambo yao kistaarabu na kwamba hakuna haja ya kuweka shinikizo kwa maandamano, migomo na mabango.

Kuhusu mapumziko siku ya maadhimisho ya mwaka mpya wa Kiislaamu, Mufti Simba alisema tayari wameshaiandikia serikali kuomba jambo hilo kama ilivyo kwa sherehe za maadhimisho ya miaka mingine.
Aliwataka Waislaamu kuijali siku hiyo na kufanya maadhimisho mbalimbali katika ngazi ya taifa, kanda, mkoa, wilaya, kata na hata msikiti, ikiiwa ni pamoja na kupamba nyumba zao na sehemu zao za kazi kuashiria sherehe hizo.

"Ili serikali iweze kutusikia na kutufikiria, lazima sisi wenyewe tuonekane tunaihitaji hiyo siku. Ombi tayari tumelifikisha serikalini na tunaamini serikali italishughulikia," alisema Mufti Simba.
Mufti alisema mapumziko katika sikukuu ya mwaka mpya wa Kiislaam yangekuwapo, lakini kulikuwa na makosa mwanzoni.
"Miaka ya nyuma; wazee wetu kabla sisi hatujaja, waliulizwa wataje sikukuu za Waislaam, wakasema ni Idd Kubwa na Idd ndogo pamoja na siku ya Maulidi ya kuzaliwa kwa Mtume Muhammad (S.A.W). Wakaisahau siku ya mwaka mpya wa kiislaamu," alibainisha Mufti Simba.

Mufti aliwata Waislaamu kuingia katika mwaka mpya wa 1432 ambao ulianza jana kwa kuwajibika katika kujitafutia maendeleo na sio kutegemea wafadhili katika kila jambo.
Aliwataka Waislaam kuhama kutoka katika maovu na kuhamia katika kufanya mema na kushiriki katika kazi za ujenzi wa taifa.

Aliwaombea dua viongozi wa nchi, akiwemo Rais Jakaya Kikwete, Makamu wake na baraza lote la mawaziri na kuwataka kuihamisha Tanzania kutoka katika hali iliyopo sasa ya kiuchumi na kuipeleka kwenye maendeleo mazuri.
Tatizo letu hatuijui katiba yetu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuhusu hili suala la dini! kinachoniuma zaidi hata viongozi wenyewe wa nchi hii hawaijui katiba yao ndi maana wanakurupuka tu kwenye sehemu zao za ibada na kuongea masuala ambayo hayapo kikatiba, nchi hii si ya kiislam jamani mkijua hapo tu suala la mahakama ya kadhi luanzishwa na serikali si tu litafutwa, bali kuondolewa katika mawazo ya wasiolewa katiba na taratibu
 
Qadi (also known as Qaadi, Qaadee, Qazi, Kazi or Kadi) (Arabic: قاضي qāḍī‎) is a judge ruling in accordance with the sharia, Islamic religious law appointed by the ruler of a Muslim Country. Because Islam makes no distinction between religious and secular domains, qadis' traditionally have jurisdiction over all legal matters involving Muslims. The judgment of a qadi must be based on ijmah, the prevailing consensus of the ulema, Islamic scholars.

A qadi must be an adult and free man(not a slave or having been one), a Muslim, sane, unconvicted of slander, educated in Islamic science, and his performance must be totally congruent with Sharia without using his own interpretation. In a trial in front of a qadi, it is the plaintiff who is responsible to bring evidence against the defendant in order to have him or her convicted. There are no appeals to the judgements of a qadi.The Qadi must exercise his office in a public place, the chief masjid is recommended, or, in his own house, where public should have free access. A qadi must not receive gifts from participants in a trial and he must be careful in engaging himself in trade. Despite the rules for the office, Muslim history is full of complaints about qadis. Often it has been a problem, that qadis have been managers of waqfs, religious endowments. The origin of the institution of qadi, is the old Arab arbitrator, the hakam, but qualities from officials in areas conquered by Arabs have been added to the structure.
 
ITAENDESHWA KWA GHARAMA ZA NANI ? KAMA NI KWA GHARAMA ZA SERIKALI WATAKUWA NA UPUNGUFU WA AKILI KICHWANI. :mod:
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom