Mahakama ya Afrika Mashariki imekataa ombi moja katika kesi ya kupinga Muungano wa Tanzania

Kunguru Mjanja

JF-Expert Member
Aug 22, 2012
2,036
3,929
Mahakama ya Haki ya Afrika Mashariki(EACJ) jana Septemba 19, 2018 imetupilia mbali kesi ya Rashid Salum Adiy na wenzake 39,999 dhidi ya Serikali ya Tanzania

Walifungua kesi hiyo mnamo Februari 13 mwaka huu wakipinga uhalali wa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar

Kwa mujibu wa Msemaji wa Serikali amesema sababu za kina za uamuzi huo zitatolewa baadae lakini Majaji wamewashauri walalamikaji kuwa wanaweza kuwasilisha madai yao upya katika Mahakama za Zanzibar

Katika shauri hilo, Serikali ilitetewa Mawakili waliongozwa na Naibu Wakili Mkuu wa Serikali Dkt. Ally Possi

=======

Mahakama ya Afrika Mashariki imetupilia mbali ombi lililowasilishwa na raia wa Zanzibar kupinga uwepo wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutaka kesi hiyo isikiliziwe Zanzibar.

Rashid Salum Adiy na wenzake 39,999 kutoka Zanzibar wamewasilisha kesi dhidi ya Serikali ya Tanzania wakisema muungano huo ni haramu.

Walalamishi walikuwa wamejitetea kwamba wengi wao ni wakazi wa Zanzibar na huenda ikawa vigumu kwao kuhudhuria vikao vya kusikilizwa kwa kesi hiyo iwapo itaendelea kusikiliziwa Zanzibar.

Ombi hilo limetupiliwa mbali na majaji katika mahakama hiyo mjini Arusha, ingawa hawakutoa maelezo kuhusu sababu zilizowaongoza kutoa uamuzi huo.

Katika uamuzi wake, majaji walisema hakuna haja na wala haifai kwa mahakama hiyo kuagiza kwamba vikao vya kesi hiyo viandaliwe Zanzibar.

Kifungu 68 cha sheria za mahakama hiyo kinawaruhusu kutoa uamuzi kwanza na kisha kutoa maelezo ya kina baadaye.

Wameahidi kutoa maelezo ya kina baadaye.

Katika kesi hiyo, Salum na wenzake wawawameshtaki miongoni mwa wengine Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Katibu Mkuu wa Baraza la Mapinduzi la Zanzibar na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.


Mwezi Machi, mahakama hiyo ilikuwa imetupilia mbali ombi la walalamishi la kutaka kumteua Japheth Kiziba kuwa mwakilishi mpya mahakamani.

Majaji wakiongozwa na Jaji Monica Mugenyi walilalamikia walichosema ni ishara za walalamishi kutochukulia kwa uzito kesi waliyokuwa wameiwasilisha, wakizungumzia moja ya maombi yaliyokuwa yamewasilishwa.

"Hii ni kama kuipotezea muda mahakama hii na ni hatua ambayo imesababisha kuchelewa kusikizwa kwa kesi hii, na pia ni kutumia vibaya mchakato wa mahakama," walisema majaji.

Wakati mmoja, walalamishi walijaribu kutumia lugha ya Kiswahili, jambo ambalo mahakama hiyo mwezi Machi ilisema linaenda kinyume na mkataba wa kuundwa kwa mahakama hiyo Kifungu 46 ambacho kinasema lugha ya Kiingereza ndiyo lugha pekee ya jumuiya hiyo.

-----
KUMRADHI: MAHAKAMA 'HAIJATUPILIA MBALI' KESI YA KUPINGA MUUNGANO BALI IMEKATAA OMBI MOJA KATIKA KESI HIYO

Mahakama ya Haki ya Afrika ya Mashariki imekataa ombi namba 7 la Walalamikaji 40,000 Waliotaka Kesi ya kupinga uhalali wa Muungano wa Tanzania ikasikilizwe Zanzibar

Kwenye uamuzi huo, Mahakama haikutajwa kuwa kesi yenyewe ya kuupinga uhalali wa Muungano imetupiliwa mbali

Walalamikaji hao wanaoongozwa na Rashid Salum Adiy Walifungua kesi hiyo mnamo Februari 13 mwaka huu

Hata hivyo, Msemaji wa Serikali kupitia akaunti yake katika Mtandao wa Twitter ameandika kuwa Mahakama hiyo imetupilia mbali kesi hiyo

Soma zaidi.....Mahakama ya Afrika Mashariki Arusha: Muendelezo wa kesi ya kuhoji uhalali wa muungano - JamiiForums
 
Not decided on merit, I guess! hivyo bado kuna nafasi ya kuipeleka tena ikitoka zanzibar ambako definitely watashindwa
 
Huu muungano hata shetani anajua utabaki milele,atakayetaka kuuvunja atavunjwa mwenyewe
 
  • Thanks
Reactions: Oii
Recent-Decisions


Jurisdiction


The Court has jurisdiction to hear and determine:
  • Disputes on the interpretation and application of the Treaty.
  • Disputes between the Community and its employees arising from the terms and conditions of employment or the interpretation and application of the staff rules and regulations
  • Disputes between the Partner States regarding the Treaty if the dispute is submitted to it under a special agreement
  • Disputes arising out of an arbitration clause contained in a contract or agreement which confers such jurisdiction on the Court to which the Community or any of its institutions is a party
  • Disputes arising out of an arbitration clause contained in a commercial contract or agreement in which the parties have conferred jurisdiction on the Court
  • The jurisdiction of the Court may be extended to human rights at a suitable date to be determined by the Council
 
Hawa wazanzibar waachiwe waondoke kama wanahisi wananyonywa maana tumewachoka,

Kwanza mtanzania bara ndo ananyonywa sana,

1.Uniti price ya umeme Zanzibar iko chini kuzidi bara,

2. Wanafunzi wa vyuo vikuu wote upata mikopo tena 100% wakati bara si hivo

3. Kutoa kitu Zanzibar kupeleka bara mpaka ushuru wakati kupeleka Zanzibar Si hivo,

4. Wana wawakilishi ndani ya bunge, bara haina
5. Wana rais sisi hatuna
 
Naijulikane kwamba hatoki mtu hapa!!!ila sarakasi rukhsa.
Haya mambo huwa yananishangaza sana inapotokea swala kama hili kwenye mataifa ambayo kuna ukrst haupendi mambo yanavyo kwenda hatuwa huchukuliwa haraka haraka mfano Sudan ndio ilikuwa inchi moja lakini waliweza kuigawa nakuwa nchi mbili nakutangaziwa dunia kuwa wamepata Uhuru ndani ya nchi moja nilitegemea kama ni Uhuru ungeombwa kwa Sudan nzima sio upande wa sudani sasa inashindikana nini kwa Tanganyika na Zanzibar na historia inaonyesha tokazamani zilikuwa nchi mbili tofauti?je au kunaupande unaudai upande mwingine ulipwe ilitufikietamati nini tatizo na muungano huu unalinda maslahi yanani wapewe nchi yao wafanye mambo yao wenyewe
 
Hawa wazanzibar waachiwe waondoke kama wanahisi wananyonywa maana tumewachoka,

Kwanza mtanzania bara ndo ananyonywa sana,

1.Uniti price ya umeme Zanzibar iko chini kuzidi bara,

2. Wanafunzi wa vyuo vikuu wote upata mikopo tena 100% wakati bara si hivo

3. Kutoa kitu Zanzibar kupeleka bara mpaka ushuru wakati kupeleka Zanzibar Si hivo,

4. Wana wawakilishi ndani ya bunge, bara haina
5. Wana rais sisi hatuna
Kama wanafanyiwa yote hayo lakini hawataki nafikiri hayo hawataki kwasababu niyaduniani nibora upate shida duniani kuliko kuyakosa mazuri ya ahadi waliowekewa na muumba
 
Mahakama ya Haki ya Afrika Mashariki(EACJ) jana Septemba 19, 2018 imetupilia mbali kesi ya Rashid Salum Adiy na wenzake 39,999 dhidi ya Serikali ya Tanzania

Walifungua kesi hiyo mnamo Februari 13 mwaka huu wakipinga uhalali wa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar

Kwa mujibu wa Msemaji wa Serikali amesema sababu za kina za uamuzi huo zitatolewa baadae lakini Majaji wamewashauri walalamikaji kuwa wanaweza kuwasilisha madai yao upya katika Mahakama za Zanzibar

Katika shauri hilo, Serikali ilitetewa Mawakili waliongozwa na Naibu Wakili Mkuu wa Serikali Dkt. Ally Possi

=======

Mahakama ya Afrika Mashariki imetupilia mbali ombi lililowasilishwa na raia wa Zanzibar kupinga uwepo wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutaka kesi hiyo isikiliziwe Zanzibar.

Rashid Salum Adiy na wenzake 39,999 kutoka Zanzibar wamewasilisha kesi dhidi ya Serikali ya Tanzania wakisema muungano huo ni haramu.

Walalamishi walikuwa wamejitetea kwamba wengi wao ni wakazi wa Zanzibar na huenda ikawa vigumu kwao kuhudhuria vikao vya kusikilizwa kwa kesi hiyo iwapo itaendelea kusikiliziwa Zanzibar.

Ombi hilo limetupiliwa mbali na majaji katika mahakama hiyo mjini Arusha, ingawa hawakutoa maelezo kuhusu sababu zilizowaongoza kutoa uamuzi huo.

Katika uamuzi wake, majaji walisema hakuna haja na wala haifai kwa mahakama hiyo kuagiza kwamba vikao vya kesi hiyo viandaliwe Zanzibar.

Kifungu 68 cha sheria za mahakama hiyo kinawaruhusu kutoa uamuzi kwanza na kisha kutoa maelezo ya kina baadaye.













Wameahidi kutoa maelezo ya kina baadaye.

Katika kesi hiyo, Salum na wenzake wawawameshtaki miongoni mwa wengine Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Katibu Mkuu wa Baraza la Mapinduzi la Zanzibar na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.


Mwezi Machi, mahakama hiyo ilikuwa imetupilia mbali ombi la walalamishi la kutaka kumteua Japheth Kiziba kuwa mwakilishi mpya mahakamani.

Majaji wakiongozwa na Jaji Monica Mugenyi walilalamikia walichosema ni ishara za walalamishi kutochukulia kwa uzito kesi waliyokuwa wameiwasilisha, wakizungumzia moja ya maombi yaliyokuwa yamewasilishwa.

"Hii ni kama kuipotezea muda mahakama hii na ni hatua ambayo imesababisha kuchelewa kusikizwa kwa kesi hii, na pia ni kutumia vibaya mchakato wa mahakama," walisema majaji.

Wakati mmoja, walalamishi walijaribu kutumia lugha ya Kiswahili, jambo ambalo mahakama hiyo mwezi Machi ilisema linaenda kinyume na mkataba wa kuundwa kwa mahakama hiyo Kifungu 46 ambacho kinasema lugha ya Kiingereza ndiyo lugha pekee ya jumuiya hiyo.

Soma zaidi.....Mahakama ya Afrika Mashariki Arusha: Muendelezo wa kesi ya kuhoji uhalali wa muungano - JamiiForums

Acha kudanganya watu. Badilisha kichwa cha habari kisomeke. MAHAKAMA YAKATAA KUSIKILIZA KEZI YA MUUNGANO ZANZIBAR.

Hapo hakuna mahala mahakama ilipotupilia mbali kesi ya muungano. Uwe makini wakati mwengine.
 
Afrika Mashariki hawawezi kutenda haki lazima hapo kidudu kitapenya katikati mi nadhan hili shauri likafunguliwe Mahakama za Kimataifa uko, apa ni kupoteza muda tu
 
1.Uniti price ya umeme Zanzibar iko chini kuzidi bara,

2. Wanafunzi wa vyuo vikuu wote upata mikopo tena 100% wakati bara si hivo

3. Kutoa kitu Zanzibar kupeleka bara mpaka ushuru wakati kupeleka Zanzibar Si hivo,
Mkuu umeshaamka? Kanawe uso kwanza!!
 
I KNOW WHY A CAGED BIRD SINGS.
BY MAYA ANGELOU
A free bird leaps
on the back of the wind
and floats downstream
till the current ends
and dips his wing
in the orange sun rays
and dares to claim the sky.

But a bird that stalks
down his narrow cage
can seldom see through
his bars of rage
his wings are clipped and
his feet are tied
so he opens his throat to sing.

The caged bird sings
with a fearful trill
of things unknown
but longed for still
and his tune is heard
on the distant hill
for the caged bird
sings of freedom.

The free bird thinks of another breeze
and the trade winds soft through the sighing trees
and the fat worms waiting on a dawn bright lawn
and he names the sky his own

But a caged bird stands on the grave of dreams
his shadow shouts on a nightmare scream
his wings are clipped and his feet are tied
so he opens his throat to sing.

The caged bird sings
with a fearful trill
of things unknown
but longed for still
and his tune is heard
on the distant hill
for the caged bird
sings of freedom.
 
Some Birds Are Not Meant To Be Caged

Some birds are not meant to be caged, that's all. Their feathers are too bright, their songs too sweet and wild. So you let them go, or when you open the cage to feed them they somehow fly out past to you. And the part of you that knows it was wrong to imprison them in the first place rejoices, but still, the place where you live is that much more drab and empty for their departure

- Stephen King.
 
Katika mambo ya kijinga kabisa ambayo nimeyashuhudia hapa duniani ni hii union .Anayeyonywa ndo kamng'ang'ania mnyonyaji.
mtaani wanadai eti muungano upo kwa ajili ya kudhibiti dini ya visiwani..kwa hiyo usishangae
 
Back
Top Bottom