Mahakama ya Ardhi na NIDA inanifanyia hujuma mimi

Civilian Coin

JF-Expert Member
Dec 2, 2012
2,305
4,334
TUIFUNDISHE KAZI MAHAKAMA YA ARDHI na IDARA YA VITAMBULISHO VYA TAIFA(NIDA) KATIKA MABADILIKO YA MAJINA KISHERIA

Ndugu zangu na Mashabiki wangu, habari za asubuhi!

Naandika hotuba hii nikiwa ofisini Mkolani Sekondari nimekaa kwenye kiti na kunywa uji wa ulezi, naitwa DON NALIMISON, Mwanamziki, Mtetezi wa Haki za Binadamu na Maswala ya Ushauri ya Usalama. Leo tufahamu iwapo mtu amekula kiapo kisheria au kaenda kwa wakili kubadili jina, je Idara ya Mahakama ya Ardhi na NIDA wanawajibika kufanya nini?

Nchi inaongozwa na Sheria, na Sheria zimetungwa na Bunge na sisi ni watekelezaji wa Sheria, tunapoenda kinyume na Sheria hizo ni ishara Taifa linaongozwa na VICHAA wasiofata walichokitunga.

Leo DON NALIMISON nimeenda kwa Wakili nimefata Utaratibu wa Kisheria wa Kubadili Majina ambao unakubalika nchi nzima na dunia nzima. Lakini naenda Mahakama ya Ardhi ili kunihalalishia napewa Masharti ambayo hayana msingi wowote. Mtu kaleta viapo vyake na ameamua mwenyewe kwa mapenzi yàke. Sasa inakuwaje mnataka vielelezo vingine wakati Wakili au Mahakama au Jaji au Hakimu Kisha mdhibitisha kuwa kabadili jina.

Mahakama ya Ardhi inatakiwa kutoa hati bila kutaka vielelezo vingine bali vielelezo vya majina yaliyoachwa tu. Taifa hili halijui Sheria Ila linaigiza Sheria. Nao NIDA mtu anapokuja kubadilishiwa kitambulisho na anakielelezo cha kisheria iwe kwa Wakili au Mahakama wanatakiwa kumbadilishia jina muombaji kutokana na vielelezo vyake vya kisheria na sio kumshauri aendelee na jina la kwanza, Sheria imesha thibitisha kubadilika kwa jina na sahihi na hivyo, lazima mabadiliko ya jina lazima yafanyike ili pia DON NALIMISON aweze kupata Passport ya kusafiria akafanye show Marekani, Afrika Kusini na Uingereza na Australia.

Pia, ili aweze kufanya Mambo mengine katika jamii kwa jina alilochagua kisheria. Lakini ubumbumbu wa Sheria tunajikuta tunawekeana vikwazo vya kijinga visivyo na tija kwa Taifa.

Iweje Baraza la Mtihani linaruhusu mabadiliko ya majina ila nyinyi mkatae? Kuna haja ya wanasheria wafundwe upya maana ya utekelezaji wa Sheria, unajua kusoma Sheria sio KUJUA utekelezaji wa Sheria. Lazima Sheria ziheshimiwe nasio kusikiliza Mkuu wa Wilaya au Mkuu wa Mkoa au DAS/RAS au Waziri, Bali sikiliza Sheria inataka Nini?

Na je mhusika amefata Utaratibu wa Kisheria au lah, Kama amefata Utaratibu wa Kisheria Basi arekebishiwe haraka NIDA yake na Mahakama ya Ardhi impe hati yake bila pingamizi maana yeye ndiye aliyeamua kubadili jina nasio Mahakama Bali ni Sheria imemthibitisha. Zaidi utazipata zote kwa Lugha ya kiingereza kwenye Kitabu Cha "CONVICTION SHAPED MY KNOWLEDGE" kinachoandaliwa na DON NALIMISON mwenyewe.

DON NALIMISON.
O'CLOCK MUSIC PRESS.
20 JULAI 2020.
Simu: +255 682 94 29 01
 
... lazima MABADILIKO ya jina lazima yafanyike ili pia DON NALIMISON aweze kupata Passport ya kusafiria akafanye show Marekani, Afrika Kusini na Uingereza na Australia.

Hawa jamaa wanazingua, wafanye haraka aisee ili show zianze rasmi.

Sasa hivi nimeelewa kwa nini album yako ina nyimbo nyingi za kiingereza, target ni soko la nje.

Big up Don.
 
Don Nalimison dish halijayumba, ila Yuko kazini, kikosi maalum.
Umeshawahi kuona wapi mtu anafungwa miaka mitatu jela halafu anarudi kutumikia kwenye Ofisi ya serikali?
Hata magereza alienda kimkakati. Rejea ule waraka wake anaieleza kwa vielelezo mashtaka aliyekuwa nayo, Ni dhahiri alikuwa anajitafutia sababu ya kufungwa
Duuh watu wengine bwana... ila watu kama hawa wanapaswa kuwepo ili historia iandikwe kwa vizazi vijavyo!
 
Ooh my human of strength is here. You is know these humans is not want you to climb a bird and fly away. They is wants you to sit here here in Tanzania, is very many bad behaviour, bad behaviourn't?

You is now drinking porridge dry dry my human you is not eating powerful breakfast. Watch out not to that extent.
 
Hakuna kitu mm uncle kakaa gerezani 4 yrs kwa kosa la murder case bd kamaliza kifungo chake karudi serikalini , ni mikakati tu. Huyo jamaa sio TISS dishi limeyumba.
kwani mbali na ujomba unamfahamu vipi kaka wa mama yako????
 
Hakuna kitu mm uncle kakaa gerezani 4 yrs kwa kosa la murder case bd kamaliza kifungo chake karudi serikalini , ni mikakati tu. Huyo jamaa sio TISS dishi limeyumba.

Toka hapa kesi yangu ni hii ni "Kutoa Taarifa za Uongo Kwenye Mfumo wa Kompyuta"
 
Mahakama ya ardhi na kubadirisha jina vinahusiana vipi? Ukitaka kubadirisha jina kina stage za kufuata:

1. Unaenda kwa wakili/mahakaman kutengeneza kiapo/ instruments inatambulika kama Deed Poll. Amboyo utasign na itakua attested na wakili au hakimu au kamishina mwingine yoyote wa viapo umjuae.

2. Baada ya hatua ya kwanza unapeleka nyaraka yako/Deed Poll yako kuisajili na msajili wa nyaraka ambae ndio amekasimiwa kazi ya usajilo wa nyaraka. Na instrument/Deed Poll ina kua halali baada ya kusajiliwa.

NB: Msajili wa nyaraka anapatikana katika ofisi za msajili wa ardhi. Yaan msajili wa ardhi ndo msajili wa nyaraka japo majukumu yake ya usajili wa ardhi na usajili wa nyaraka anaufanya chini ya sheria mbili tofauti.
 
Don kula kiapo cha kuyakubali majina yote hili la Don na lile la awali la Deo Kisandu ili usiwe na sababu ya kubadili majina kwenye hati yako ya ardhi pamoja na NiDA ID.
 
Ni kweli na mpaka Leo sijajamiana.
Sasa Don si utumie huduma ya kununua? Unamtafuta Ijumaa usiku unamlipa gharama ya ijumaa usiku, jumamosi siku nzima na jumapili jioni ndiyo anaondoka.

Rahisisha mambo usije ukabaka bure tukaukosa muziki wako
 
  • Thanks
Reactions: _ID
Mkuu una ma - complaint mengi sana...
vp hujaenda tu Marekani....
manake ulisema siasa za Afrika zinakuboa!
 
Horseshoe Arch,

Don Nalimison dish halijayumba, ila yuko kazini, kikosi maalum.

Umeshawahi kuona wapi mtu anafungwa miaka mitatu jela halafu anarudi kutumikia kwenye Ofisi ya serikali?

Hata Magereza alienda kimkakati. Rejea ule waraka wake anaieleza kwa vielelezo mashtaka aliyekuwa nayo, Ni dhahiri alikuwa anajitafutia sababu ya kufungwa.
Huyu jamaa Kuna wakat nahisi dish lipo sawa ila saaingine simwelewi
 
Back
Top Bottom