Mwanahabari Huru
JF-Expert Member
- Mar 9, 2015
- 14,243
- 34,899
Mahakama Kuu Kanda ya Dar Es Salaam imepanga kusikiliza Kesi ya Madai Na. 8/2018 iliyofunguliwa na chama cha ACTwazalendo dhidi ya Jeshi la Polisi kutokana na kuingilia shughuli za ziara ya chama. Kesi hiyo itasikilizwa Aprili 5, 2018.
========
Kesi za ACT Wazalendo Dhidi ya Jeshi la Polisi Kuanza Kusikilizwa Aprili 5.
Machi 18 tulizungumza na umma juu ya hali mbaya ya nchi Kiuchumi, na tukaeleza hatua ambazo kama chama tutachukua katika kutatua masuala kadhaa ya kinchi. Kwenye eneo la DEMOKRASIA tulieleza kuwa tumefungua Kesi ya Madai Na. 8/2018 Mahakama Kuu hapa Dar Es Salaam, kulishtaki Jeshi la Polisi, kutokana na Jeshi hilo kuingilia, visivyo halali shughuli za ziara yetu ya kuhamasisha maendeleo katika Kata tunazoziongoza.
Leo Mahakama imeipangia tarehe kesi husika, itasikilizwa kwa mara ya kwanza, Aprili 5, 2018 chini ya Majaji watatu, Jaji Ferdinand Wambari, Jaji Sameja na Jaji Rose Teemba.
Abdallah Khamisi
Afisa Habari, ACT Wazalendo
Machi 23, 2018
Dar Es Salaam
========
Kesi za ACT Wazalendo Dhidi ya Jeshi la Polisi Kuanza Kusikilizwa Aprili 5.
Machi 18 tulizungumza na umma juu ya hali mbaya ya nchi Kiuchumi, na tukaeleza hatua ambazo kama chama tutachukua katika kutatua masuala kadhaa ya kinchi. Kwenye eneo la DEMOKRASIA tulieleza kuwa tumefungua Kesi ya Madai Na. 8/2018 Mahakama Kuu hapa Dar Es Salaam, kulishtaki Jeshi la Polisi, kutokana na Jeshi hilo kuingilia, visivyo halali shughuli za ziara yetu ya kuhamasisha maendeleo katika Kata tunazoziongoza.
Leo Mahakama imeipangia tarehe kesi husika, itasikilizwa kwa mara ya kwanza, Aprili 5, 2018 chini ya Majaji watatu, Jaji Ferdinand Wambari, Jaji Sameja na Jaji Rose Teemba.
Abdallah Khamisi
Afisa Habari, ACT Wazalendo
Machi 23, 2018
Dar Es Salaam