Mahakama kuamua kama Mbowe ana kesi ya kujibu au hana leo Februari 18, 2022

beth

JF-Expert Member
Aug 19, 2012
3,877
6,326
1645171556976.png

Mahakama Kuu Divisheni ya Rushwa na Uhujumu Uchumi leo Februari 18, 2022 inatarajiwa kutoa uamuzi kama Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe pamoja na Washtakiwa wengine watatu wana Kesi ya Kujibu au Hapana

Februari 15, 2022 Upande wa Mashtaka katika Kesi hiyo ya Uhujumu Uchumi yenye Mashtaka ya Ugaidi inayowakabili Wanne hao ulifunga Ushahidi baada ya Shahidi wa 13 kumaliza kutoa Ushahidi wake

Mawakili wa Jamhuri waliomba Mahakama hiyo chini ya Jaji Joachim Tiganga kuona ikiwa Washtakiwa wana Kesi ya kujibu ili hatua nyingine zifuate
 
Leo ni leo , utatupa update miss, vipi iyo avatar, jina na ninaona kama vina uzuri flani ivi.
 
Nachokijua sio gaidi.

Hakuna ugaidi wa 600k kwenye nchi yenye watu Million 60.

Natamani Ziro na wenzie wapande kizimbani wavune walichokitengeneza wakidhani bado watanzania wote ni wajinga.
 
Mbona jibu lishajulikana tangu tamati ya makutano ya Ubelgiji.
Leo mapema tu, Mbowe ataachiwa huru kwa mahakama kutomkuta na hatia.
Hili lipo wazi kabisa......
 
Nachokijua sio gaidi.

Hakuna ugaidi wa 600k kwenye nchi yenye watu Million 60.

Natamani Ziro na wenzie wapande kizimbani wavune walichokitengeneza wakidhani bado watanzania wote ni wajinga.
Wenzake wamesha nyolewa atie maji kabisaaa🤯
 
Mbona jibu lishajulikana tangu tamati ya makutano ya Ubelgiji.
Leo mapema tu, Mbowe ataachiwa huru kwa mahakama kutomkuta na hatia.
Hili lipo wazi kabisa......
Wekeni akiba msijiaminishe mia kwa mia kwani hao jamaa sio mara zote wanachokisema ndio wanachokitenda. Kumbukeni waliomtengenezea hilo dude mwenyekiti wenu bado wapo kazini sidhani kama watakubali hilo goma liishe kirahisi rahisi maana yake itabidi wawajibike/wawajibishwe wao ili kulinda heshima ya mkuu. Ila kama hii ngoma amefosi McAlister,EU na watasha kwa ujumla wao mkuu atakuwa hana ujanja atatema bungo asubuhi tu mapema na mweyekiti wenu atakula "lunch" na familia yake.
 
Mahakama Kuu Divisheni ya Rushwa na Uhujumu Uchumi leo Februari 18, 2022 inatarajiwa kutoa uamuzi kama Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe pamoja na Washtakiwa wengine watatu wana Kesi ya Kujibu au Hapana

Februari 15, 2022 Upande wa Mashtaka katika Kesi hiyo ya Uhujumu Uchumi yenye Mashtaka ya Ugaidi inayowakabili Wanne hao ulifunga Ushahidi baada ya Shahidi wa 13 kumaliza kutoa Ushahidi wake

Mawakili wa Jamhuri waliomba Mahakama hiyo chini ya Jaji Joachim Tiganga kuona ikiwa Washtakiwa wana Kesi ya kujibu ili hatua nyingine zifuate
Watasema ana kesi ya kujibu ili waendelee kupiga per diem
 
Duh kwa mwenendo wa ile kesi na jinsi jaji alivyokua anatupilia mbali mapingamizi ya utetezi basi kama ni ku beti naweka 100k.. FAM ana kesi ya kujibu.
Binafsi sidhani kama serikali itakua tayari kuendelea 'kuvuliwa nguo' na upande wa utetezi kwa kuendeleza kesi, hii ngoma nadhani inaenda kumalizwa kiutu uzima tu, ili mambo yasiwe mengi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom