Mahakama Kuu yaamuru madaktari kusitisha mgomo

Waziri mponda mbishi, anasema mbona waziri wa ulinzi na JKT ameshakutwa na mabalaa mara nying tu, yakiwemo ya gongolamboto na mbagala, pia waziri wa mambo ya ndani, polis wake wanaua raia kila kukicha, yeye kutofautiana na madaktar imekuwa nongwa!

Tupe chanzo cha taarifa yako.
 
Uliandika vizuri sana lakini sentensi yako ya mwisho imechafua maana nzima, nimekudharau sana! hivi nchi hii yenye wakaazi zaidi ya milion 44 haina watu wengine wanoweza uongozi zaidi ya kutegemea mafisadi walishindwa kuongoza wakalazimishwa kujiuzulu, mbona kuna vijana wengi tu wenye uwezo na upeo na makini wasio na chembe za ufisadi na wizi?? Think twice before you put your rubbish here!!

Queen kyusa like this
 
Kama wameamua kuzama na meli maboya wanalilia ya nini?.....Ukipewa uchaguzi, chagua vizuri usifuate mkumbo...
 
Watu wanakufa, kisa, wacheza mieleka wawili wanatunishiana misuli. HAIKUBALIKI.

Sasa Jaji wa Mahakama kuu, kitengo cha kazi, katoa AMRI, Madaktari wote warudi kazini kama kawaida, tena na wale wliotumia vyombo vya habari kutangazia mgomo, wanatakiwa warudi tena kwenye vyombo vilevile wakatangaze kusitisha mgomo, la sivyo...

Haya sie yetu macho tunaangalia hii mechi itaishaje?
 
Nadhani wanasheria watujuze hii kitu imekaaje.Maana hata mie nimesikia kuwa mahakama imewataka madokta kuacha mgomo mara moja..na wamekitaka MAT na Jumuiya ya madaktari kuwatangazia madokta kuwa wamesitisha mgomo kama ambavyo waliwatangazia mara ya kwanza kwenye vyombo vya habari..Nadhani tusipuuze hili tamko,tungepata tafsiri ya kisheria ya agizo hili ingekuwa mujarabu zaidi.
 
sasa ukisikia tunaishi maisha ya vichekesho ndio haya.....na leo Mh. nasikia ataongea tena na wazee wa Dar es salaam, subirinin mitusi sasa
 
Huyu aliyeleta hii topic ametumwa atest zali kama wakiingia na hiyo singo ya mahakama, madaktari watakuwa wamejipangaje?

Madaktari na nyie kama hamjajipanga na hili, hakikisheni mnakuwa hatua mbele yao. Watafuteni watu kama kina Tundu Lisu wasiohongeka ili wawashauri.

Kwenye red hapo.......... mitaani wanasema mgomo una mkono wa wanasiasa wa Chama Cha Maandamano. chunga kauli zako.
 
this government ain't serious at all...the only open and easy solution to this matter iz to suck mponda na nkya, and not to use mahakama to intimidate doctors. very silly
 
NANUKUU...
mahakama kuu kitengo cha kazi imewaamuru Madaktari kurudi kazini mara moja na kutoa ufafanuzi kuwa majadiliano ya haraka yanatakiwa kufanyika kati ya upande wa serikali na upande wa madaktari ili kuweza kumaliza tofauti zilizopo...
MWISHO WA KUNUKUU...

Tamko la mahakama kama ndio hilo ni zuri.
 
Umeona hee gwalu niaje lakini!
kwa hapa ilipofikia ni kuwa serikali imeshindwa kufanya maamuzi pamoja na kutimiza majukumu yake.

Kwa hiyo ijiuzuli yote ili nchi iwe chini ya Jaji Mkuu (kwa maana ndio wanaweza kutoa maamuzi) wakati tukiangalia jinsi ya kutatua matatizo mengine!

 
Huyo mwanasheria mkuu wa serikali na mahakama yake ni kama wanatingisha kibiriti!!! Unamtishia mtu mzima nyau?
 
this government ain't serious at all...the only open and easy solution to this matter iz to suck mponda na nkya, and not to use mahakama to intimidate doctors. very silly
"mende Kaangusha kabati"
Madr.wakikomaa hiili ndilo litakua anguko la serikali,maana kama nguvu kubwa utatumika na madr. kugoma kurudi kazini serikali itakua imeprove failure.Ikumbukwe jaribio la kwanza la waziri mkuu kuwatishia lilishindikana,tunasubiri hili la pili litakuwaje.Lakini madr, wakumbuke kwamba "penye mwamba mgumu ndio penye mafuta"wakishinda na hili wanaelekea kunako mafanikio.Mafanikio hayapatikani kwa lelemama.
 
kinachonitisha hasa ni kuwa suala hli ambalo kwa kweli ni la kisiasa lingeweza kumalizwa nje ya mahakama. Kuiingiza mahakama kwenye hili ni kutaka kuleta matatizo kwa mahakama vile vile. Hivi, madaktari wakiamua kudharau amri hiyo ya mahakama kwa sababu wanaamini siyo halali nini kitafanyika? Well, inaweza kuwasaidia serikali kufanya mambo fulani fulani "kwa sababu madaktari wamekataa amri halali ya mahakama" lakini haiwezi kufanya serikali ionekane kuwa inahoja. Kwa kukimbiliaa mahakamani imeonesha tu kuwa serikali imeshindwa hoja ya kushawishi.

Ndio uzuri mmoja wa migomo kama hii kwani hapa POlisi au FFU hawawezi kutumika. Hawawezi kwenda kwenye nyumba za madaktari na kuwaburua kwenda hospitali! Hawawezi kutumia vikosi vya jeshi kuwalazimisha madaktari kuandika tiba na kufanya uchunguzi. Njia pekee ni kuwashawishi. Sasa hata tukiassume kuwa madaktari - technically - wanarudi kazini kutii amri ya mahakama je mahakama inaweza kuwalazimisha kufanya kazi? Itakuwaje kama madaktari wote as strategic move wanaamua kurudi kazini lakini hawafanyi kazi mahakama itawaagiza nini "watibu"?

Mahakamani ndio ambapo haki huwa inapatikana, sasa madaktari nao waende wakapambane kisheria ndio tuone uhalali wa madai yao. Si wote serikali na madaktari wapo chini ya katiba ya jamhuri?

Wakirudi kama hawafanyi kazi kuna hatua za mahala pa kazi ambazo zinaweza kuchukuliwa.
 
Hii mahakama ya ccm ilikuwa wapi kipindi kile cha mgomo wa wauza mafuta? Hakuna marefu yasiyo na ncha, serikali ya ccm imekuwa inatumia vyombo vya dola kukandamiza wananchi, sasa wameshikwa pabaya. Utamlamishaje daktari kutibu? Utamshikilia sindano?

Lakini ni kwanini serikali inatumia nguvu kubwa sana kuwahifadhi watu wawili na kutesa watu milioni 40? Scandal ya vipimo vya ukimwi ilitosha kabisa kuwatosa wawili hawa lakini bado wako ofisini!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom