Mahakama ya ICJ yaiamuru Uganda kuilipa DRC faini dola milioni 325

Suley2019

JF-Expert Member
Oct 7, 2019
1,813
4,544
1644470069053.png

Mahakama ya Kimataifa ya Haki (ICJ) ilitangaza Jumatano wiki hii kwamba dola Milioni 325 ndio kiasi cha fidia ambacho Uganda inapaswa kuilipa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, ambayo ilikuwa ikidai zaidi ya dola bilioni 11 kwa uvamizi wa Uganda mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo wakati wa vita vya miaka ya 1998-2003.

ICJ, mahakama ya juu zaidi ya Umoja wa Mataifa, ilibaini kwamba Uganda inapaswa kulipa DRC dola milioni 225 kwa kusababisha vifo vya raia wa nchi hiyo, dola Milioni 40 kwa uharibifu wa mali na dola milioni 60 kwa uharibifu wa maliasili, alisema jaji kiongozi wa mahakama hiyo, Joan Donoghue.

Kesi hii ilianza mwaka wa 2005, ikiwa ni pamoja na malalamiko ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo dhidi ya majirani zake wawili, Uganda na Rwanda, ambazo ziliendesha vita katika eneo hilo wakati huo.

Kigali ilijiondoa haraka katika kesi hii, kwa sababu Mahakama ilijikuta kuwa haina uwezo wa kuhukumu Rwanda. Imesalia Uganda, ambayo imepatikana na hatia ya kuingilia masuala ya DRC. Imetakiwa kurekebisha uharibifu iliyosababisha wakati wa uvamizi kati ya mwaka wa 1998 na 2003 na jeshi lake katika mkoa wa Ituri hasa.
 
Mahakama ya Kimataifa ya Haki, ICJ, imeiamuru Uganda kuilipa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo dola milioni 325 kama fidia kutokana na kujihusisha katika mgogoro kwenye jimbo la Ituri mwishoni mwa miaka 1990.

Amri ya kulipa fidia hiyo imetolewa leo zaidi ya miaka 15 baada ya mahakama hiyo ya Umoja wa Mataifa kutoa uamuzi katika hukumu ngumu yenye kurasa 119, kwamba mapigano yaliyofanywa na majeshi ya Uganda nchini Kongo yalikiuka sheria ya kimataifa.

Jaji Mkuu wa ICJ, Joan Donoghue amesema Uganda inapaswa kulipa dola milioni 225 kwa madhara waliyopata raia, dola milioni 40 kwa uharibifu wa mali na dola milioni 60 kwa uharibifu wa maliasili. Hata hivyo, kiasi kitakachotolewa ni chini ya kiwango kilichoombwa na Kongo na kuwasilishwa mahakamani cha zaidi ya dola bilioni 11.
 
Mahakama ya Kimataifa ya Haki, ICJ, imeiamuru Uganda kuilipa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo dola milioni 325 kama fidia kutokana na kujihusisha katika mgogoro kwenye jimbo la Ituri mwishoni mwa miaka 1990.

Amri ya kulipa fidia hiyo imetolewa leo zaidi ya miaka 15 baada ya mahakama hiyo ya Umoja wa Mataifa kutoa uamuzi katika hukumu ngumu yenye kurasa 119, kwamba mapigano yaliyofanywa na majeshi ya Uganda nchini Kongo yalikiuka sheria ya kimataifa.

Jaji Mkuu wa ICJ, Joan Donoghue amesema Uganda inapaswa kulipa dola milioni 225 kwa madhara waliyopata raia, dola milioni 40 kwa uharibifu wa mali na dola milioni 60 kwa uharibifu wa maliasili. Hata hivyo, kiasi kitakachotolewa ni chini ya kiwango kilichoombwa na Kongo na kuwasilishwa mahakamani cha zaidi ya dola bilioni 11.
Na kwa Rwanda vp, yenyewe haikushtakiwa ndg.
 
Back
Top Bottom