Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,316
- 33,112
KIONGOZI wa chama cha kisiasa cha DP, Christopher Mtikila anakabiliwa na hatari ya kufungwa jela baada ya mahakama kuamua kuwa iwapo zoezi la kuuza mali za mchungaji huyo ili kufidia deni la Sh8.8 milioni litashindikana, ombi la kumfunga litazingatiwa.
Awali Mahakama ya Wilaya ya Ilala ilikuwa imeamua kuwa nyumba ya mchungaji huyo iliyo Mikocheni jijini Dar es salaam iuzwe ili kufidia deni hilo, lakini Hakimu Hakimu Afumwisye Kibona jana alisitisha uamuzi huo na kuagiza mali zake nyingine ziuzwe kufanikisha malipo ya deni hilo.
Mtikila na mwenzake Mariam Issa wanadaiwa zaidi ya Sh8 milioni na Pascazia Matete ambaye anadai aliwakopesha wawili hao kwa ajili ya kufanyia biashara. Matete alishinda kesi namba 78 ya mwaka 2008 aliyoifungua katika Mahakama ya Mwanzo ya Kariakoo mbele ya Hakimu Benjamin Mwakasonda.
Akitoa amri hiyo, Hakimu Kibona alisisitiza kuwa iwapo ombi hilo la kutafuta mali mbadala za Mtikila ziuzwe kwa ajili ya kulipa deni hilo halitafanikiwa, ombi la kumfunga jela litafuatia. Alisema uamuzi huo wa kumfunga au kutomfunga utatolewa Machi 18 na Hakimu Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Ilala, Joyce Minde.
Hatua hiyo ilifikiwa jana baada ya Matete kuomba mahakama iamuru nyumba ya Mtikila yenye namba MKC/MCB 1135 iliyo kwenye kiwanja namba 237, Kitalu C Mikocheni ambayo ni mali ya Mwenyekiti huyo iuzwe ili alipwe deni lake.
Matete alifungua kesi hiyo katika Mahakama ya Mwanzo ya Kariakoo na baadaye Mtikila kufanikiwa kuiahamishia Mahakama ya Wilaya ya Ilala kutoka na kutoridhika. Pamoja na kesi hiyo kuhamishiwa Ilala, Matete alishinda kutokana na Mchungaji Mtikila kutofika mahakamani.
Hata hivyo, ombi la kuuza nyumba hiyo lilishindikana baada ya kampuni ya kimataifa ya Cielmac kuwasilisha pingamizi ikieleza kuwa ilishanunua nyumba hiyo kwenye mnada uliofanywa na benki ya NBC baada ya Mtikila kushindwa kurejesha mkopo wa Sh15 milioni aliouchukua katika benki hiyo. Pingamizi hilo lilikuja wakati kampuni ya Comrade Auction Mart Court Brokes ikiwa imeshatangaza kuwa itaiuza nyumba hiyo kwenye kwenye mnada uliopangwa kufanyika Februari 6 mwaka huu.
http://www.mwananchi.co.tz/newsrids.asp?id=18346
Awali Mahakama ya Wilaya ya Ilala ilikuwa imeamua kuwa nyumba ya mchungaji huyo iliyo Mikocheni jijini Dar es salaam iuzwe ili kufidia deni hilo, lakini Hakimu Hakimu Afumwisye Kibona jana alisitisha uamuzi huo na kuagiza mali zake nyingine ziuzwe kufanikisha malipo ya deni hilo.
Mtikila na mwenzake Mariam Issa wanadaiwa zaidi ya Sh8 milioni na Pascazia Matete ambaye anadai aliwakopesha wawili hao kwa ajili ya kufanyia biashara. Matete alishinda kesi namba 78 ya mwaka 2008 aliyoifungua katika Mahakama ya Mwanzo ya Kariakoo mbele ya Hakimu Benjamin Mwakasonda.
Akitoa amri hiyo, Hakimu Kibona alisisitiza kuwa iwapo ombi hilo la kutafuta mali mbadala za Mtikila ziuzwe kwa ajili ya kulipa deni hilo halitafanikiwa, ombi la kumfunga jela litafuatia. Alisema uamuzi huo wa kumfunga au kutomfunga utatolewa Machi 18 na Hakimu Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Ilala, Joyce Minde.
Hatua hiyo ilifikiwa jana baada ya Matete kuomba mahakama iamuru nyumba ya Mtikila yenye namba MKC/MCB 1135 iliyo kwenye kiwanja namba 237, Kitalu C Mikocheni ambayo ni mali ya Mwenyekiti huyo iuzwe ili alipwe deni lake.
Matete alifungua kesi hiyo katika Mahakama ya Mwanzo ya Kariakoo na baadaye Mtikila kufanikiwa kuiahamishia Mahakama ya Wilaya ya Ilala kutoka na kutoridhika. Pamoja na kesi hiyo kuhamishiwa Ilala, Matete alishinda kutokana na Mchungaji Mtikila kutofika mahakamani.
Hata hivyo, ombi la kuuza nyumba hiyo lilishindikana baada ya kampuni ya kimataifa ya Cielmac kuwasilisha pingamizi ikieleza kuwa ilishanunua nyumba hiyo kwenye mnada uliofanywa na benki ya NBC baada ya Mtikila kushindwa kurejesha mkopo wa Sh15 milioni aliouchukua katika benki hiyo. Pingamizi hilo lilikuja wakati kampuni ya Comrade Auction Mart Court Brokes ikiwa imeshatangaza kuwa itaiuza nyumba hiyo kwenye kwenye mnada uliopangwa kufanyika Februari 6 mwaka huu.
http://www.mwananchi.co.tz/newsrids.asp?id=18346