Leo Tarehe 28/2/2019 Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala Kuu ya Dar es salaam Mbele ya Mheshimiwa Jaji Stephen Magoiga, imetoa uamuzi wa kuzuia kufanyika kwa Mkutano Mkuu wa Chama cha Wananchi CUF uliopangwa na upande unaomuunga Mwenyekiti wa chama hicho Prof. Ibrahim Lipumba.
Uamuzi huo wa Mahakama Kuu unatokana na shauri Na. 248 la mwaka 2018 lililofunguliwa kwa pamoja na Manaibu Katibu Wakuu Mhe. Joran Lwehabura Bashange (Tanzania Bara) na Mhe. Nassor Ahmed Mazrui (Zanzibar) chini ya mawakili wa Chama hicho waheshimiwa Juma Nassoro Dovutwa, Daimu Halfani na Loveness Denis.
Hili ni pigo la pili kwa kambi hiyo ya Mwenyekiti baada ya wiki iliyopita Mahakama Kuu kuifuta bodi yake ya wadhamini kupitia shauri Na.13 la mwaka 2017 lililofunguliwa na Mhe. Ally Saleh (Mbunge) dhidi ya RITA na wengine 17.
Katika uamuzi wake Mhe. Jaji Magoiga amesema, mahakama imejiridhisha kuwa kwa kutolewa zuio hilo wadaiwa (Respondents) hawatadhurika chochote, lakini kinyume chake zuio lisipotolewa waleta maombi (Applicants) watapata madhara makubwa ikiwemo kufukuzwa uongozi, uanachama wao na hivyo kukosa haki zao za msingi za kikatiba.
Mahakama imepanga shauri Na. 284 la mwaka 2018 liitwe Tarehe 3/4/2019 kwa ajili ya usikilizwaji wa awaji (Pre trial conference).
Uamuzi huo wa Mahakama Kuu unatokana na shauri Na. 248 la mwaka 2018 lililofunguliwa kwa pamoja na Manaibu Katibu Wakuu Mhe. Joran Lwehabura Bashange (Tanzania Bara) na Mhe. Nassor Ahmed Mazrui (Zanzibar) chini ya mawakili wa Chama hicho waheshimiwa Juma Nassoro Dovutwa, Daimu Halfani na Loveness Denis.
Hili ni pigo la pili kwa kambi hiyo ya Mwenyekiti baada ya wiki iliyopita Mahakama Kuu kuifuta bodi yake ya wadhamini kupitia shauri Na.13 la mwaka 2017 lililofunguliwa na Mhe. Ally Saleh (Mbunge) dhidi ya RITA na wengine 17.
Katika uamuzi wake Mhe. Jaji Magoiga amesema, mahakama imejiridhisha kuwa kwa kutolewa zuio hilo wadaiwa (Respondents) hawatadhurika chochote, lakini kinyume chake zuio lisipotolewa waleta maombi (Applicants) watapata madhara makubwa ikiwemo kufukuzwa uongozi, uanachama wao na hivyo kukosa haki zao za msingi za kikatiba.
Mahakama imepanga shauri Na. 284 la mwaka 2018 liitwe Tarehe 3/4/2019 kwa ajili ya usikilizwaji wa awaji (Pre trial conference).