This shows that the Judiciary is trying to hold its muscles and seek its independence. But why after 10 years? Just Delayed is justice denied! Mama Tibaijuka sasa waweza rudi kuendesha chombo ulichokianzisha.
Na Claud Mshana
MAHAKAMA Kuu imetengua uamuzi wa serikali kulifungia lililokuwa Baraza la Wanawake Tanzania (Bawata) na kwamba chombo hicho sasa kitaendela kuwepo na kufanya shughuli zake kisheria.
Wakitoa hukumu hiyo, majaji watatu wa mahakama hiyo, Lauren Kalegeya, Juxon Lay na Amir Manento walisema Bawata bado inatambulika kisheria na kuongeza kuwa ipo katika katika orodha ya msajili kwa kipindi chote cha miaka 13 ya kusikilizwa kesi hiyo.
Pamoja na kutangaza uamuzi huo, mahakama hiyo pia imelipa Sh20 milioni kwa baraza hilo kama fidia ya jumla.
Mwaka 1997, serikali iliishutumu Bawata kuwa inajihisisha na shughuli za siasa na hivyo kutaka ijisajili upya ili ifanye kazi na malengo inayokusudia.
Kufungiwa kwa Bawata kulisababisha malalamiko mengi sana kwa wadau wa haki za binadamu, waliodai kuwa serikali haikufuta haki na kwamba chombo hicho hakikupewa haki ya kusikilizwa.
Mara baada ya uamuzi huo wa Mahakama Kuu, wakili aliyekuwa akiitetea Bawata ambaye pia ni mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Prof Issa Shivji alisema watu wanapaswa kuwa na imani na mahakama zetu.
"Ninafurahi hasa jinsi kesi nzima ilivyoendeshwa, jinsi vipengele mbalimbali vya sheria vilivyotafsiriwa. Hii inaonyesha ni jinsi gani mahakama zetu zilivyo mstari wa mbele katika kutetea na kulinda haki za binadamu," alisema Prof. Shivji.
Bawata iliundwa mwaka 1994 ikiwa na lengo la kuwaunganisha wanawake wa aina zote kupigania usawa wa kijinsia hasa katika mfumo wa vyama vingi nchini.
Source: Mwananchi
Na Claud Mshana
MAHAKAMA Kuu imetengua uamuzi wa serikali kulifungia lililokuwa Baraza la Wanawake Tanzania (Bawata) na kwamba chombo hicho sasa kitaendela kuwepo na kufanya shughuli zake kisheria.
Wakitoa hukumu hiyo, majaji watatu wa mahakama hiyo, Lauren Kalegeya, Juxon Lay na Amir Manento walisema Bawata bado inatambulika kisheria na kuongeza kuwa ipo katika katika orodha ya msajili kwa kipindi chote cha miaka 13 ya kusikilizwa kesi hiyo.
Pamoja na kutangaza uamuzi huo, mahakama hiyo pia imelipa Sh20 milioni kwa baraza hilo kama fidia ya jumla.
Mwaka 1997, serikali iliishutumu Bawata kuwa inajihisisha na shughuli za siasa na hivyo kutaka ijisajili upya ili ifanye kazi na malengo inayokusudia.
Kufungiwa kwa Bawata kulisababisha malalamiko mengi sana kwa wadau wa haki za binadamu, waliodai kuwa serikali haikufuta haki na kwamba chombo hicho hakikupewa haki ya kusikilizwa.
Mara baada ya uamuzi huo wa Mahakama Kuu, wakili aliyekuwa akiitetea Bawata ambaye pia ni mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Prof Issa Shivji alisema watu wanapaswa kuwa na imani na mahakama zetu.
"Ninafurahi hasa jinsi kesi nzima ilivyoendeshwa, jinsi vipengele mbalimbali vya sheria vilivyotafsiriwa. Hii inaonyesha ni jinsi gani mahakama zetu zilivyo mstari wa mbele katika kutetea na kulinda haki za binadamu," alisema Prof. Shivji.
Bawata iliundwa mwaka 1994 ikiwa na lengo la kuwaunganisha wanawake wa aina zote kupigania usawa wa kijinsia hasa katika mfumo wa vyama vingi nchini.
Source: Mwananchi