MamaSamia2025
JF-Expert Member
- Mar 29, 2012
- 10,143
- 22,111
Mwaka huu nimetokea kuvutiwa na siasa za Zambia na kuamua kufuatilia mambo kadhaa kupitia mitandao ya kijamii. Kuna jambo limetokea siku za hivi karibuni ambalo limenishangaza sana na ni somo kubwa sana kwa siasa za Tanzania na mhimili wa mahakama.
Wote tunakumbuka uchaguzi wa wenzetu ulifanyika mwezi wa nane ambapo baada ya matokeo kukatokea washindani ambao waliona uchaguzi haukuwa huru na wa haki waliamua kwenda mahakamani kudai haki. Hilo sio jambo la kushangaza kwasababu hata hapa kwetu kila baada ya uchaguzi kuna kesi hufunguliwa kupinga matokeo.
Kinachoshangaza ni kwamba chini ya mitatu tangu kesi kufunguliwa tayari mahakama za Zambia zimeshatoa hukumu ya hizo kesi. Wabunge watano hadi leo tayari wamepata pigo ya ushindi wao kubatilishwa na mahakama. Wabunge hao na majimbo yao ni;
1. Bowman Lusambo - Kabushi
2. Joseph Malanji - Kwacha
3. Mutotwe Kafwaya - Lunte
4. Sibongile Mwamba - Kasama Central
5. Lukas Simumba - Nakonde.
Binafsi kilichonishangaza zaidi ni wabunge hao kupokea maamuzi ya mahakama kwa heshima bila kutoa maneno ya kuudhi dhidi ya mahakama kama ilivyo kwa CHADEMA hapa Tanzania.
Wanasiasa na Mahakama zina kujifunza toka kwa wenzetu. Kesi zichukue muda mfupi na pia wanasiasa hasa wa upinzani waziheshimu mahakama.
Wote tunakumbuka uchaguzi wa wenzetu ulifanyika mwezi wa nane ambapo baada ya matokeo kukatokea washindani ambao waliona uchaguzi haukuwa huru na wa haki waliamua kwenda mahakamani kudai haki. Hilo sio jambo la kushangaza kwasababu hata hapa kwetu kila baada ya uchaguzi kuna kesi hufunguliwa kupinga matokeo.
Kinachoshangaza ni kwamba chini ya mitatu tangu kesi kufunguliwa tayari mahakama za Zambia zimeshatoa hukumu ya hizo kesi. Wabunge watano hadi leo tayari wamepata pigo ya ushindi wao kubatilishwa na mahakama. Wabunge hao na majimbo yao ni;
1. Bowman Lusambo - Kabushi
2. Joseph Malanji - Kwacha
3. Mutotwe Kafwaya - Lunte
4. Sibongile Mwamba - Kasama Central
5. Lukas Simumba - Nakonde.
Binafsi kilichonishangaza zaidi ni wabunge hao kupokea maamuzi ya mahakama kwa heshima bila kutoa maneno ya kuudhi dhidi ya mahakama kama ilivyo kwa CHADEMA hapa Tanzania.
Wanasiasa na Mahakama zina kujifunza toka kwa wenzetu. Kesi zichukue muda mfupi na pia wanasiasa hasa wa upinzani waziheshimu mahakama.