Mahakama Kuu ya Tanzania kuzuia malipo kwa DOWANS?

Mmeongea mengi sana, tena yenye busara, lakini mwisho wa mchezo ni 90 mins, kipenga cha mwisho. Hapo ndo tutajua kuwa nani kaliwa, wananchi kama kawaida au wenye nchi.
 
Pamoja na kwenda ICC, The Arbitration Act inasema kuwa Mahakama ya Tanzania ndiyo yenye uamuzi wa mwisho iwapo maamuzi ya ICC yatekelezwe au la. Hivyo mwenye final say kwenye hili jambo ni the High Court of Tanzania na si ICC kwani ruling ya ICC lazima iwe registered kwenye Mahakama Kuu ya Tanzania na mahakama iseme kama malipo haya ni halali au siyo halali na kuyakataa. Kama ilivyokuwa quoted kwenye hii habari ya THISDAY, sheria ya Tanzania inasema:

"Where an arbitrator or umpire has misconducted himself or an arbitration or award has been improperly procured, the court may set aside the award."

Tuombe iwe hivyo!!!
 
Ni sahihi kabisa, arbitration contract na ICC ruling vyenyewe vinatambua kuwa ili hukumu ya ICC iweze kuwa enforced, ni lazima isimamiwe na itafsiriwe kwa mujibu wa sheria za Tanzania. Hii ina maana kuwa Mahakama Kuu ya Tanzania kwa kutumia The Arbitration Act inaweza kabisa bila wasiwasi wowote kuitupilia mbali hukumu ya ICC kwa hoja mbalimbali ikiwemo kuwa hukumu ya ICC inapingana moja kwa moja na sheria ya Tanzania ya PPA ya 2004 au hata on moral grounds kama ulivyosema.

Tatizo ni kuwa kuna nguvu kubwa sana za kifisadi ndani ya serikali, miongoni mwa wanasiasa (wakiwemo hata wa upinzani) na humu JF kutaka kulazimisha malipo kwa Dowans kwa hoja potofu kuwa maamuzi ya ICC ni final, mali za Tanzania nje zinaweza kupigwa mnada, we messed up we must pay up, etc.

Ukweli ni kuwa Mahakama Kuu ya Tanzania ina uwezo, mamlaka na kila sababu ya kutupilia mbali hukumu ya ICC kwani ICC judges erred in their interpretation of Tanzania's PPA Act of 2004. No one is better placed to declare the correct interpretation ya sheria hii kuliko Mahakama Kuu ya Tanzania.

Hapa ndipo unapochanganya vitu tena. Mahakama Kuu ya Tanzania haina mamlaka ya ku-set aside award ya ICC. Unachotaka kushinikiza wafanye ndicho kinachotoa credence kwa mashirika/makampuni ya nje kukataa dispute resolution kuwa governed na sheria za Tanzania. Mahakama Kuu mamlaka yake yanaishia kwenye mipaka ya Tanzania wakati mamlaka ya ICC yameenea kwenye nchi zote ambazo ni signatories wa New York Convention ya 1958. Mahakama yetu ikiingilia uamuzi huo, Dowans watakuwa bado wana uwezo wa kwenda kwenye nchi nyingine ambako Tanzania ina assets na kudai ziwe seized ili kutimiza award. Tusidhanie kuwa the only recourse ya ku-enforce award hii ni judicial system ya Tanzania. Tutakuwa tunajidanganya na mwisho wa siku tutalipa kuliko hiki tunachotaka kukataa.

Amandla.......
 
Hapa ndipo unapochanganya vitu tena. Mahakama Kuu ya Tanzania haina mamlaka ya ku-set aside award ya ICC. Unachotaka kushinikiza wafanye ndicho kinachotoa credence kwa mashirika/makampuni ya nje kukataa dispute resolution kuwa governed na sheria za Tanzania. Mahakama Kuu mamlaka yake yanaishia kwenye mipaka ya Tanzania wakati mamlaka ya ICC yameenea kwenye nchi zote ambazo ni signatories wa New York Convention ya 1958. Mahakama yetu ikiingilia uamuzi huo, Dowans watakuwa bado wana uwezo wa kwenda kwenye nchi nyingine ambako Tanzania ina assets na kudai ziwe seized ili kutimiza award. Tusidhanie kuwa the only recourse ya ku-enforce award hii ni judicial system ya Tanzania. Tutakuwa tunajidanganya na mwisho wa siku tutalipa kuliko hiki tunachotaka kukataa.

Amandla.......

Ulazima wa kutaka ruling ya ICC ipate blessing ya Mahakama Kuu ya Tanzania maana yake ni kuwa hukumu hii haina meno na haiwezi kuwa enforced mpaka Mahakama Kuu ya Tanzania ikubali. Vinginevyo wangeenda kuikazia hii hukumu Costa Rica, New York, Paris au Iran.

Endeleeni kujaribu kupotosha mambo, lakini ukweli unabaki pale pale. Mwenye final say kuhusu kutekelezwa kwa hukumu ya ICC ni Mahakama Kuu ya Tanzania na ina mamlaka ya kuitupilia mbali hukumu hii.

Ni uzushi na fear mongering kusema mali za Tanzania nje zinaweza kukamatwa. SI KWELI. Tanesco inajitegemea kama shirika linaloweza kushitaki na kushitakiwa, huwezi kukamata mali za serikali.

Kukamata assets za serikali nje itakuwa ni kama wewe Fundi Mchundo uishitaki Tanzania Ports Authority (TPA) kwa kuwa kontena lako limepotea bandarini halafu mahakama itoe hukumu kuwa TPA ikulipe sh milioni 200 kwa mfano. TPA ikikaidi kukulipa au ikasema haina pesa, je unaweza kwenda kuikamata shangingi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar kwa vile ni mali ya serikali na kusema unaipiga mnada ili kufidia deni lako na TPA?

Tusitake kudanganyana bure hapa.
 
Iyo ela itasaidia CCM kurecover from the billions of money spent kwa election
You said it ALL!

Kinachotusumbua hapa ni CCM na wala si RA na EL, hawa ni wakopeshaji wa CCM tunawajua na wanataka pesa yao halali na faida kutoka CCM. Sidhani CCM inachochote cha kung'ang'aniwa na hawa Jamaa, wanajua wanapata faida kwa kuikopesha CCM.
Huu ndiyo umafia wa CCM bwana, tumewsikia wanakati cost maana matumizi ya uchaguzi wa 2010 yalizidi unga. Nadhani wakubwa ambao huponea kwenye uchaguzi mwaka huu ngoma ilikuwa ngumu maana pesa zote zimetumika kwenye mabango ya JK na kuwahonga walalahoi. Sasa wanataka hizi pesa kwa udi na uvumba, wako tayari kumnyamazisha mtu yoyote kwenye hili dili. Mwenye suluhisho la kutolipa hizi pesa ni Watanzania wakiongozwa na wanaharakati na vyama vya upinzani. Kinyme na hapo pesa hii lazima itachukuliwa tu. Bila Bonge la mgomo na maandamano mambo hayatabadilika. Wanaangalia upepo na reaction ya Wtz. Yangu macho kama tukikomaa Pesa hatoki!
CCM huamgalia upepo tu , tukizubaa tumeliwa!
 
Under Section 66 of the 1996 Act, the court's permission is required for an international arbitral award
to be enforced in the UK. Once the court has given permission, judgment may be entered in terms of the arbitral award and enforced in the same manner as a court judgment or order.​
Permission will not be granted by the court if the party against whom enforcement is sought can show that

(a) the tribunal lacked substantive jurisdiction and
(b) the right to raise such an objection has not been lost.

New York Convention 1958 Arbitral Awards​
An arbitral award will be made under the New York Convention if it is made pursuant to an arbitration agreement in the territory of a state which is a party to the New York Convention - see Appendix 1 for a list of the contracting states to the New York Convention1.

An award is treated as being made at the seat of the arbitration in spite of where it was signed, sent from or delivered to. For example, if an award is made in Paris, the seat of the award is France. France is a party to the New York Convention and the award can therefore be enforced internationally as a New York Convention award.

Under section 101 of the Arbitration Act 1996, an award subject to the New York Convention is recognised as binding between the parties and with the court's permission can be enforced in England and Wales in the same manner as a judgment or court order.

The procedure to apply for enforcement is the same as section 66 of the Arbitration Act 1996.

Recognition or enforcement of an award can be refused under section 103 (2) of the Arbitration Act 1996, if it is proved that:

(a) a party to the arbitration agreement under the law applicable to him, was under some incapacity;
(b) the arbitration agreement was not valid under the law to which the parties subjected it or, failing any indication thereon, under the law of the country where the award was made;
(c) the defendant was not given proper notice of the appointment of the arbitrator or the arbitration
proceedings or was otherwise unable to present its case;
(d) the award deals with an issue not contemplated by or not falling within the terms of the
submission to arbitration or contains decisions on matters beyond the scope of the submission to
arbitration;
(e) the composition of the arbitral tribunal or the arbitral procedure was not in accordance with the

agreement of the parties or, failing such
 
Ulazima wa kutaka ruling ya ICC ipate blessing ya Mahakama Kuu ya Tanzania maana yake ni kuwa hukumu hii haina meno na haiwezi kuwa enforced mpaka Mahakama Kuu ya Tanzania ikubali. Vinginevyo wangeenda kuikazia hii hukumu Costa Rica, New York, Paris au Iran.

Endeleeni kujaribu kupotosha mambo, lakini ukweli unabaki pale pale. Mwenye final say kuhusu kutekelezwa kwa hukumu ya ICC ni Mahakama Kuu ya Tanzania na ina mamlaka ya kuitupilia mbali hukumu hii.

Ni uzushi na fear mongering kusema mali za Tanzania nje zinaweza kukamatwa. SI KWELI. Tanesco inajitegemea kama shirika linaloweza kushitaki na kushitakiwa, huwezi kukamata mali za serikali.

Kukamata assets za serikali nje itakuwa ni kama wewe Fundi Mchundo uishitaki Tanzania Ports Authority (TPA) kwa kuwa kontena lako limepotea bandarini halafu mahakama itoe hukumu kuwa TPA ikulipe sh milioni 200 kwa mfano. TPA ikikaidi kukulipa au ikasema haina pesa, je unaweza kwenda kuikamata shangingi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar kwa vile ni mali ya serikali na kusema unaipiga mnada ili kufidia deni lako na TPA?

Tusitake kudanganyana bure hapa.

Uongo tena. Ingekuwa award haiwi enforced mpaka Mahakama ya nchi husika ikubali basi hakuna ambaye angekubali kupoteza muda kwenda Paris wakati mwisho wa siku maamuzi yote yatafanyika Kivukoni. Hii imeletwa Tanzania kwa registration na primary enforcement kwa sababu ni hapa ndipo mkataba uliingiwa na mdaiwa ana makao makuu yake. Recourse ya kwenda Costa Rica, New York, Paris au Iran ipo kama Mahakama Kuu itaonekana inataka upindisha maamuzi ya ICC. Ni uzushi kudai kuwa Mahakama Kuu ya Tanzania ina uwezo wa ku-set aside award ya ICC. Ni kama vile kusema kuwa Mahakama Kuu yetu inaweza ku-set aside hukumu iliyotelewa na International Criminal Court. Tutaweza kujibalaghua humu mwetu lakini vyombo hivi ni pan-territorial, watatubana kwengine. Dowans ana haki ya ku-submit maombi ya enforcement kokote ambako nchi zake ni signatories wa New York convention.

Unazidi kupotosha. Hapo hatuzungumzii jurisdiction. TPA hawataomba Mahakama i-set aside hukumu kwa vile hawana uwezo wa kunilipa. Pamoja na wao kusema hivyo, nitakuwa na uwezo wa kwenda mahakamani na kuonyesha kuwa TPA wana assets ambazo zinashikika tofauti na wanavyosema. Mahakama itanipa mamlaka ya kuzishika sasa kwa nini nikamtafute Mkuu wa Mkoa?

Ni wewe unayetaka kutudanganya kwa kulazimisha hoja isio na mantik.

Amandla.......
 
August,

Mahakama ku inaweza kukataa ku-enforce award lakini haina maana kuwa ime-annul award yenyewe. Award inabaki pale pale na claimant kama anataka anaweza kwenda kwengine ku-omba enforcement. Mfano wa Bashir unaweza kutupa ufafanuzi wa ishu hii. ICC wametoa arrest warrant, akamatwe. Kisheria ICC hawana mamlaka ya ku-enforce warrant hiyo bali wanategemea mahakama za nchi zilizo wanachama kuisaidia kuitekeleza. Kwa maana hiyo, Mahakama ya Sudan ilitakiwa itoe amri Bashir akamatwe apelekwe The Hague kwa Pilato. Lakini wote tunajua hakuna hakimu au jaji wa Sudan ambaye anaweza kudiriki kufanya hivyo. Kwa hali Mahakama Kuu ya Sudan inaweza kukataa ku-enforce arrest warrant hiyo kwa kusema kuwa ilikuwa ni ya kisiasa bla bla. Nchi nyingine za Afrika zinaweza nazo kusema hivyo hivyo. Lakini kwa kufanya hazifuti arrest warrant hiyo kwa sababu hazina uwezo na mamlaka ya kufanya hivyo. Arrest warrant iko hai na Bashir anajua kuwa akilogwa kukanyaga paris, atakamatwa kwa sababu Mahakama za kule ziko tayari ku-enforce warrant hiyo.

Ndivyo ilivyo kwenye hili la wakina Dowans. Mahakama yetu inaweza kukataa kuamrisha award hiyo itekelezwe lakini haina uwezo wa kuifuta award yenyewe. Award itabaki hai na claimant atakuwa na haki ya kutafuta haki yake sehemu nyingine ambako Tanzania au Tanesco wana assets na mahakama zake ziko tayari ku-enforce maamuzi ya ICC. Kushauri kuwa tuvimbishe misuli ni kuwa myopic.

Amandla.....
 
Uongo tena. Ingekuwa award haiwi enforced mpaka Mahakama ya nchi husika ikubali basi hakuna ambaye angekubali kupoteza muda kwenda Paris wakati mwisho wa siku maamuzi yote yatafanyika Kivukoni. Hii imeletwa Tanzania kwa registration na primary enforcement kwa sababu ni hapa ndipo mkataba uliingiwa na mdaiwa ana makao makuu yake. Recourse ya kwenda Costa Rica, New York, Paris au Iran ipo kama Mahakama Kuu itaonekana inataka upindisha maamuzi ya ICC. Ni uzushi kudai kuwa Mahakama Kuu ya Tanzania ina uwezo wa ku-set aside award ya ICC. Ni kama vile kusema kuwa Mahakama Kuu yetu inaweza ku-set aside hukumu iliyotelewa na International Criminal Court. Tutaweza kujibalaghua humu mwetu lakini vyombo hivi ni pan-territorial, watatubana kwengine. Dowans ana haki ya ku-submit maombi ya enforcement kokote ambako nchi zake ni signatories wa New York convention.

Unazidi kupotosha. Hapo hatuzungumzii jurisdiction. TPA hawataomba Mahakama i-set aside hukumu kwa vile hawana uwezo wa kunilipa. Pamoja na wao kusema hivyo, nitakuwa na uwezo wa kwenda mahakamani na kuonyesha kuwa TPA wana assets ambazo zinashikika tofauti na wanavyosema. Mahakama itanipa mamlaka ya kuzishika sasa kwa nini nikamtafute Mkuu wa Mkoa?

Ni wewe unayetaka kutudanganya kwa kulazimisha hoja isio na mantik.

Amandla.......
refer to post niliyo weka juu au ukitaka kitu yote fuata hiyo link, uone maelezo umuhimu au ulazima ya hii kitu kuwa registered katika mahakama husika ili iwe enforceable case ya dowans sa costa rica vs tanesco itkuwa maakama ya tanzania au huko costa rica kwa sababu interested parties ndiko makazi yao.
 
refer to post niliyo weka juu au ukitaka kitu yote fuata hiyo link, uone maelezo umuhimu au ulazima ya hii kitu kuwa registered katika mahakama husika ili iwe enforceable case ya dowans sa costa rica vs tanesco itkuwa maakama ya tanzania au huko costa rica kwa sababu interested parties ndiko makazi yao.

An award is treated as being made at the seat of the arbitration in spite of where it was signed, sent from or delivered to. For example, if an award is made in Paris, the seat of the award is France. France is a party to the New York Convention and the award can therefore be enforced internationally as a New York Convention award.

Nimeangalia na nimeona hilo.

Amandla.....
 
Mimi kwa elimu yangu ndogo ya Sheria, katika kupitia hii Enforcing International Arbitration Awards in
England and Wales

1. Tanzania tumesaini International convention ipi amabyo ni relavant to this case

  • The New York Convention 1958
  • Geneva Convention 1927 arbitral awards
Nimeona kati ya vitu ambavyo vinaweza kuifanya award ikawa rejected na state husika ni hiki hapa chini.
Recognition or enforcement of an arbitral award mayalso be refused where it would be contrary to public
policy.



2. Lakini najaribu kujiuliza, je hakuna policy ya nchi iliyokiukwa kweli katika mkataba huu?

karibuni kujadili.
 
Hivi hawa wanasheria wa-Tanzania wanafanya nini???, hii sio issue ya mtu mmoja inabidi wote kuumiza vichwa ili tuweze kupata loopholes, am sure there is nothing like open and close case..... if you look hard enough lazima kuna kipengele kitapatikana cha kuweza kujinasua kwenye hii issue, au hawa jamaa hawawezi ku-work for free... mpaka wapelekewe kesi na mshiko??? Jamani hivi hakuna any patriotism??
Ndugu yangu wanasheria waliokuwa na patriotism ni wakina marehemu Ndyanabo na hawapo tena. Leo tumezalisha wanasheria wengi sana lakini?! Mmmhhh ni kama ni mafisadi tu pia. Wanatuingiza mikenge makusudi kwenye mikataba mibovu na wanashindwa kututetea kwenye shida kama hizi.TUMEKWISHA.
 
Kushauri kuwa tuvimbishe misuli ni kuwa myopic.

Amandla.....

kwahiyo in not so many words ni kwamba "we are done for", tumekwisha......, "no way out".....

Mi naona sasa tungeconcentrate kuwatafuta hao wahusika waliotufikisha hapa ili tutaifishe mali zao ziweze kulipia huu uozo. I am sure you cant tell me kwamba hata hao wahusika hatuwezi kuwapata au kuna kipengele kinachowalinda kwa kufanya huu uozo, and I mean kuwafunga jela haitoshi, hata wasipofungwa ila mali zao zipigwe mnada....
 
kwahiyo in not so many words ni kwamba "we are done for", tumekwisha......, "no way out".....

Mi naona sasa tungeconcentrate kuwatafuta hao wahusika waliotufikisha hapa ili tutaifishe mali zao ziweze kulipia huu uozo. I am sure you cant tell me kwamba hata hao wahusika hatuwezi kuwapata au kuna kipengele kinachowalinda kwa kufanya huu uozo, and I mean kuwafunga jela haitoshi, hata wasipofungwa ila mali zao zipigwe mnada....

Hiyo solution ya pili iko ndani ya uwezo wetu lakini sidhani kama kuna political will ya kuitekeleza. Ni rahisi zaidi kujifanya kupambana na adui aliye nje kuliko kushughulikia udhaifu wako. Hao wanaojiita wazalendo huu ulikuwa ndio wakati wa kuhoji tumefikaje hapo? Kwa nini tumeshindwa na tufanye nini ili tusijikute tena mahali kama hapa. Kama kuna uzembe, tuushughulikia. Kama kuna udhaifu katika utendaji tufanye capacity building ili technocrats wetu wawezekutushauri vyema safari ijayo maana mikataba bado tutaingia na makampuni ya nje.

Amandla.....
 

Rules of Arbitration

International Chamber of Commerce

International Court of Arbitration

Article 28
Notification, Deposit and Enforceability of the Award
1​
Once an Award has been made, the Secretariat shall notify to the parties the text signed by the Arbitral Tribunal, provided always that the costs of the arbitration have been fully paid to the ICC by the parties or by one of them.
2​
Additional copies certified true by the Secretary General shall be made available on request and at any time to the parties, but to no one else.
3​
By virtue of the notification made in accordance with Paragraph 1 of this Article, the parties waive any other form of notification or deposit on the part of the Arbitral Tribunal.
4​
An original of each Award made in accordance with the present Rules shall be deposited with the Secretariat.
5​
The Arbitral Tribunal and the Secretariat shall assist the parties in complying with whatever further formalities may be necessary.
6​
Every Award shall be binding on the parties. By submitting the dispute to arbitration under these Rules, the parties undertake to carry out any Award without delay and shall be deemed to have waived their right to any form of recourse insofar as such waiver can validly be made.
 
pamoja na sarakasi nyingi za kisheria kuonyesha nani yuko right in legal terms...............the reality ni kuwa kama Taifa TUNAIBIWA.............na hiyo ndio recourse yetu
 
pamoja na sarakasi nyingi za kisheria kuonyesha nani yuko right in legal terms...............the reality ni kuwa kama Taifa TUNAIBIWA.............na hiyo ndio recourse yetu

Viongozi na sisi wenyewe watanzania tumekosa uzalendo kwa nchi yetu! Kila mtu anaChukua Chake Mapema. Kuna baadhi ya nchi, huwezi kusikia madudu kama haya...watu 'wanaivuruga' mpaka Ikulu. Linapokuja suala la rushwa na ufisadi, natamani sana kama tungeiga kutoka China!
 
Sina utaalamu sana na sheria lakini kusoma ufafanuzi wa AwArd yenyewe kutoka kwenye kundi linaloonesha uko uwezekano wa ku-set aside ruling (Fareed & Co) na wale wanaoweka wazi kutokuwezekana kupingwa (Zitto & Co) kwa Award hii nagundua kitu kimoja.......

TANESCO wanajua mchezo woteeeee....................ila kwa sababu moja au nyingine, hawakuweka wazi mambo yote ICC ili kuwezesha ruling ya haki na award ambayo kwa vyovyote ingetu-favor watanzania-


Bado namnukuu mkuu mmoja wa Tanesco ALIEWAHI kunukuliwa na Raia Mwema aksiema kuwa watachukua hatua za kisheria dhidi ya hukumu hii na kama watashindwa juu ya hili basi wataweka wazi mambo yote. Na niliwahi kuhoji kwenye thread moja hapahapa jamvini kwa nini Tanesco wanaweka ukweli huu pembeni mpaka ruling yao ishindwe, kwa nini wasingeweka mapema wakati kesi iko ICC?? https://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/94391-nukuu-ya-raia-mwema-na-ujambazi-wa-watendaji-wetu.html

Lazima kuna namna iliofanyika na Tanesco wakakaa kimya na jamaa ndo wakaona loophole maana wenye ukweli wote wamepigwa gazi. Na kwa style hii hii bado tutashindwa tena. Cha muhimu ni Tanesco watutendeee haki kwa kutuambia watanzania kinagaubaga WHAT WAS AND, Yes of course, STILL IS BEHIND THE SCENE



TANESCO NYIE NDO MMESABABISHA YOTE, NA HATA MAHAKAMA KUU SIJUI NDIO IKI-SET ASIDE AU NINI ITASHINDWA TU.....SABABU NI TANESCO.

WACHA ZILIPWE TUZIME VIWANDA VYOTE........

 
ICC inaangalia mkataba ( Contract ) baina Ya Tanzania & Dowans na inaamua kufuatana na huo mkataba vipi unasema na haingalii kuwa kuna kipengele fulani ndani ya mkataba hakikubaliani na sheria za Tanzania sababu mkataba ume sainiwa na Tanzania au muakilishi was serikali ya Tanzania. Bora kulipa au tuombe mfadhili atulipie la sivyo tuta wakimbiza wawekezaji na labda hatutapata mikopo na misaada. Tunaweza kushi bila wafadhali wetu au wawekezaji ?

Am not going to pay a f@$%&*@#g dime!

Kama ni kuchelea kukosa sijui ufadhili mi nasema....screw wafadhili!

Huyo mlalahoi anafaidika na nini na these blood sucking wafadhili?
Sana sana anaishia kuchangia haya mabilion ya akina Dowans and who knows how many more "other Dowans" are in the pipeline?

Acha tuanze square 1. Ndiyo maana halisi ya mapinduzi, ebo!
 
Back
Top Bottom