Mahakama ya Afrika Mashariki Arusha: Muendelezo wa kesi ya kuhoji uhalali wa muungano

Kurudi kwa mamlaka kamili ya zanzibar
1. Uhamiaji
2. International relations
3. Current
4. Banks
5. Economic
6. Natural resources
7. Nationality
8. Politics
9. Tax
10
11.
12
13
Kwa kweli kurudi kwa mamlaka ya zanzibar kama nchi huru itabidi mjipange sana .....maana sio rahisi kama mnavyodhan
 
Ni muungano Wa kishirikina, hauna hasara wala faida, hauna ridhaa ya wananchi, tamaduni hazina mlingani, walio ubuni wamejifia, hauna uhalisia wa muungano, upo kichina kichina, wananchi wameuchoka........nyingine ongeza wewe kama huzioni nitakushangaa
Mjipange sana .....muungano huu hamuuwezi ......kuuvunja sio rahisi kama unavyodani ndugu yangu.fikirieni sana hili. Msitumie dini kuuvuruga muungano
 
Taarifa ya kuendelea kusikilizwa kwa kesi ya Muungano katika Mahakama ya Afrika Mashariki Arusha, Ombi no.9 lililowasilishwa na waombaji 40,000. linalohusiana na kuzuiliwa serikali zote mbili za Tanzania kutokufanya mabadiliko ya katiba za nchi ,kati ya Zanzibar na Tanzania.

Kutokufanyika kwa kura ya maoni juu ya suala la Muungano, kuwekewa vikwazo mbambali serikali ya Tanzania kimataifa katika nyanja mbali mbali na nchi za Afrika Mashariki, Afrika na Ulimwengu mzima.

Pamoja na mashirika ya kimataifa hadi kesi ya msingi itakapo malizika kusikilizwa na kutolewa hukumu, Ombi hili litasikilizwa mbele ya Majaji 5 siku ya Jumatano tarehe 6/6/2018 hapo Arusha saa 3:30 asubuhi. kuhusu ombi la kesi kuja kusikilizwa Zanzibar bado halijapangwa ingawa tumewasilisha marekebisho lakini mahakama italipanga kulisikiliza tena baada ya kulisikiliza ombi hili no,9.

Tunawaombeni Wazanzibari nyote tuungane kwa kulifuatilia shauri hili kwa manufaa ya nchi yetu,tafadhali sana kwa uzalendo wako ewe Mzanzibari tunahitaji mchango wako wa fikra n.k.
ili kuweza kutimiza lengo letu la kuikombowa nchi yetu katika ukoloni mambo leo wa Taifa la Tanganyika.
Tafadhali share na wengine taarifa hii.
# ZanzibarKwanza
# AjendaYaZanzibar

Habari zaidi, soma=>Wazanzibar elfu 40 wafungua kesi mahakamani kupinga muungano

View attachment 782025
Mahakama hiyo haina mamlaka ya kuongelea masuala yasio na mashiko kisheria. Muungano upo kwa mujibu wa katiba na hati alizosaini karume na nyerere zipo sasa mtakimbilia wapi?? MKITULETEA FIGISU UHAINI UTAWAHUSU ALAAH
 
....wanafikiri suala la sovereign ni kitu cha mchezo mchezo, watapata tabu sana !
Taiwan inadai sovereign mpaka leo hapati....china haikubali. Na hivo hivo Zanzibar wanaodai kuwa huru kama nchi yenye mamlaka kamili wajue kuwa hatuko tayari kupoteza ardhi yetu (Tanzania) na muungano wetu kizembe khahh
 
Kurudi kwa mamlaka kamili ya zanzibar
1. Uhamiaji
2. International relations
3. Current
4. Banks
5. Economic
6. Natural resources
7. Nationality
8. Politics
9. Tax
10
11.
12
13
1. Uhamiaji- kitambulisho cha mkaazi
2. Kuna Balozi rasmi kadhaa hapo Unguja. Naibu wa Waziri (nje) ni lazima awe mzanzibari
3. Current !??
4. Banks (ipo Banki ya watu wa Zinjibar)
5. Economics - utalii na uvuvi na uchuuzi
6. Natural resources, sheria ya mafuta ilibadilishwa mafuta yote yapo chini ya mamlaka yao
7. Nationality - Uzanzibari na Uzanzibara
8. Politics - CUF, CCM, Chadema, ACT, UPD, chauma
9. TAX - ZRB (Zanzibar revenue authority)
 
Taiwan inadai sovereign mpaka leo hapati....china haikubali. Na hivo hivo Zanzibar wanaodai kuwa huru kama nchi yenye mamlaka kamili wajue kuwa hatuko tayari kupoteza ardhi yetu (Tanzania) na muungano wetu kizembe khahh
Hong Kong imerudishwa kwenye mamalaka ya China, na wenyewe wakiona
 
Bado huelewi kuwa huo si muungano ???

Uvamizi ulipewa jina la muungano tarehe 26, Aprili 1964

Zanzibar imevamiwa Januari 12 , 1964 na Waziri mkuu na mawaziri wenzake wa Zanzibar wamekamatwa na kupelekwa kwenye majela ya Tanganyika Januari 1964 ,

KUNA MUUNGANO HAPO ??????

Hivi Iddi Amin alipoivamia kagera na kuichukua baadaye angelibadilisha jina Uganda akaiita Kaugandania ikiwemo kagera , wewe ungaliita huo ni muungano ??
....na Karume alipinduwa serikali halali na aka commit genocide atrocity
 
Mjipange sana .....muungano huu hamuuwezi ......kuuvunja sio rahisi kama unavyodani ndugu yangu.fikirieni sana hili. Msitumie dini kuuvuruga muungano
Mimi ni Mtanganyika damu nikiutafakari huu muungano ni sawa na Mtu mlie kubaliana muuwe mama zenu! Mimi nikamuua mama yangu Tanganyika baadaye Niligundua mama yake (Zanzibar) akamficha nikamwambia hapa kuna options. Uue mama yako zenj ili woote tuwe wakiwa ima nimfufue mama yangu Tg ili wote tuwe na mama zetu! Nilipata jibu la kusikitisha aliye kufa kafa hakuna kumfufua na mama yangu sumuui ng"oo wee ulie tu Jitambue Mtg Kuhusu deen Mimi ni Mkristo mujahidina kindaki ndaki kila siku Natamka kwa kinywa changu "HAKUNA MUNGU APASWAYE KUABUDIWA KWA HAQI ILA YESU NA PAULO MTUME WAKE " Pia Namuomba Yesu Unisamehe Uovu wangu lakini SITAKUKANA
 
1. Uhamiaji- kitambulisho cha mkaazi
2. Kuna Balozi rasmi kadhaa hapo Unguja. Naibu wa Waziri (nje) ni lazima awe mzanzibari
3. Current !??
4. Banks (ipo Banki ya watu wa Zinjibar)
5. Economics - utalii na uvuvi na uchuuzi
6. Natural resources, sheria ya mafuta ilibadilishwa mafuta yote yapo chini ya mamlaka yao
7. Nationality - Uzanzibari na Uzanzibara
8. Politics - CUF, CCM, Chadema, ACT, UPD, chauma
9. TAX - ZRB (Zanzibar revenue authority)
UKIJA KUJUA MAANA YA MAMLAKA KAMILI, UTAACHA KUOKOTA HIZI MASHUDU MITAANI
 
Sisi tunataka huduma za kijamii, kuboreshewa afya, elimu, n.k , habari ya muungano wa tz unatusaidia nini???????

Hizo huduma ziboroshwe kwenye nchi gani? kama jibu ni Tanzania, labda ungelijiuliza Tanzania ni nini hasa halafu rudi hapa useme muungani wa tz unakuhusu nini?
 
hakuna aliyefikiria kugawanyika kwa soviet union, ethiopia, sudan etc.time will tell
....kwahiyo unakesha usiku na mchana nchi igawanyike !? Usiogope siku ukisikia na Walemba nao wanaomba Pemba isiwe sehemu ya Unguja. Kwanza Mpemba huwa hampigii kura Muunguja. Tusubiri tuone Jamhuri ya Pemba.
 
Back
Top Bottom